Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,685
- 29,897
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ametamka wazi akiweka angalizo la uwepo wa wakimbizi ( niseme WAHAMIAJI) kwenye teuzi tena level za maamuzi ndani ya nchi yetu.
Nimeona wachambuzi mbalimbali wakimpongeza kwa kuweka wazi angalizo hilo. Nimemsoma mtani wangu kisiasa Yericko Nyerere akichambua kwa undani maeneo ambayo ujasusi umetamalaki na namna ufundi mkubwa uliofanyika kufifisha kila juhudi ya Taifa kujikwamua
Pamoja na kumpongeza CDF Nkunda, lakini tujitathmini kama Taifa kwamba tumefikaje hapa.. Mamlaka ya uteuzi imeainishwa kwenye Katiba yetu. Tumezoea utamaduni wa viongozi wakuu kuvunja Katiba kama vile kufanya teuzi bila kuzingatia vettings. Unaweza kukuta vetting imefanyika lakini inatupiliwa mbali.
Chama Cha Mapinduzi kimejitwalia mamlaka makubwa zaidi na hatima ya Taifa wameifumbata mikononi mwao. Sasa linapokuja suala la teuzi ama kushinda chaguzi mbalimbali, Chama huamua nani ashinde ama ateuliwe. Hivyo angalizo la CDF limeivua ngup CCM na Mwenyekiti wake kwa kuonesha namna gani wanavyojali maslahi yao zaidi ya maslahi ya Taifa.
Imefika mahala, inapotamkwa ama kuelezewa hoja ya USALAMA WA TAIFA inamaanisha usalama wa CCM hususan nafasi za juu za utawala.
Ushahidi wa haya ni namna ambavyo Katiba na hususan sheria ya uchaguzi inavyovunjwa wazi wazi kwa kufanya kampeni kwa mgombea wa CCM wakati kipenga cha uchaguzi hakijapulizwa bado.
Wakimbizi kuteuliwa na kuwekwa kwenye nafasi za maamuzi ya nchi ni jambo hatari sana kwa usalama na ustawi wa nchi yetu.
Tujitathmini, tuchukue hatua kusahihisha hili kosa kubwa.
Ninapata hisia kuwa yule aliyeamrisha jeshi kufanya usafi tarehe 24 anaweza akawa kaguswa na tamko hili.
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki JamiiForums
Nimeona wachambuzi mbalimbali wakimpongeza kwa kuweka wazi angalizo hilo. Nimemsoma mtani wangu kisiasa Yericko Nyerere akichambua kwa undani maeneo ambayo ujasusi umetamalaki na namna ufundi mkubwa uliofanyika kufifisha kila juhudi ya Taifa kujikwamua
Pamoja na kumpongeza CDF Nkunda, lakini tujitathmini kama Taifa kwamba tumefikaje hapa.. Mamlaka ya uteuzi imeainishwa kwenye Katiba yetu. Tumezoea utamaduni wa viongozi wakuu kuvunja Katiba kama vile kufanya teuzi bila kuzingatia vettings. Unaweza kukuta vetting imefanyika lakini inatupiliwa mbali.
Chama Cha Mapinduzi kimejitwalia mamlaka makubwa zaidi na hatima ya Taifa wameifumbata mikononi mwao. Sasa linapokuja suala la teuzi ama kushinda chaguzi mbalimbali, Chama huamua nani ashinde ama ateuliwe. Hivyo angalizo la CDF limeivua ngup CCM na Mwenyekiti wake kwa kuonesha namna gani wanavyojali maslahi yao zaidi ya maslahi ya Taifa.
Imefika mahala, inapotamkwa ama kuelezewa hoja ya USALAMA WA TAIFA inamaanisha usalama wa CCM hususan nafasi za juu za utawala.
Ushahidi wa haya ni namna ambavyo Katiba na hususan sheria ya uchaguzi inavyovunjwa wazi wazi kwa kufanya kampeni kwa mgombea wa CCM wakati kipenga cha uchaguzi hakijapulizwa bado.
Wakimbizi kuteuliwa na kuwekwa kwenye nafasi za maamuzi ya nchi ni jambo hatari sana kwa usalama na ustawi wa nchi yetu.
Tujitathmini, tuchukue hatua kusahihisha hili kosa kubwa.
Ninapata hisia kuwa yule aliyeamrisha jeshi kufanya usafi tarehe 24 anaweza akawa kaguswa na tamko hili.
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki JamiiForums