Hivi unafikiri lema kulalama humu kuna saidia kumuondoa mnafiki kwenye chama zaidi ya kuendeleza malumbano yasiyo na tija? hivi kwanini lema aoneshe kuwa chadema kina lea wasaliti? kwanini asipeleke ushahidi wake kwenye vikao vya chama.
mwigamba alitumia id fake, lema ametumia id yake mwenyewe.
Na ili tusirudi huko ni lazima tuchukue different approach ku-deal na elements zinazofanana na zile zilizoiua NCCR-Mageuzi.Ndiyo falsafa ya kumtoa nyoka mdogo ndani
It ain't over 'til it's over.Game over!!!!!!
Ukitaka kutenda haki kwanini usiiweke na hii https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-dhambi-dhambi-ni-posho-inapokosa-utu-16.html au na wewe ni kati ya alio wataja....Mkuu Lema, pengine utusaidie kutupatia maana halisi ya 'Usaliti', 'Unafiki' na 'utu' kwa namna uelewavyo wewe.
Maneno haya kutoka kwako yananishangaza kidogo, kwa vigezo kuwa kwa yale unayofanya nawewe unaweza fuzu kuitewa Mnafiki na Msaliti asie na utu. Labda kama unatumia hii njia kujikosha baada ya wewe pia kutambua kuwa umeonyesha Usaliti mkubwa kwa Watanzania unaowawakilisha.
Lema inatakiwa uelewe haya;
Unatakiwa kujua kuwa hata kina KUBENEA wameshakuchoka, yeye si mmoja wa hao anaowasema? (Au woga ambao siku zote unashabikia ni sumu leo si sumu tena?), pitia hii https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/547535-mh-lema-anaivuruga-chadema.html
Watanzania wengi washakushtukia, unakiruvuga chama kwa siasa zako za kishabiki na kitoto wenzetu wanaita 'armature' (an insult ukiichukulia undani wake) pitia hii https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...gwe-gavana-rahisi-kusababisha-mitafaruku.html
Inawezekana unawashambulia Shibuda na Zitto kwenye bandiko hili, vipi ni kwakuwa wewe Lema unapenda sana Posho hivyo umeamua liwalo na liwe? pitia hii https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...bungeni-zitto-lema-katika-vita-ya-maneno.html
Au unataka kusema hizi posho zinamaanisha Uzalendo na Utu kwa Taifa? (Are you serious??). Zitto alisha litabiri hili na kueleza wazi (hakutumia unafiki) kuwa Siasa za Posho zitasababisha mjenge chuki na mmwite majina yote mabaya! www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/299635-zitto-sijahongwa-ni-siasa-za-urais-na-hasira-za-posho.html
Au hii ndiyo step ya kwanza ya kufanya Zitto aondoke Chadema? Maana inajulikana wazi kuwa kuna mkakati wa kumkatisha tamaa Zitto aondoke CHADEMA mapema kabla mwaka haujaisha ili mpumue ndani ya chama cha watu wa Kaskazini (viongozi wa juu). Inaturudisha kule kule mnako kukataa siku zote (Udini/Ukabila).
Pole zako Lema, watanzania wa leo si mabwege!
hawezi kwani wanayemtuhumu ndio anasimamia ukweli, katiba na maamuzi ya vikao vyao......kasimamia kutochukua posho, wakati wanachadema wabunge wote walisema hawatachukua posho
Katiba yao imebakwa na adui yao mkubwa aliyebaki ni zittto akna kafulila, shonza, mtela, mwigamba, marehemu wangwe n.k wooote waliondoka na same tuhuma juu ya CDM, si chama cha wanachama ni cha watu wachache na ubabe wao na nguvu yao
Itakuwa raha kwa uongozi wa sasa wa chadema kufanya lolote kumuondoa zitto kabwe ambaye anasimamia haki na ukweli......wakimwondoa wanapata raha,
Lema anaona kila mtu mjinga humu ANAJIANIKA VIBAYA SANA, na zitto yuko mioyoni mwa watu wapende wasipende.............matatizo yote ya nchi hii Lema anakuja na wasaliti wa taifa na chama
wasaliti nyie msiofanya uchaguzi kihalali na kupoteza matumaini ya wataka mabadiliko, CDM ni mbaya sana kuliko CCM at this point na view..................WATU WAZURI WOTE WALIO NDANI YA CDM wanaoisaidia jamii na taifa ndio wabaya wa CDM....something is wring here
Chacha wangwe alitaka ubia wa wananchi na ule mgodi wa dhahabu musoma, akasimamia hoja na kupinga ndani ya CDM na akaishia kufa............SOMETHING IS WRONG HAPA
Wapi kaburu...Msimamo wa mbowe,slaa ni kuwa zitto ni msaliti. Hawawezi kumfukuza na wakiitsha uchaguzi huru na haki ztto anachukua kitengo. Ukweli mchungu ni kuwa zitto akfukuzwa chadema ndo mwsho wa wanachadema wenye akili kuwa cdm.watabaki wapuuzi tu na misukule
Lawyer,
It is unfortunate wewe siyo mhudhuriaji sana wa hili jukwaa, ama we ni msomaji zaidi ya mchangiaji. Kama unavyoelewa kuna mada nyingi dhidi ya Lema siku za hivi karibuni, ambayo ilitaka kugeuza taswira sahihi na watu wakauamini uwongo kuwa ukweli.
Lema hajamtaja mtu, bali ametoa hili kama angalizo kwa chama akiwa verified. ni kweli kwamba hakumjua leo huyu msaliti.
Kwa kufanya alichokifanya Lema jamii inajua Lema ni mtu wa namna gani. Kukaa kimya wakati mwingine jamii inaweza kuaminishwa tofauti na ukweli.
Alichokifanya Lema ni kutoa elimu kwa jamii kuwa wanafiki na wasaliti siyo wakuvumiliwa hata kidogo. wanatakiwa kuondolewa kabla hawajaleta madhara. Ni jukumu la chama sasa kuchukua hatua.
Kuleta hii mada humu inasaidia jamii hasa GTs kutoa maoni yao juu ya hatua inayotakiwa kuchukuliwa dhidi ya wasaliti mahali popote siyo tu chadema, bali hata kwenye taasisi zingine za kujamii