USA vs N.Korea Military Power

Nimecheck video hapa chini. Nimegundua USA anambwembwe nyingi sana. Kwa upande wa majini N. Korea iko njema sana. Vile vile kwa upande wa nchi kavu N. Korea wapo vizuri kinoma. Nina shawishika kusema kwamba N. Korea ni tishio kubwa sana kwa USA.

Ninathubutu kusema kwamba Trump anapiga mikwara tu. Na isitoshe kuna vifaavingine vingi vya N. Korea hawavijui. Kwa upande wa anga USA wapo vizuri sana lakini wanaweza kuingia N. Korea yenye uwezo mkubwa majini na nchi kavu?

Attack Submarine N. Korea 70 wakati USA 55


" Torpedo Boats and Missile Craft N. Korea zipo 250 wakati USA 0."mkuu unakosea haki mada...USA ndiye muundaji na mzalishaji wa Torpedo;inakuwaje anamiliki 0!
 
Ulishaiona size ya N Korea alafu ulinganishe na USA.... ndo utajua kwanini haitaji msaada wowote kuingia na kumtandika. Tatizo tuu ni wananchi wakawaida ndo watakao taabika ndo maana busara inatakiwa itumike sana. Manake akimtandika itabidi awape msaada maradufu tena watu wa N Korea baada ya kichapo kwa dogo.
Irefu wa pua sio wingi wa mafua. Msela akitaka kuingia vitani lazima atafute wa kumburuza, waburuzwaji ni UK na France. Na uku Asia ataburuzwa mjapan na SK, atawasaidia siku mbili tatu mwisho atakuwa anawauzia silaha tu na kuwapa mafunzo. Mbepari huyu hana masihara kwenye pesa
 
Vita ni hela
Vita ni gharama
Vita ni technics
Vita ni silaha
Kwa muktadha huu bila shaka ni aibu kwa US kupigana na N.K maana anaizidi kila kitu.

Vita ikianza itapiganwa katika ardhi ya N.K ,kwa hiyo shughuli zote za uzalishaji,viwanda na huduma za kijamii zitasimama na hii inamaanisha N.K hawataweza kupigana vita hii kwa muda mrefu bila kuanza kulia lia upungufu wa silaha,chakula,maradhi na madawa.

Kwa upande wa US yeye vita haitafika kwake kwa hiyo shughuli zote za kiuchumi zitaendelea kama kawaida na atapata faida kwa kuwauzia washirika wake silaha (Nato,S.K na Japan) bila kusahau kutest silaha zake mpya.

Mwisho wa siku Kim ataishiwa kunyongwa kama tulivyoona kwa Saddam na Gaddaf (R.i.p)
87d96464c95006898c912b854ba0bae8.jpg
nina mashaka na ufahamu wako wa geographical location ya US na NK.

Moja ya vitu vinavyoifanya marekani kusita kupigana na NK sio kwamba korea anauwezo bali ni jiografia itaruhusu raia wa US kuguswa na vita directly...tofauti na vita vingine ilivyowahi kushiriki.hupenda vita inayotumia ardhi ya nchi zingine mfano Afghan,Libya,misri n.k

Marekani na korea ni pua na mdomo. Marekani atashinda vita ila raia wake lazima wafe sana.. kutakuwa na direct impact kubwa sana US kiuchumi kijamii
 
Hatimae bw. Donald Trumpkakimbia rasi ya Korea. Ana Bahati Mkubwa mwenzie China kamuonya kua ukijaribu wanapiga. Usa. Itakua history. Ndio mwanzo wa kudharauliwa huo. Kubwa zima limeingia mitini.
 
Siyo mkono bro. Kwa upande wa majini N. Korea wapo njiema sana. Na upande wa ground wapo na multiple rocket launcher 2400 wakati USA wapo na 1200.
Korea atapigwa popote tu, iwe majini, angani au ardhini, hata nje ya dunia atapigwa tu. Miaka 72 yote hiyo tangu bomu la atomic huko Japan, wewe unadhani leo mwaka 2017 wana silaha za aina gani. Usijidanganye, USA kajiimarisha maeneo yote!!
 
