Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

hivi maana ya demokrasia ni nini? kwa nini watu wanaweweseka sana kwa Zitto Kabwe jutangaza nia yake? mara kadhaa amesema 'IWAPO CHAMA KITAMPA RIDHAA" sasa tunashindwaje kusoma na kuelewa maana ya haya maneno? je, yeye ni dikteta ya kwamba atajichagua mwenyewe? chama si kina kamati kuu halmashauri kuu na mkutano mkuu? hivi si ndio vikao vitakavyompitisha mgombea wa CDM? Kuanza sasa kumwekea kauzibe ni kuifinya demokrasia, pili ni kuwapa nafasi wale wenye hoja dhaifu za ubaguzi, mwacheni azungumze wajumbe ndio watapembua nani anafaa na nani hafai

hoja ya kwamba hajishughulishi kujenga chama pia yaweza kuwa disqualification factor kwake wakati muafaka utakapowadia, maana kila mtu si atajinadi? yeye ni nani, kafanya nini kwa chama na kwa taifa? kama zitto hashiriki M4C then wapinzani watatumia kete hiyo kumgaragaza, let nature follow its course jamani, mbona Barack Obama alionyesha nia ya kugombea urais wa Marekani toka 2004? au huko hawakujua demokrasia ni nini?
 
Zito anajidanganya sana,aache kuropoka,anakuwa kama hajaenda shule!,subiri muda ufike utangaze nia yako,sasa hivi jenga chama kwanza.
Tujuze Mkuu huo muda wa kutangaza nia ya kuomba kuwa Raisi kupitia CHADEMA utafika lini? Maana kama Zito angekuwa anaufahamu asingekuwa anahangaika kutangaza sasa! Kimsingi huo muda uko tayari na ndiyo maana yeye kishatuonyesha NIA yake ya kuutaka URAISI wa JMT hivyo si kosa kwake. Anayotamka Mzee Mtei kumwambia Zitto kuwa ajenge Chama kwanza si sahihi mbona wakati ule Zitto anagombea Uenyekiti wa CHADEMA huyu Mzee alimjia juu Zitto kana kwamba ameguswa sehemu za SIRI kulikoni na CHADEMA?
 
asante kwa taarifa.......ole wao wanaodhani watanzania hawajui udhaifu wao..... Sasa hivi watz walio wengi wanajua kuchambua upi mbunga na yapi makapi.... Tumtakie kila la heri..
 
Mkuu naona umeamka naona sasa thread yangu itajaa maana ukiona thread yangu hata kama unaoga unaacha.Kweli CDM ni Lifestyle!

Mkuu Molemo nipo tayari kuwaelemisha makamanda; sasa hebu tueleze tatizo lipo wapi kwa Zitto kusema atagombea uraisi? Sijawahi kumsikia Zitto akisema atalazimisha ili kutimiza azma yake ameweka bayana atafuata taratibu zote za chama kutimiza lengo lake; mkuu mimi nilitarajia Chadema iwe ni mfano wa demokrasia; je kinaogopewa kitu gani? Mpaka nyote mmetengeneza kimtandao kumpiga majungu Zitto? mkuu nijiandaa kulala nipe majibu yenye mwelekeo wa kidemokrasi; na huyu mzee Mtei yeye ni bado mwenyekiti wa Chadema?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Namsihi Zitto mzee wa Panone atulie tu muda wake bado sana. Ana kazi kubwa ya kijpanga hata afikie hatua ya kujiita mgombea urais. Asifikiri popularity aliyo nayo itamsaidia chochote.
 
Zitto anajua anafanya makusudi kabisa akijua kwamba ana lengo lake maalumu. nilishasema siku nyingi kuwa huyu jamaa ni opputunist anayetegemea kubebwa na vyombo vya habari.
 
Zitto kamjibu vizuri hicho kizee,Mtei yuko bias katika mambo ya chama na ndio muasisi wa ukanda, ukabila,kuoleana,undugu na bado unaulea upuuzi huo kwa nguvu zote.Sijawahi na haitatokea kumsikia akiwa na misimamo tofauti kwa mkwewe Mbowe au Dr Slaa hata kama watafanya mambo ya kijinga.Ila utasikia akilalama kwa lolote la Zitto au wakuja wenzake hata kama ni zuri ama ni haki yao kama wanachama wa CDM kulifanya,ni heri atamke wazi kuwa CDM bado inamtazamo wa Ki-NGO na si chama cha siasa zenye mlengo wa kidemokrasia na uhuru wa mawazo ili watu wawaachie chama chao kuliko utapeli huu wa siasa wanaoufanya.
 
