Ushauri: Nimeitwa Polisi

Ushauri: Nimeitwa Polisi

Kwa hiyo nitoe hii line waliotumia kunipigia au

Sent using Jamii Forums mobile app
Ikiwezekana hata simu badili kabisa!
Hawachelewi kukwambia unawasiliana na jambazi aliyetafutwa toka 2017.

Polisi, kuna michezo mingi sana kwa raia, kuikwepa ni vigumu mno hasa wanapozihitaji pesa! Raia wengi tunaishi kwa kudra za Mungu tu.

Ila nawe uwe unajijua ni msafi kimatendo, kama unahusika kwa mikasa ya kihalifu, basi ujue utanaswa tu. Maana hata ubadili simu na laini, ila kama bado unaendelea kuwasiliana na mhalifu, watakupata tu.

Serikali yetu ina mkono mrefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu bwana......wanavyokazania uende na advocate (by the way Kuna tofauti Kati ya Mwanasheria na wakili.....advocate and a lawyer) utafikiri tupo Washington DC USA......

Hapa Ni Africa, Tanzania...... Kama huwaelewi choma line, tupa simu au muuzie mtu msala ukitokea umuangukie ..... Kama umepanga rum moja hama leo leo.....

Jeshi la Polisi Tanzania bado mno.......watakupotezea muda wako,kipato na wakimalizana na wewe Heshima kwenye jamii inayokuzunguka huna.
 
Ikiwezekana hata simu badili kabisa!
Hawachelewi kukwambia unawasiliana na jambazi aliyetafutwa toka 2017.

Polisi, kuna michezo mingi sana kwa raia, kuikwepa ni vigumu mno hasa wanapozihitaji pesa! Raia wengi tunaishi kwa kudra za Mungu tu.

Ila nawe uwe unajijua ni msafi kimatendo, kama unahusika kwa mikasa ya kihalifu, basi ujue utanaswa tu. Maana hata ubadili simu na laini, ila kama bado unaendelea kuwasiliana na mhalifu, watakupata tu.

Serikali yetu ina mkono mrefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sina mawasiliano yeyote ya kiuhalifu kaka
Ingekua ni hivo wala nsingeomba ushauri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wakuu

Nimepokea simu kutoka kwa mtu anasema yuko central kitengo cha cyber na kuna namba inaonekana naongea nayo na wanataka kujua machache kuihusu
Nimewauliza ni ipi niwajibu? wamekataa wamesema niende central au niwaambie nilipo wanifate nimewajibu ntaenda kesho

Hasa hapa najiuliza niende au? maana polisi wetu hawaaminiki unaeza fika yakawa mengine

Ushauri


Sent using Jamii Forums mobile app
simu yako ulinunua wapi dukani au mkonani
 
Nchi hii uonevu na ugandamizaji umekithiri. Hivi inakuwaje mtu aitwe polisi amekwenda pasi na shaka, akahojiwa mawili matatu akajibu na ikabainika kwamba mtu huyo hana shida sana,iweje aambiwe vua viatu,mkanda zama ndani? Kwa nini asiendelee kutoa ushirikiani huku akiwa nje na shughuli zake za kila siku? Hii nchi raia akiitwa polisi pasipokujali alichoitiwa 99% ana uwezekani Wa kuwekwa ndani
Wakutendee wema wote huo halafu wao wakale wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sina msala kaka yani sijui hata nini shida

Sent using Jamii Forums mobile app

Binadamu tuna siri sana, inawezekana hata mmoja wa rafiki zako mnayewasiliana nae sana ana mambo yake ya siri ambayo wewe huyajui kuwa anafanya kama ugaidi, wizi, utapeli n.k ila hapa nnahisi ni simu ya wizi inatumika kukupigia sasa kama inaonekana anawasiliana na namba yako sana lazima wakuite wakuhoji kuhusiana nae, obvious hawana shida na wewe kwa maana wakikutaka wanakupata fasta, hawataki kupoteza resource
 
Habari wakuu

Nimepokea simu kutoka kwa mtu anasema yuko central kitengo cha cyber na kuna namba inaonekana naongea nayo na wanataka kujua machache kuihusu
Nimewauliza ni ipi niwajibu? wamekataa wamesema niende central au niwaambie nilipo wanifate nimewajibu ntaenda kesho

Hasa hapa najiuliza niende au? maana polisi wetu hawaaminiki unaeza fika yakawa mengine

Ushauri


Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu wala usiende,acha wafanye kazi yao ya kùkutafuta wakukamate,utajipelekaje polisi na wewe?,endelea na kazi zako mpaka watakapokukamata sio wewe ujipeleke,ukijipeleka hakutapunguza makosa kama yapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom