we are not interested in these cheap F4F , internal wranglings za CHADEMA.
Leteni mambo ya kitaifa hapa,
QUOTE=Mshombsy;7723170]
Maelezo ya Lema juu ya CHADEMA kuwafukuza wanafiki kwa kufanya maamuzi magumu ni ya kutafuta kuungwa mkono na wanachama wa CHADEMA, sioni ubaya kabisa kwa kusema ndani kuna wanafiki. Wale wanaosema angeongelea kwenye vikao nadhani ameonyesha kutekeleza ilo kwa kusema chama kifanye maamuzi magumu hata kama 2015 hawatashika dola lakini watakuwa wamebadilisha watu fikra.
Maelezo yake hayatofautiani na Zitto aliposema Kuna mbunge wa upinzani anadai kuwekewa kauzibe kwenye posho. Na hii mngesema basi Zitto angeitolea kwenye vikao vya chama na si kwenye majukwaa ya kijamii.
Zitto aliitoa ili apate huruma ya jamii kwasababu inagusa jamii. Lema hapa ni kwa wanaCHADEMA suala la wanafiki litakapofika kwenye chama.
Niseme tu kwamba namuhusudu Zitto kwa ujasiri wake wa kupambana lakini anashindwa kuelewa lengo la yeye kuwa mpinzani ni nini na kwanini yuko CHADEMA.
Ninaachokiona kwa watu hawa wawili hasa upande wa Zitto ni kuwinda pointi za kisiasa zaidi kuliko kupeperusha itikadi ya chama. Itikadi ina umuhimu kwenye chama kwani ndo inatoa mwelekeo na inaunganisha wanachama.
Hivyo lazima itikadi itetewe, ifagiliwe na itafutiwe pointi za kisiasa ili kuvuta watu zaidi kwenye chama na hii ndo lengo la Lema. Zitto anaenda kinyume ni yeye tu yani anamwangalia Zitto atoke vipi. Kwa mambo yanayogusa maslahi ya umma ni vizuri kuwa na msimamo wa ki-chama.
Ukianzia suala la posho, kukaguliwa na CAG ni wazi Zitto mbali ya kuwa naibu katibu hakuwahi kuhuliza chama chake msimamo juu ya posho na kama kimekamilisha hesabu kwa mujibu wa taratibu kabla ya kulifikisha mbele ya kamati za bunge.
NI KWANINI ALILIPELEKA SUALA LA HESABU KAMATI YA BUNGE? Anajua kabisa kwamba maono ya wengi ni kwamba CHADEMA ni cha wenyewe, yeye anatengwa kitu ambacho si kweli, alijua kabisa watu watasema jamaa wa Kanda ya kaskazini hawajakamilisha hesabu na kuna kitu hapo. Lengo lake lilifanikiwa.
Utategemea Naibu katibu mkuu ahakikishe Chama chake kinakamilisha hesabu ili kisimwaribie uhadilifu wake mbele ya wanakamati, hiyo miaka yote alisema hawawakilishi hesabu alikuwa haudhulii vikao na kuuliza kama walishawakilisha kwa Msajili? Ni kucheza na fikra za watu "chama cha kikanda, chama cha wenyewe". Na anaelewa kabisa mwisho wake ungekuwa hivyo. Mahojiano na clouds fm alisema ikifika zamu ya CHADEMA yeye hatakuwa mwenyekiti wa kikao cha kamati kuondoa mgongano wa kimaslahi. Hii inaonyesha anajua yeye ni CHADEMA, kwanini hakuwapelekesha wahasibu wa chama na viongozi wenzake kulinda heshima ya chama ambacho ye ni kiongozi.
Tukirudi kwenye suala la posho hivi hawakuitana wabunge wa CHADEMA kabla ya kikao cha bunge na kuwa na uhamuzi wa pamoja?. Lakini akasimama mwenyewe na kusema hataki posho. Ikalazimu Chama kutoa taarifa badae kumuunga mkono juu ya posho.
NANI AMESIKIA WABUNGE CCM NA WINGI WAO WANAKATAA POSHO HATA MABILIONEA KAMA MO DEWJI? Hakuna. Wali-caucus na kuja na uhamuzi wa pamoja kwa manufaa ya chama wa kuunga mkono posho. Kama ingewazamisha ni wote si mmoja mmoja.
Hii ndo ilikuwa hoja ya Lema kwa kila nafasi mtu aliyonayo awe mbunge, mwanachama au kiongozi ni kukipigania chama, kukipa pointi za kisiasa, kujua lengo ni chama kuchukua dola, kuvutia wanachama
Inawezekana lugha ya Lema haikustahili lakini ujumbe wake ni kwa watu kujitambua kwanini ni wapinzani na kwanini wako chama fulani.
Natambua Zitto analitumikia taifa kama mbunge lakini haiondoi wajibu wa kukikuza chama kwa hoja za pamoja.
Hatutaki kumpa mtu urais alafu aanze kutafuta pointi za kisiasa za jumuiya ya Afrika Mashariki.[/QUOTE]