Jamani nashangaa majadiliano. Mbona Korea Kaskazini wana idadi kubwa lakini kwa jumla mitambo yao ni makumbusho ya teknolojia, nusu (au zaidi) ya makombora machache waliyorusha yalilipuka na kuharibika mapema na karibu nusu ya wananchi wao hawana chakula cha kutosha. Hatari kutoka kwao ni kichaa cha uongozi na pia ya kwamba mpaka wao uko kilomita 40 tu kutoka Seoul/ Korea Kusini. Maana wanaweza kufikia mji wa watu mamilioni kwa mizinga - na hapa teknolojia ya karne iliyopita inatosha kwa bahati mbaya.
220px-Korean_Peninsula_at_night_from_space.jpg
Basi picha hii inasema mengi kuhusu hali ya kiteknolojia ya Korea Kaskazini (sehemu ya giza) kulingana na Korea Kusini (sehemu ya nuru chini) na China (juu kwenye picha) katika picha hii kutoka angani. (Inaonyesha rasi ya Korea wakati wa usiku)
 
Bila shaka na Wewe umemezwa na ngonjera za Mrus na NK unadefend kwA nguvu zote as if ulikuwepo mradi hoja yako ipate mashiko...

Yawezekana ukawa sahihi, ila pima ukisikiacho na kinachotokea, uhasama wa us na korea tokea 1950, uhasama wa us na iraq tokea 1988, korea anadunda huku akiwa jeuri, iraq kasambaratishwa vibaya, unafikiri nini sababu za hayo matukio. Afu hiyo kauli ya kwamba nadefend as if nilikuwepo, ni kauli za watu wenye mawazo madogo, usIandike tena unajidhalilisha, si kila ukweli unafahamika bayana kwa kuwepo kwako sehemu husika au katika hali fulani. Unaweza ukawa Tanzania ukaijua Dar peke yake, afu mtu akaisoma Tanzania katika kitabu, kilichopitishwa na mamlaka kadhaa tena well researched akajua mila, taratibu, mfumo wa maisha ya watz wa mikoa hata 15, ILA YUPO MBALI. VINGINE UNAJIULIZA NA KUPATA MAJIBU.
 
Siyo mkono bro. Kwa upande wa majini N. Korea wapo njiema sana. Na upande wa ground wapo na multiple rocket launcher 2400 wakati USA wapo na 1200.
Uchambuzi mwingine ni vituko,hizo rocket laucher ni pesa ngapi hata marekani ashindwe kuunda/kununua kama anazihitaji?
 
Advantage aliyonayo USA(kama vita otapiganwa) ni kwamba vita itapiganwa Korea na sio america so either way Korea watapata hasara sana
enter continental missiles. Korea hawana akili ndogo....pigana nyumban kwake yeye anatupoa kwako..tena nuclear
 
Hata enzi za iraq mlisema kuwa USA atajuta!! Kiulaini mtu akapigwa N. KOREA hana ubavu wa kupambana na Marekani bwana!


Usijetegemea yaliyotokea iraq yataweza kutokea tena. Dunia ya leo ni tofauti na miaka 10 iliyopita. Marekani bad anajitathimini na hii inaweza kuwa chambo kwake. Kaishia wapi na iran? Unadhan mrusi anampenda? Mjapani anampenda? Kwa nini mjerumani na mwingireza wamekaa kando. Tuweke ushabiki pembeni. Korea anajua fika marekani ana nyuklia je unafikiri ataenda kikuku. Inahitaji tafakari kubwa sana
 
Jeuri ya USA ni angani tu, ardhini hata sisi tunaweza kuwatoa upepo tu![/QUOTE
wewe jidanganye tu kununua kivuko shida meli za kawaida huna ya kijeshi hufikirii vifaru vyenyewe vya 80's wanajeshi wapo vizuri kiasi leo karne ya 21 ukapigane na usa wakati Tanzania haipo 20 bora kwa vifaa vya kijeshi Africa, ndio we are not in top 20 in Africa based on military weapon
 
Mwaga facts bana, hao South Korea washauliwaga hadi president wao na assasins wa DPRK na waliufyata.Japan ndio kashajichokeaga kitambo tu.
Nnachojua Japan ni super power too far from NK, na kawaida nchi yoyote yenye nguvu kubwa kiuchumi pia inauwezo mkubwa kijeshi....Ni ulimbukeni tu wa mapank....Kuhusu Seoul hakuna ushahidi kuwa NK ndo walifanya assassin ya president wao........
 
