Gentlemen_
JF-Expert Member
- Nov 24, 2019
- 3,563
- 10,553
Huu wimbo uliachiliwa Mwaka 2001, katika albam yake ya Machozi, Jasho na Damu.
Nitachambua na kuunganisha na Matukio ya sasa ambayo enzi hizo yalikuwepo ila baadhi ya watu wanayafanya kama ni mambo mapya... na uzuri huyu PROFESA Alichimba ndani sana..
1- Ushoga
2- Umalaya na Kuuza Miili
3- Tabia za watanzania za kuponda starehe pale akipata vihela
na Mambo mengine mengi..
Twende nami..
" Subiri kichapo chake pale mbongo anapozipata
Mwendo wa kiti kirefu jirani na nyama choma
Na toto mbili tatu za geti au za kona"
Huu utaratibu bado tunaendelea nao mpaka hii leo watu wanaenda ktk maeneo ya starehe huku wamezungukwa na wachumba kwenye meza wakitusua manyama na unywaji wa pombe za kutosha..
neno Toto mbili tatu za geti au za KONA... nafkiri biahsara ya uuzaji Utamu maeneo ya Sinza pale Kona Bar ni wa muda mrefu miaka 22+
"Pitia pitia night kali mitaa ya Kinondoni
Kina dada poa nusu uchi fegi mdomoni
Na kama una gari watajazana madirishani wee
Mpaka ukose hewa wote wanataka hisani"
Hapa tunaona Biashara ya uuzaji miili ndani ya DSM ni ya kitambo, hivyo yale malalamiko ya mara kwa mara humu kanakwamba ni jambo jipyaa mie nafkiri baadhi ya watu (Wakuja/Wamikoani) hivi vitu kwao ni vipya.
"Mpaka bibi vizee sasa wanafanya ukahaba"
Mnajionea wenyewe PROFESA anazidi kutuhabarisha ndani ya mwaka huo 2001 mabibi pia walikuwa wanauza miili...
"Vijana wamejibana wapate mtaji wa biashara
Nawaita machinga ingawa sio wote kutoka Mtwara
Mbaya kuliko vyote mnapovunja vibanda vyao
Wengine walikuwa wezi, je warudie zama zao?"
Hapa aligusa jamii.. hasa ya wafanya biashara kuhusu vita yao na serikali.. hi vita ni ya miaka nenda rudi.
"Wabongo wanapenda sana starehe kuliko kazi
Wanatamani wangezaliwa Blue Nay wamwage radhi"
Nyuzi nyingi hata humu JF zinahusiana na Mapenzi na Ngono pamoja na starehe zingine hii inasadiki na ni tabia ya WABONGO mpaka hii leo huu utaratibu wa kupenda starehe upo.
"Mablaza majina yao ya asili hawayataki
Bitoz Nyangema anataka aitwe Tupac!"
Wacha tufanye utafiti wa Majina ya members humu jee wana majina ya Asili? hii ni tabia ya kitambo sana tunaona hapo baadae kizazi hiki kinachokuja hakitakuwa na majina ya Asili tena.
"Funga mkanda, fungua mabano unavyotaka"
anayejua maana ya hii vesi anijulishe........!
"Sinza ya leo, kila baada ya nyumba bar
Na zote zinajaa, hapo ndipo utakaposhangaa
Na kwenye night club ni lundo la kaka poa
Huwezi ukaamini jinsi walivyojipodoa"
Kama mnavyoona hapo ishu ya USHOGA ipo na ilikuwepo ingawa sahivi watu wanaipa sana airtime kama vile ni jambo jipya ktk jamii.. kuna nyuzi za kuigusia SINZA za hivi karibuni watu wanaijadili Sinza kama ni sehemu iliyoharibika hivi karibuni.. kumbe ndio sehemu iliyochachuka miaka na miaka.... ni ASILI ya hilo eneo.
"Na watu wana magari mpaka ya milioni 200"
Hapa watu wanashangaa Mhe MSUKUMA kuvuta chuma cha mil 400+ hali ya kuwa mwaka 2001 huko watu walimiliki vyuma vya mil 200.. unaweza kufikiri ni jinsi gani watu walikuwa na hela ukizingatia mfumo wa ujamaa ulikuwa bado una vimizizi kipindi hicho.
Huyu Jamaa PROF JAY ni kichwa.. na ni msanii mbunifu na mwenye uwezo mkubwa wa uandishi na kupangilia ngoma ambazo zitaishi miaka mingi. huu wimbo ni kama umetoka mwaka jana.
JIONI NJEMA....
Nitachambua na kuunganisha na Matukio ya sasa ambayo enzi hizo yalikuwepo ila baadhi ya watu wanayafanya kama ni mambo mapya... na uzuri huyu PROFESA Alichimba ndani sana..
1- Ushoga
2- Umalaya na Kuuza Miili
3- Tabia za watanzania za kuponda starehe pale akipata vihela
na Mambo mengine mengi..
Twende nami..
" Subiri kichapo chake pale mbongo anapozipata
Mwendo wa kiti kirefu jirani na nyama choma
Na toto mbili tatu za geti au za kona"
Huu utaratibu bado tunaendelea nao mpaka hii leo watu wanaenda ktk maeneo ya starehe huku wamezungukwa na wachumba kwenye meza wakitusua manyama na unywaji wa pombe za kutosha..
neno Toto mbili tatu za geti au za KONA... nafkiri biahsara ya uuzaji Utamu maeneo ya Sinza pale Kona Bar ni wa muda mrefu miaka 22+
"Pitia pitia night kali mitaa ya Kinondoni
Kina dada poa nusu uchi fegi mdomoni
Na kama una gari watajazana madirishani wee
Mpaka ukose hewa wote wanataka hisani"
Hapa tunaona Biashara ya uuzaji miili ndani ya DSM ni ya kitambo, hivyo yale malalamiko ya mara kwa mara humu kanakwamba ni jambo jipyaa mie nafkiri baadhi ya watu (Wakuja/Wamikoani) hivi vitu kwao ni vipya.
"Mpaka bibi vizee sasa wanafanya ukahaba"
Mnajionea wenyewe PROFESA anazidi kutuhabarisha ndani ya mwaka huo 2001 mabibi pia walikuwa wanauza miili...
"Vijana wamejibana wapate mtaji wa biashara
Nawaita machinga ingawa sio wote kutoka Mtwara
Mbaya kuliko vyote mnapovunja vibanda vyao
Wengine walikuwa wezi, je warudie zama zao?"
Hapa aligusa jamii.. hasa ya wafanya biashara kuhusu vita yao na serikali.. hi vita ni ya miaka nenda rudi.
"Wabongo wanapenda sana starehe kuliko kazi
Wanatamani wangezaliwa Blue Nay wamwage radhi"
Nyuzi nyingi hata humu JF zinahusiana na Mapenzi na Ngono pamoja na starehe zingine hii inasadiki na ni tabia ya WABONGO mpaka hii leo huu utaratibu wa kupenda starehe upo.
"Mablaza majina yao ya asili hawayataki
Bitoz Nyangema anataka aitwe Tupac!"
Wacha tufanye utafiti wa Majina ya members humu jee wana majina ya Asili? hii ni tabia ya kitambo sana tunaona hapo baadae kizazi hiki kinachokuja hakitakuwa na majina ya Asili tena.
"Funga mkanda, fungua mabano unavyotaka"
anayejua maana ya hii vesi anijulishe........!
"Sinza ya leo, kila baada ya nyumba bar
Na zote zinajaa, hapo ndipo utakaposhangaa
Na kwenye night club ni lundo la kaka poa
Huwezi ukaamini jinsi walivyojipodoa"
Kama mnavyoona hapo ishu ya USHOGA ipo na ilikuwepo ingawa sahivi watu wanaipa sana airtime kama vile ni jambo jipya ktk jamii.. kuna nyuzi za kuigusia SINZA za hivi karibuni watu wanaijadili Sinza kama ni sehemu iliyoharibika hivi karibuni.. kumbe ndio sehemu iliyochachuka miaka na miaka.... ni ASILI ya hilo eneo.
"Na watu wana magari mpaka ya milioni 200"
Hapa watu wanashangaa Mhe MSUKUMA kuvuta chuma cha mil 400+ hali ya kuwa mwaka 2001 huko watu walimiliki vyuma vya mil 200.. unaweza kufikiri ni jinsi gani watu walikuwa na hela ukizingatia mfumo wa ujamaa ulikuwa bado una vimizizi kipindi hicho.
Huyu Jamaa PROF JAY ni kichwa.. na ni msanii mbunifu na mwenye uwezo mkubwa wa uandishi na kupangilia ngoma ambazo zitaishi miaka mingi. huu wimbo ni kama umetoka mwaka jana.
JIONI NJEMA....