Ushauri: Nimeitwa Polisi

Ushauri: Nimeitwa Polisi

Kachague selo!


Nimecheka sana
Kuna siku nilishuhudia jamaa kaenda pale anasema nimekuja niliitwa sasa nimekuja, akaulizwa unaitiwa nini akasema mimi sijui lakini nimeambiwa nahusishwa na wizi wa laptop, akaulizwa aliyekushitaki yupo wapi? Akasema sijui? Wakamwambia basi kaa hapo usubiri yeye akasema mm sina muda nina mambo yangu mengine kama yeye hayupo basi ile kabla hajamaliza akaambiwa hiyo haya vua mkanda, vua viatu, weka mazaga pale alafu kachague selo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cha kwanza, nenda jumatatu, usiende weekend hii fanya uwezalo waambie utafika kituoni jumatatu, pili unaitiwa mambo ya simu, hivyo hakikisha simu yako anzia sasa unaclear kila kitu yaani unachoona sio sawa clear it halafu weka simu yako password matata ambayo katu usiwape ilimradi kwa ridhaa yako wakitaka kitu au taarifa waambie, una haki ya faragha kisheria.( au nunua simu ya tochi weka laini yako)..zingatia ninachokuambia pia uende na ndugu au mtu mwingine au mwanasheria wako
 
Cha kwanza, nenda jumatatu, usiende weekend hii fanya uwezalo waambie utafika kituoni jumatatu, pili unaitiwa mambo ya simu, hivyo hakikisha simu yako anzia sasa unaclear kila kitu yaani unachoona sio sawa clear it halafu weka simu yako password matata ambayo katu usiwape ilimradi kwa ridhaa yako wakitaka kitu au taarifa waambie, una haki ya faragha kisheria.( au nunua simu ya tochi weka laini yako)..zingatia ninachokuambia pia uende na ndugu au mtu mwingine au mwanasheria wako
Ko nijipeleke yani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Najaribu kuwaza tu kimoyomoyo... hivi anayeona namba ninazowasiliana nazo si yule service provider wangu tu tena ni privacy yangu!? Ilimradi tu sivunji sheria basi me ningemshtaki huyo anayesema amehack mawasiliano yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu

Kuna ushauri ametoa TheSpam nadhani ni issue ya simu maana kuna mshkaji wangu mmoja tulienda nae kununua Tecno Cammon X kwenye madukavwanayouza simu used kipindi cha nyuma na ndo anayo mpaka sai

Na kweli huwa tunawasiliana sana maana ndo mshkaji wangu mno Asa kwa mantiki hii nafanyaje?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
We jamaa, Kesho ipigie hiyo number ya aliyejitambulisha ni Polisi, mwambie uko far na utafika kituoni J3. Mwambie J3 aje akuchukue kwenye ofisi ya serikali ya kijiji.

Weka line yako Kwa simu ya kitochi, J3 asubuhi kamtaarifu kiongozi wa mtaa/kijiji scenerio yote, ili hao Polisi waje wakuchukulie Kwa Mkiti. Hakikisha upo na nduguyo ili ikitokea shitaka akuwekee dhamana.

Usiwakimbie Polisi, na Acha woga. Shits happen n life guy!!

Hakikisha huna msala!

NB: huyo msela unayehisi anatafutwa usimjuze chochote! Kama huna Roho ya narco sicario!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii inshu waweza uichukulie poa
Ila kusema ukweli kupigiwa simu ya kiofisi na police nakukuita kituoni ni shughuli nyingee

Mm walishawahi nipigia japo ile najiandaa niende wakaniambia samahani tumekosea una bahati sanaa.

Aloo nili haha sanaa
Niliwaza kila kitu lakn sioni nilipo na kosaa

Nilitrace miaka miwili nyuma sioni kosa ila naogopa.

Polisi wakikupigia simu tuu jua huna pakutokea wakiamua, labda km wanaona uhitaji wao kwako sio mkubwa sanaaa wakiona unawasumbua na huna msaada mkubwa wanakupotezea.

Tena washakuambia hao n watu wa Cyber

Amini usiamini, wanamawasiliamo ya watu angalau watano unaowasiliana nao mara kwa mara,
Kwenye hio kesi ya mshkaj wangu niliyosema hapo juu, nae walimuita akagoma
Wakanipigia mm, nikaongea na mshkaji akagoma,
Wakampigia baba yake, baba akampigia mwanae ndio mshkaji akaenda, tunafika wakamweka ndani kwa usumbufu.

Mkuu nakushauri sana nenda mzee nendaaa....
Wana angalau nusu ya details zako zote ndio maana wanajiamini kukupigia

Nenda mzeee


Ila twaweza ongea hapa kumbe una siri zako,
Kama una msala mzito mzee USIENDEEEEEE
Japo unazidi kuharibu ila sikushauri
Mm nikiwa na msala mkubwa haki nahama nchi
Kule mahali sipoooo

Kitu cha kwanza kikubwa achana na yote Ni TB.
Hii kitu asilimia kubwa wanaoenda selo wanatoka nayo

Ni hayo tuu
 
Nilishawambia watu wote wa karibu yangu akinunuwa simu used likitokea suala la kuitwa polisi ama kukamatwa Mimi sitakuwa na huruma ya kwenda kumuona huko polisi
Maana nikupotezeana muda kwa mambo ya kijinga kabisa !
 
Kuna jambazi/mhalifu unawasiliana naye au mtu wako wa karibu?

Aliyekuita alijitambulisha vipi na wewe unamwamini vipi kuwa ni polisi na si tapeli au mwenye nia mbaya na wewe?

Kama upo ok chukua mtu wa kukusindikiza ambaye atakuwa nawe in case of anything. Ili ukatoe ushirikiano kwa kile unachokifahamu.chukua jina la askari husika na namba yake. Nenda kituoni uliza kama kuna mtu mwenye jina na namba hiyo.then waambie amekuita kwa simu unataka onana naye ukiwa na mtu amekusindikiza na umeoa taarifa kwa watu wa karibu.

Then waoneshe ushirikiano.

Kama unatembea na mke wa mtu na chats zenu zimeonekana ni issue ujue. Ombea mwenye mke asiwe karibu akakuona na jinsi ulivyokuwa ukitamba kwenye chats kwa kumkunja mkewe pasipo huruma.
Hiyo paragraph ya mwisho hiyo. Hizo chats zao zitaonekana wapi mkuu?. Kwa wahusika kama voda,airtel,tigo? Au kiaje mkuu?. Kama ni kwa mtandao hiyo nao si watakuwa na kesi ya kujibu. Kumpa mtu mwingine deteries za mwingine?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiona polisi wanafikia hatua ya kukuita basi jua wana details zako zote na wameona wasisumbuke kukutafuta.

Mwaka jana hii iliwahi kunitokea nilipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni askari wa kituo kimoja hapa dar, akanitajia hadi kazi yangu akaniambia nijisalimishe mwenyewe centl nikaweka mgomo jamaa kila siku ananipigia kuwa niende nimalize msala nikagoma.
Aise siku moja mida ya saa moja jioni ndani ya wiki hiyo hiyo nimekaa zangu ndani sehemu napiga story nashangaa zinatokea jemba mbili zimeshiba zikajitambulisha wakaniambia dogo ulijifanya mjanja sana.

Aise nikapandishwa ndani ya Noah nyeusi mpaka kituoni nililala huko kesho nikapata dhamana jamaa aliyenikamata baadae tukawa kama marafiki ndo akanipa mkanda mzima watu niliokuwa nawasiliana nao,nyumba ninayoishi ndugu zangu mpaka demu wangu anamjua.

Jamaa akaniambia ukiona wamefikia hatua ya kukuita wajua kuwa huna pa kutokea hata kama utavunja simu na kubadili laini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dogo kama ulinunua simu mkononi usiende vunja line na simu ipasue uendelee na mambo yako vingunevyo utapewa kesi ya mauaji na itakutoka zaidi ya M kadhaa kusawazisha mambo

Sent using Jamii Forums mobile app
Wadau wamezungumza mengi na ushauri,kaa tuliza akili ikiwezekana shirikisha mtu wako wa karibu na toa taarifa kwa kiongozi wa mtaa wako,,inaonekana shida sio kubwa maana wangekuja bila wew kujua,,wakakuchukua mpaka ofisini,,lakini wameweka bayana kuwa kuna namba unawasiliana nayo,,hapa napo kupaamini ni shida kidogo,, yaweza kuwa njia rahisi ya wao kukupata wakuaminishe hivo ili wakupate kirahisi,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom