Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Rushwa ni kitu kibaya sana kinamtia mtu upofu kabisa Zitto haoni kabisa ni kipofu.
 
Mtei ameshindwa kumuita Zito na kumuambia haya?
 
Mimi naunga mkono ushauri wa Mzee Mtemi, kijana mwenzetu Zitto Kabwe awe na subira hadi muda utakapofika wa kinyang'anyiro cha kutafuta mgombea wa Urais ndio aaze hizo harakati, sasa hivi wajenge chama imara chenye wanachama wengi hasa kupia M4C, waendelee kupita kwenye mikoa yote na vitongoji vyote waelezee vuguvugu la mabadiliko ni strategic nzuri sana, muda bado kijana mwezetu, na ikumbukwe yeye ni kiongozi wa ngazi za juu kwenye chama, tumia busara, sikiliza wazee wanavyo kushauri
 
Hivi uenyekiti wa CDM Zitto alipotangaza nia akabaniwa kigezo kilikuwa umri? Wazee wa CDM hawana tofauti na wachawi..

Mkuu chama,
Makundi kutoka Kaskazini kamwe hawawezi kuacha kupambana na Zitto, wakikaa kimya ni sawa kumuachia Nguruwe akuchomee mishikaki.

Zitto Kabwe, ana nguvu kubwa kutoka kwenye makundi ya vijana pamoja na wazee, sehemu kubwa ya Tanzania mikoa kama Dar es Saalam, Pwani, Kigoma, Mwanza, Shinyanga, Mwanza, Morogoro, Tanga, Bukoba, Mtwara, Lindi, Singida, Tabora, hawa wajumbe wote wa Chadema wapo upande wa Zitto Kabwe.

Sehemu za Kaskazini ni kweli Zitto hana nguvu zozote za kisiasa.

Mtei ameshindwa kumuita Zito na kumuambia haya?

Amefufuka kumtoa Kyasaka kwenye NGO yangu.

Mkuu Molemo, alichofanya ZZK sio kutangaza kugombea urais kupitia Chadema, bali kutangaza nia ya kuiomba Chadema kumpitisha kama mgombea wa Chadema 2015!. Naomba sana utofautishe kati ya "kutangaza nia" na "kutangaza kugombea"!.



Ili chadema kuonysha ina "practice what it preach" lazima iache democracy i prevail!.
Go ZZK Go!.

Pasco.

Mkuu Molemo nipo tayari kuwaelemisha makamanda; sasa hebu tueleze tatizo lipo wapi kwa Zitto kusema atagombea uraisi? Sijawahi kumsikia Zitto akisema atalazimisha ili kutimiza azma yake ameweka bayana atafuata taratibu zote za chama kutimiza lengo lake; mkuu mimi nilitarajia Chadema iwe ni mfano wa demokrasia; je kinaogopewa kitu gani? Mpaka nyote mmetengeneza kimtandao kumpiga majungu Zitto? mkuu nijiandaa kulala nipe majibu yenye mwelekeo wa kidemokrasi; na huyu mzee Mtei yeye ni bado mwenyekiti wa Chadema?

Chama
Gongo la mboto DSM

Shame on mzee Mtei!

Chama
Gongo la mboto DSM

Molemo did you mean 001%?

Chama
Gongo la mboto DSM



CCM @ work Pole sana Pasco najua mpango wako hutofanikiwa kamwe
 
Last edited by a moderator:
Mwasisi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA Edwin Mtei amemuonya mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuacha kutangaza mambo ya Urais sasa kwani anasababisha mpasuko ndani ya CDM na badala yake ajikite kukijenga chama mpaka muda utakapofika ili chama kitoe utaratibu.

Mzee Mtei amesema amemshauri mara kadhaa Zitto umuhimu wa kutulia kama wenzake ndani ya chama na kukijenga chama lakini mbunge huyo amekuwa mkaidi na hasikii.

Pia Mzee Mtei amesema endapo mbunge huyo ataendeleza harakati zake za kutaka umri wa Urais ushuke hadi miaka chini ya 40 ili tu yeye apate nafasi ya kugombea basi atakuwa ni mbinafsi wa kupindukia na mwenye uroho mkubwa wa madaraka.

