Nimefuatilia mjadala sana leo ukizingatia ilikuwa ni Jumamosi kwamba hatukuwa na kazi nyingi sana za Kibunge hasa baada ya kuanzisha mjadala unaosema " Usaliti na Unafiki unavyoliangamiza Taifa " na nimeona mjadala na nimejifunza mambo mengi sana sikumtaja Mtu ila Watu wengi wametaja majina ya Watu , sijui kwanini ? ila naendelea kutafakari , kesho nitaandika kuhusu mada inasema " UNAFIKI WA ZITTO KUHUSU POSHO " na mpaka saa nane mchana nitakuwa nimewasilisha na jambo hili halina mgogoro na kanuni za Chama kwani ni jambo liko wazi kwenye vyombo vya habari .
Asanteni
Mheshimiwa Lema,
Naamini wewe ni mtu mwenye busara na ndio maana wananchi katika jimbo lako wamekupa dhamana ya kuwawakilisha Bungeni. Hivi kwa busara zako, hayo malumbano mnayoendeleza hapa JF ilhali mna vikao mwafaka ndani ya chama ni kwa manufaa ya nani?
Kwa sie ambao angalau tunaafikiana na harakati zenu za kuikomboa Tanzania kutoka katika lindi la umasikini unaorutubishwa na ufisadi, tabia hii ya kugeuza social media kuwa kumbi za kujadili masuala mnayoweza kuyajadili ndani ya chama inatuvunja moyo sana.
Pamoja na kutofautiana kwangu na Zitto katika masuala mbalimbali, napingana nawe kwa nguvu zote katika uamuzi huu ambao naomba uniruhusu kuuita usio wa busara hata chembe wa kujadili tofauti zenu za kimtazamo mtandaoni.
Majuzi niliandika makala hii
Makala yangu Ktk RAIA MWEMA Toleo la Okt 30, 2013: "CCM Itang'oka, Chadema Itaweza Kuongoza?" ~ Kulikoni Ughaibuni ambayo awali ilichapishwa kwenye jarida la
RAIA MWEMA na moja ya maswali niliyouliza ni utayari wenu kuongoza Tanzania pindi CCM iking'oka madarakani.
Haihitaji darasa maalum la uongozi kutambua kuwa malumbano ya hadharani baina ya viongozi wa ngazi za juu wa chama chochote kile hayajengi, regardless ya mantiki ya mada husika.
Mmekuwa mkilalamika kuhusu hujuma mnazofanyiwa na CCM na taasisi za dola, na wengi tuliwaunga mkono kwani ili demokrasia ya kweli ifanye kazi thabiti shurti kuweke level field. Lakini yayumkinika kuhitimisha kuwa kwa mwenendo huu wa kujibishana kwenye mitandao ya jamii, adui yenu mkubwa kwa sasa ni ninyi wenyewe. Tofauti zenu za kimitazamo zinaweza kujadiliwa na hata kumalizwa ndani ya vikao husika, if not katika maongezi binafsi as viongozi wa chama kimoja.
Hebu jiulize, pamoja na uselessness yao na hata kukinzana kwao, when did you see Nape na Lowassa wakija JF 'kuonyeshana ubabe'? Si kwamba hakujawa matukio yanayoashiria bayana uwa wanasiasa hao 'picha haziivi' lakini angalau wana akili na busara za kutambua kuwa tofauti au hata uhasama wa kisiasa shurti viandane na kuthamini maslahi ya Chama chao.
Huu ni ushauri wa bure tu lakini una haki ya kuupuuza. Nimalizie kwa kukuuliza, hiyo kesho ukishatundika kuhusu 'Unafiki wa Zitto kuhus posho' itakisaidia vipi chama chenu katika harakati za kuing'oa CCM hapo 2015?