Laptop01
JF-Expert Member
- Nov 29, 2009
- 1,365
- 796
Mpango huu ni miongoni mwa njama zinazoandaliwa kwa ajili ya Chama Tawala kuangamiza upinzani wa kisiasa nchini.
Mgombea binafsi wa kiti cha urais ama ubunge atakuwepo kwa mujibu wa Katiba Mpya ijayo. Zitto utashawishiwa kugombea nafasi mojawapo kati ya hizo mbili nje na Chama ulichopo sasa. Kisha utaahidiwa uwaziri wa fedha ama madini. Utategwa ujichagulie kati ya nafasi hizo. Lengo litakuwa ni kuhakikisha unajiengua CHADEMA ili kusababisha mgawanyiko katika idadi ya wapiga kura waliowaumini wa vyama vya upinzani, CHADEMA ikilengwa.
Nawe Zitto utashawishika kwenda huko, utagombea urais, utashindwa lkn utakuwa umefanikiwa kuleta mgawanyiko ktk suala zima la wapiga kura. Ila hutaachwa hivi hivi, utapewa ubunge wa kuteuliwa kama ilivyo kwa Mtu Makini Joseph Mbatia, kisha utaingizwa Serikalini kuchukua mojawapo ya hizo nafasi nilizokutajia hapo juu.
Sasa hilo litakuwa ndiyo ANGUKO lako la jumla katika siasa za Tanzania, nawe utafuata nyayo za Waridi Amani Kaborou.
Yawezekana hulijui hilo lkn laandaliwa na laja kwa ajili yako. Tafakari wewe ni kijana mwenye uwezo mkubwa wa kufikiti. FIKIRIA
Mimi tu kukuletea habari.
Mgombea binafsi wa kiti cha urais ama ubunge atakuwepo kwa mujibu wa Katiba Mpya ijayo. Zitto utashawishiwa kugombea nafasi mojawapo kati ya hizo mbili nje na Chama ulichopo sasa. Kisha utaahidiwa uwaziri wa fedha ama madini. Utategwa ujichagulie kati ya nafasi hizo. Lengo litakuwa ni kuhakikisha unajiengua CHADEMA ili kusababisha mgawanyiko katika idadi ya wapiga kura waliowaumini wa vyama vya upinzani, CHADEMA ikilengwa.
Nawe Zitto utashawishika kwenda huko, utagombea urais, utashindwa lkn utakuwa umefanikiwa kuleta mgawanyiko ktk suala zima la wapiga kura. Ila hutaachwa hivi hivi, utapewa ubunge wa kuteuliwa kama ilivyo kwa Mtu Makini Joseph Mbatia, kisha utaingizwa Serikalini kuchukua mojawapo ya hizo nafasi nilizokutajia hapo juu.
Sasa hilo litakuwa ndiyo ANGUKO lako la jumla katika siasa za Tanzania, nawe utafuata nyayo za Waridi Amani Kaborou.
Yawezekana hulijui hilo lkn laandaliwa na laja kwa ajili yako. Tafakari wewe ni kijana mwenye uwezo mkubwa wa kufikiti. FIKIRIA
Mimi tu kukuletea habari.