Akijibu madai hayo ya Mzee Mtei, Zitto Kabwe amemuonya Muasisi huyo wa chama na amewataka wazee ndani ya CHADEMA kuheshimu Demokrasia na kusema anaamini ni yeye atakayeweza kuishinda CCM mwaka 2015 na anataka Mzee Mtei akiwa bado hajafa amshuhudie jinsi atakavyobadili nchi akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Source: Mwananchi Jumamosi.

My Take:
Nadhani umefika wakati sasa wa Kamati Kuu kutoa mwongozo kuhusu suala hili. Hili suala la kila mtu kujitangaza kugombea Urais sasa linataka kupoteza mwelekeo wa harakati za CHADEMA kujijenga.

Imefika wakati wa M/kiti na Katibu mkuu wa chama kuongoza Kamati kuu kutoa hitimisho la jambo hili. Simaanishi kufukuza watu Hapana! Lakini itangaze muda muafaka wa wanachama kutangaza nia, kwani binafsi naamini DEMOKRASIA BILA NIDHAMU NI FUJO.

Huyo mbunge Bwana ZZ Kabwe si angoje kwanza katiba ipitishe huo umri wa kugombea Uraisi???? Mbona anapaparika, au ametumwa kuhujumu chama badala ya kujenga chama yeye anatafuta Uraisi???Kama alivyo mwambia Mzee Edwin Mtei akazane kujenga chama nia yetu Wanachama wa CHADEMA NI KUINGOA CCM MADARAKANI!!! Hizo mbinu za kina NCCR zilizo zoofisha chama Kule Tanga hatuzitaki, akae akijua kuwa pamoja na demokrasia anayosema kujenga chama ni muhimu kwa sasa aache tamaa!!!!

 
Hapo tu hamjachukua nchi,mmeshaanza kugombea madaraka.Zitto wewe siyo mchaga,hautaweza kuwa rais kamwe.Rudi kigoma ukavue migebuka,baba mkwe ndo keshakukataa hivyo.
 
Mwasisi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA Edwin Mtei amemuonya mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuacha kutangaza mambo ya Urais sasa kwani anasababisha mpasuko ndani ya CDM na badala yake ajikite kukijenga chama mpaka muda utakapofika ili chama kitoe utaratibu.

Mzee Mtei amesema amemshauri mara kadhaa Zitto umuhimu wa kutulia kama wenzake ndani ya chama na kukijenga chama lakini mbunge huyo amekuwa mkaidi na hasikii.

Pia Mzee Mtei amesema endapo mbunge huyo ataendeleza harakati zake za kutaka umri wa Urais ushuke hadi miaka chini ya 40 ili tu yeye apate nafasi ya kugombea basi atakuwa ni mbinafsi wa kupindukia na mwenye uroho mkubwa wa madaraka.

Akijibu madai hayo ya Mzee Mtei, Zitto Kabwe amemuonya Muasisi huyo wa chama na amewataka wazee ndani ya CHADEMA kuheshimu Demokrasia na kusema anaamini ni yeye atakayeweza kuishinda CCM mwaka 2015 na anataka Mzee Mtei akiwa bado hajafa amshuhudie jinsi atakavyobadili nchi akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Source: Mwananchi Jumamosi.

My Take:
Nadhani umefika wakati sasa wa Kamati Kuu kutoa mwongozo kuhusu suala hili. Hili suala la kila mtu kujitangaza kugombea Urais sasa linataka kupoteza mwelekeo wa harakati za CHADEMA kujijenga.

Imefika wakati wa M/kiti na Katibu mkuu wa chama kuongoza Kamati kuu kutoa hitimisho la jambo hili. Simaanishi kufukuza watu Hapana! Lakini itangaze muda muafaka wa wanachama kutangaza nia, kwani binafsi naamini DEMOKRASIA BILA NIDHAMU NI FUJO.

Jamani mbona mnasahau kuwa ni chama cha demokrasia?sasa iyo kubanana banana ndio nini tena. Mwacheni awe huru kuzungumza. Namie naamini zitto akigombea atashinda otherwise cdm bado hamtaki kuongoza nchi.
 