Mtazamo wangu juu ya Zitto ni kwamba ameshaona hana chake ndani ya CDM, so anajaribu kutafuta sympath kwa wananchi 'kwamba anafaa ila chama kimemnyima nafasi'.
Hivyo anautega uongozi wa CDM kwa wananchi, na kwa tactic hizo yuko tayari kuamua kwamba wakose wote.
 
Zitto anajua anafanya makusudi kabisa akijua kwamba ana lengo lake maalumu. nilishasema siku nyingi kuwa huyu jamaa ni opputunist anayetegemea kubebwa na vyombo vya habari.

Correct 100%
 
Mtazamo wangu juu ya Zitto ni kwamba ameshaona hana chake ndani ya CDM, so anajaribu kutafuta sympath kwa wananchi 'kwamba anafaa ila chama kimemnyima nafasi'.
Hivyo anautega uongozi wa CDM kwa wananchi, na kwa tactic hizo yuko tayari kuamua kwamba wakose wote.

Correct 100%
 
Zitto, unajua nani atatangulia kufa kati yako na mzee mtei? angalia kauli zako kijana.
 
Mzee mtei yule aliyehesabu wajumbe wa katiba kwa dini zao????!!! Hawezi kumuunga mkono zitto kamwe na kauli kama hii ni kuzidi kujiaibisha.
 
Mwasisi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA Edwin Mtei amemuonya mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuacha kutangaza mambo ya Urais sasa kwani anasababisha mpasuko ndani ya CDM na badala yake ajikite kukijenga chama mpaka muda utakapofika ili chama kitoe utaratibu.

Mzee Mtei amesema amemshauri mara kadhaa Zitto umuhimu wa kutulia kama wenzake ndani ya chama na kukijenga chama lakini mbunge huyo amekuwa mkaidi na hasikii.

Pia Mzee Mtei amesema endapo mbunge huyo ataendeleza harakati zake za kutaka umri wa Urais ushuke hadi miaka chini ya 40 ili tu yeye apate nafasi ya kugombea basi atakuwa ni mbinafsi wa kupindukia na mwenye uroho mkubwa wa madaraka.

Akijibu madai hayo ya Mzee Mtei, Zitto Kabwe amewataka wazee ndani ya CHADEMA kuheshimu Demokrasia na kusema anaamini ni yeye atakayeweza kuishinda CCM mwaka 2015 na anataka Mzee Mtei akiwa bado hajafa amshuhudie jinsi atakavyobadili nchi akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Source: Mwananchi Jumamosi.

My Take:
Nadhani umefika wakati sasa wa Kamati Kuu kutoa mwongozo kuhusu suala hili. Hili suala la kila mtu kujitangaza kugombea Urais sasa linataka kupoteza mwelekeo wa harakati za CHADEMA kujijenga.

Imefika wakati wa M/kiti na Katibu mkuu wa chama kuongoza Kamati kuu kutoa hitimisho la jambo hili. Simaanishi kufukuza watu Hapana! Lakini itangaze muda muafaka wa wanachama kutangaza nia, kwani binafsi naamini DEMOKRASIA BILA NIDHAMU NI FUJO.

Reading between the lines, Zitto hajakidhi cigezo vya kuiwakilisha CDM katika kinyang'anyiro cha Urais.
Mzee Mtei did not mince his words.
Kama Zitto kweli ni mtu wa CdM ushauri huu atauchukua , kama si wa CDM ataukidi, na wenziwe watammaliza.

Tusisahau kuwa Mzee Mtei ni Baba Mkwe wa Mbowe, Mwenyekiti wa CDM, na hayo aliyoya sema Mzee Mtei ndiyo ambayo angepaswa kusema Freeman Mbowe mwenyewe.

Watch out zitto before the vultures start circling!
 
20% ameimba...Acha tamaa mbaya, zitto ni kigeugeu! Traitor! Mnafiki! Mfitina! Janga la CDM na Taifa kwa ujumla! Anapenda sifa! Anajifanya anajua kila kitu! Anawadharau wenzake! Anatumika na magamba! Time will come watamtupa kama used toilet paper.
 
Back
Top Bottom