Hakuna wakumshinda USA hizi zote nimbwembwe na aliye kwambia Korea ana submarine nyingi kuliko marekan ni nani au data zako hizo
 
Mkuu China Isikutishe sana kijeshi hasa katika hayo makombora ya nyuklia, wakati Urusi (USSR wakati huo) inaeneza teknolojia ya nyuklia kwa mataifa machache ya Kikomunisti baada ya kuiwezesha Korea Kaskazini, sasa ikawa zamu ya Cuba ili kuinyamazisha US mwaka 1962 lile tikisiko la amani ya dunia lililoitwa Missile Crisis, baada ya Urusi kukubali kusitisha kupeleka yale makombora na mpango wa kujenga vinu vya kinyuklia Cuba, kuliibuka mgogoro mkubwa sana kati ya China na Urusi, hivyo China hakuwa mfaidika wa teknolojia hii, na hakukuwepo taifa lingine la kuipatia china teknolojia hii kwa sababu China ilikuwa nchi ya kijamaa na hivyo ni Urusi tu ndo wangeweza kuwapatia. China sasa hivi silaha yake KUBWA ni watu, yaani idadi, ndo imekuwa tishio kwa uchumi wa mataifa makubwa hasa unapoingia naye uhasama. kwa sababu ya soko CHINA IKIGEUKIA KUNUNUA BIDHAA TOKA TAIFA FULANI INAWEZA KULIFANYA KUWA TAJIRI NDO MAANA MAREKANI AKAONDOA UHASAMA NA KUANZA KUWEKEZA CHINA. Hivo China imekuwa ni taifa linalogombaniwa kuwa rafiki wa kila taifa kubwa kwa sababu za kiuchumi.

Kama unakumbuka vizuri mwaka 1999 wakati majeshi ya NATO yakiishambulia Yugoslavia kumtoa Slobodani Milosovic yalipiga ubalozi wa China yalivodai kwa bahati mbaya, lakini nafikiri pia ilikuwa kutingisha kiberiti, China iliwaka na kudai iombwe radhi, nakumbuka Marekani ilijibu kihuni kwamba tumetoa maelezo kwamba shambulizi lilikuwa la bahati mbaya na hamna haja ya kurudia kutoa maelezo, hii ni kwa sababu ile nguvu ya China kijeshi ambayo wengi tumeipachikia haina ni PSEUDOPOWER ipatayo kutoka kwa tusio makini na historia ya Dunia.

The same ikatokea 2005 marekani ilishambulia masafara wa barozi wa Italia na kumwua afisa upelelezi wa Italia, wakidai walidhani msafara wa kumtorosha Saadam Hussein, Italia ikakasirishwa na jambo hilo, ikataka maelezo ya msingi, pia askari waliohusika katika tukio hilo wapelekwe italia mashtaka. Marekani chini ya Bushi ilijibu kwa ustaarabu na umakin mkubwa na kuomba radhi juu ya hayo yaliyotokea kisha kuandika maelezo ya kutosha juu ya shambulizi lenyewe na kosa lilitokea.
Nakukumbusha kuwa kuna mataifa yenye nguvu yanayoogopwa si China kama tunavowapamba, China ina nguvu ila Magiants hawahofu mno kama tunavopenda kusema. Mataifa yasiyotabilika na yanaogopwa ni, Urusi, German, Italy, N. korean na Cuba. Sijataja US, UK na France maana husimama upande mmoja kuchokoza wengine. France anjificha kwa US na UK, mataiofa hayamuhofu sana siku zote. Kumbuka sakata la Edward Snowden, ndio maana yeye pia kakimbilia Urusi, nchi nyingine ingepigwa mkwara, ingevamiwa au CIA wangemfuata na kumwulia humohumo, lakini sasa Snowden amepewa kibali cha kuishi na ameajariwa.
Mkuu hebu Funguka kuhusu huyo Snowden, ameajiliwa kwa kibarua gani...?
 
Back
Top Bottom