Hivi nyinyi wapenzi wa Chadema, bado hamjajua ZZK ndio mtaji wenu pekee wa ushindi 2015?(Sababu ni muislamu au?). Jee mnajua CCM itamsimamisha Membe?(Waislamu hawatampigia kura Membe sababu ni mkristo), sasa kwa vile huyo mgombea kipenzi wetu na Membe hawana tofauti katiuka zile kampeni za "kivile",(wote wakristo (Membe na Slaa) na hamjajua kwa mujibu wa katiba mpya, ili chama kishinde urais wa JMT, lazima kipate angalau theluthi moja ya kura za Visiwani!(99% Waislamu), hivi huyo mgombea wenu kipenzi (Dk Slaa-Mkristo), kwa siasa zetu "zile", hizo theluthi ya kura kutoka visiwani zinatokea wapi?!.

ZZK anakubalika sana kutokana na kuendesha "strategic politics" kwa urafiki wake na January Makamba(Muislamu), atazivuna kura zote za vijana wa CCM!, kwa urafiki wake na Jussa(Muislamu), atazivuna kura zote za CUF (Wanachama wake karibia woote waislamu) kule visiwani. Kwa usomi wake, atazivuna kura zote za vijana/wasomi na wataka badiliko ya kweli with clear goals na right strategies!.Nafikiri mtakuwa mmemuelewa kwanini anataka ZITO awe Rais,Viongozi wa CHADEMA haya ndio baadhi ya mawazo ya wanachama wenu kaeni chini muyapatie ufumbuzi!VIVA CDM!

acha ramli mwanangu hadi umefikia mahali kuwadhalilisha waislamu kwamba wapo remoted! kwa sasa waislamu wengi wanamjuwa adui yao na hawatatumika tena na wanasiasa uchwara na ghilba! si huyo hapo JK anaongoza kiislamu? mbona hajawapa kadhi kama walivyo taka? au! si kaapa kwa katiba? Hivi ccm na CDM wakiweka mgombea muislamu na DP wakaweka mgombea Mkristo hapo napo vipi! achana na siasa za ismailia jusi bro!
 
True colour zinaanza kuonekana taratibu
Huyu jamaa hafai hata kidogo

IMG_3027.JPG
 
kuna namna nyingi za kumbana mtu.
1.kumpuuza mpaka ajue sasa ninapuuzwa
2.kumfukuza
3.kumkanya
4. kumsihii aondoke mwenyewe

hoja 2: haifai kwani huyu tunajua kuna maslahi fulani nyuma yake, wantaka kuharalisha hoja fulani dhidi ya chadema kumfukuza itakuwa ni kosa la gharama. wapinzani wa CDM watapata cha kusema. Nidhamu yake ya ovyo itageuzwa kuwa ni vita ya cdm na waislam

hoja3: huyu sasa ni sikio la kufa hawezi kuelewa chochote kwani ana maslahi ya wazi na siri kwa hicho anachofanya

hoja4; haiwezekani kwa kuwa mission is still incomplete na kama akiondoka basi mradi umekufa bila mafanikio

hoja1: ndio inayofaa kwa sasa, zito amekuwa msumbufu wa chinichini , ukiona ameamua kuja hadharani ujue kule kusumbua kisirisiri kumekwama, hizi ni hatua zake za mwisho ZA KUSHINDWA KABISA,


NAWASHAURI CDM WASIAANGAIKE KUMJIBU
 
Mkuu Molemo nipo tayari kuwaelemisha makamanda; sasa hebu tueleze tatizo lipo wapi kwa Zitto kusema atagombea uraisi? Sijawahi kumsikia Zitto akisema atalazimisha ili kutimiza azma yake ameweka bayana atafuata taratibu zote za chama kutimiza lengo lake; mkuu mimi nilitarajia Chadema iwe ni mfano wa demokrasia; je kinaogopewa kitu gani? Mpaka nyote mmetengeneza kimtandao kumpiga majungu Zitto? mkuu nijiandaa kulala nipe majibu yenye mwelekeo wa kidemokrasi; na huyu mzee Mtei yeye ni bado mwenyekiti wa Chadema?

Chama
Gongo la mboto DSM
Kwanza alisema hatogombea tena ubunge ila urais hapo 2015 inamaana tayari keshajiteua ww unaona ni sawa?
 
Mtei ameshindwa kumuita Zito na kumuambia haya?
Hana hoja anasukumwa na ukanda na udini,tena simshauri Zitto kumsiliza huyu babu naona sasa hivi anatamani makao makuu ya chama yaamie kwake.

 
Kama lengo lenu (CHADEMA) ni kukomboa watanzania kutoka mikononi mwa wale wanaotafuna rasmali za nchi hii huku watanzania tukizidi kutopea kwenye lindi la umasiki, basi, sitarajii malumbano ya nani agombee urais 2015 kwa sasa nje ya utaratibu wenu kupitia kamati za chama chenu zinazoshughulikia suala hilo.

Kwa sasa Wanaokitakia mema CHADEMA basi acheni kulizungumzia suala hili la mgombea urais mpaka hapo muda muafaka utakapofika. Bado mnayo kazi ya kuwafikia watanzania wengi na kuwaeleza nia yenu ya kuwainua kutoka katika lindi la umasikini, hasa walioko Zanzibar. Natarajia M4C iwaunganishe wanaCHADEMA wote kulikomboa taifa hili kama sera za chama chenu zinavyoainisha.

Mwaweza kumuacha pembeni huyo au wale anaye/wanaoliamsha suala hili la kugombea urais kabla ya wakati wenu mliyojiwekea kulizunguzia kwa kutomjibu/wajibu kile ana/wanachokizungumza juu ya jambo hili.
 

Kweli wakuu kama ZITO yuko hivyo ni Agent wa TISS (kwa sababu hawezi kukwepa kuwa sio agent labda kama hajijui anatumiwa) huku ndani ya CDM anatafuta nini??? Labda kama ni kwa nia nzuri ya kuimalisha chama cha kuingoa CCM, LAKINI KAMA ANA MAHUSIANO NA MAFISADI HAPA SIO MAHALI PAKE!!!!Atupwe nje ya chama juhudi za kuleta maendeleo zisonge mbele, kwanza siku hizi hana faida yoyote kazi ni kutetea mafisadi tu!!!!

 
Mkuu chama,
Makundi kutoka Kaskazini kamwe hawawezi kuacha kupambana na Zitto, wakikaa kimya ni sawa kumuachia Nguruwe akuchomee mishikaki.

Zitto Kabwe, ana nguvu kubwa kutoka kwenye makundi ya vijana pamoja na wazee, sehemu kubwa ya Tanzania mikoa kama Dar es Saalam, Pwani, Kigoma, Mwanza, Shinyanga, Mwanza, Morogoro, Tanga, Bukoba, Mtwara, Lindi, Singida, Tabora, hawa wajumbe wote wa Chadema wapo upande wa Zitto Kabwe.

Sehemu za Kaskazini ni kweli Zitto hana nguvu zozote za kisiasa.

Mkuu unafurahia fedha zenu mlizompa zito zinavyofanya kazi ingawa mbinu zenu zimegundulika mchana kweupe mnalo mwaka huu mnaomba 2015 isifike.
 
Last edited by a moderator:
Labda mi sielewi; Tatizo ni Zitto kuwa na nia ya kugombea au tatizo ni yeye "kutangaza nia" mapema?
 
CCM @ work Pole sana Pasco najua mpango wako hutofanikiwa kamwe

ungejibu hoja zao mkuu, sio kuwaita ccm.
Huko ni kukimbia hoja.

Zkk alisema atakiomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea, na akasema kisipompitisha atampigia kampeni mgombea yeyote atakae pitishwa na chama.
Sasa tatizo liko wapi?

Na kama mtei anakipenda kweli chama na hataki malumbano, kwanini anaongea hayo kwenye media na asimuite zito au ashauri chama kiitishe kikao kujadili hilo swala?

Kama tatizo umri, sio zito pekee anaepinga huu umri, vijana wengi hatuutaki na tunataka katiba mpya iupunguze.
Ikumbukwe Wastan wa maisha ya mtanzania ni miaka 45.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom