Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Mkuu wangu chama,
Ndani ya Chadema makundi yapo wala sio siri tena, Edwin Mtei, hawezi kumwambia hayo maneno mkwe wake Mbowe wala Dr Slaa, kamwambia Zitto sababu sio chaguo lake.

Mkuu,Kwani Mbowe na Dr Slaa wameropoka huu upuuzi lini? wale wana akili na hekima ya uongozi na utulivu.Hawana mihemko ya kiujana kama huyu Kabwe.Mtu mwenye tamaa sana ni wa kuogopwa.Watu wanatakiwa wakuone unafaa then waku endorse.Sio ngoma "unapiga wewe na unacheza wewe"-@Pasco wa JF
 
ni kwel kabisa mkuu sabasita nani asiyetaka utajiri wa ges na mafuta halafu ukute m2 mwenyewe katoka kwenye dhiki
 
Last edited by a moderator:
Molemo naamini wewe ni kijana mcha Mungu wa kikristo uwongo ni dhambi kubwa nieleze Zitto anaogopewa kitu gani? Nasubiri majibu nina shauku kujua kabla sijapanda kitandani! Leo ni sabato

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Zzk ajiulize 2010 hakuna mtu alijua kama slaa ndiye angagombea hadi dakika za mwisho sasa yeye anakurupuka nini? Au ametumwa
 
Mwanzoni nilidhani chadema itatuongoza na kutupeleka nchi ya ahadi ifikapo 2015 lakini kwa jinsi mambo yanavyoendelea ndani ya chama safari baaaaado sana na km hamtashtuka na kujipanga vzr CCM itatawala milele na mtabaki kulalamika wakati tatizo liko kwenu wenyewe. Why is it tht everyone is against zitto, whts the secret behind? So mmeshindwa km chama kukaa ndani ya vikao na kuwekana sawa mpaka mmehamia kwenye vyombo vya habari,,,zitto zitto zitto me nshawachoka, jipangeni
 
Mkuu Molemo, alichofanya ZZK sio kutangaza kugombea urais kupitia Chadema, bali kutangaza nia ya kuiomba Chadema kumpitisha kama mgombea wa Chadema 2015!. Naomba sana utofautishe kati ya "kutangaza nia" na "kutangaza kugombea"!.

ZZK alipotangaza nia, mimi nilimuunga mkono na kutangaza nia ni jambo jema na jambo la kheri na nikatoa wito kabisa kuwa kila mwenye nia na aitangaze!, hivi kuna ubaya gani?. Hebu kanisome hapa Urais 2015 tusimlaumu Zitto; Nani anaujua Msimamo wa Dr. Slaa ...

Lakini ZZK alipojitangaza rasmi kuwa hagombei tena ubunge na badala yake "atagombea urais kupitia Chadema" nilimpinga!. Nilimwambia wazi, that was wrong!, hakupaswa kujitangazwa, bali alipaswa tuu kuonyesha vitendo vya ki presidential candidate ndani ya chama, ili wenzake ndio wamuone na kumuomba agombee na sio kujipigia debe na hapa nilimtahadharisha Urais wa ZZK 2015: Ngoma Ikivuma Sana...!. Wenye uwezo wa kumtangaza mgombea ni Chama na sio mwan achama individual!.

Ila lazima mkubali, mkatae, ndani ya Chadema kuna double standards za hali ya juu!, kuna baadhi ya mambo yakifanywa na kina fulani ni halali, ila wakifanya kina fulani inageuka ningwa!.

Tatizo ni kuwa ndani ya mioyo ya wana Chadema wengi, wanaye mgombea wao mioyoni mwao, sio tuu kuwa mgombea huyo anakubalika sana kwao, bali anaabudiwa!. Kitendo cha ZZK kujitokeza anaonekana kama kumkufuru huyo mungu mtu anaye abudiwa!. Na kwa wasio jua, mimi naujua msimamo wa huyo mgombea wenu kipenzi kuhusu kugombea au kutogombea urais na usome hapa Msimamo wa Dr. Slaa Kwenye Urais 2015 ...

Unashauri kamati kuu itoe miongozo, hivi kumbe Chadema haina demokrasia ya kila mwanachama yoyote kugombea nafasi yoyote ni mpaka kamati kuu itoe miongozo!.

Tena kwa vile ZZK ni rafiki yangu, na kabla hata ya huo urais kuna uchaguzi wa viongozi wa Chadema, nitamshauri agombee tena Uenyekiti na this time hakuna kujitoa mpaka kieleweke!.

Hivi nyinyi wapenzi wa Chadema, bado hamjajua ZZK ndio mtaji wenu pekee wa ushindi 2015?. Jee mnajua CCM itamsimamisha Membe?, sasa kwa vile huyo mgombea kipenzi wetu na Membe hawana tofauti katiuka zile kampeni za "kivile", na hamjajua kwa mujibu wa katiba mpya, ili chama kishinde urais wa JMT, lazima kipate angalau theluthi moja ya kura za Visiwani!, hivi huyo mgombea wenu kipenzi, kwa siasa zetu "zile", hizo theluthi ya kura kutoka visiwani zinatokea wapi?!.

ZZK anakubalika sana kutokana na kuendesha "strategic politics" kwa urafiki wake na January Makamba, atazivuna kura zote za vijana wa CCM!, kwa urafiki wake na Jussa, atazivuna kura zote za CUF kule visiwani. Kwa usomi wake, atazivuna kura zote za vijana/wasomi na wataka badiliko ya kweli with clear goals na right strategies!.

Nashauri, baada ya Mzee Mtei kukikabidhi chama kwenye "safe hands" za mkwewe, his advisory role yake ibaki limited kwa insiders tuu wa chama na sio ku express his public opinion publically as if chama bado ni chake!. Heshima yake kama muasisi ipo pale pale, lakini kwa sasa chama sio chake tena, sasa chama ni cha wanachama!, tena Mwenyekiti Mbowe anatakiwa kujipambanua kabisa kwa hili kuwa "amekata kabisa zile mothers apron strings" ili isje onekana kina Mzee Edwin Mtei ndio bado wanaendesha chama by proxy kupitia kwa wakwe zao!.

Ili chadema kuonysha ina "practice what it preach" lazima iache democracy i prevail!.
Go ZZK Go!.

Pasco.
Hivi nyinyi wapenzi wa Chadema, bado hamjajua ZZK ndio mtaji wenu pekee wa ushindi 2015?(Sababu ni muislamu au?). Jee mnajua CCM itamsimamisha Membe?(Waislamu hawatampigia kura Membe sababu ni mkristo), sasa kwa vile huyo mgombea kipenzi wetu na Membe hawana tofauti katiuka zile kampeni za "kivile",(wote wakristo (Membe na Slaa) na hamjajua kwa mujibu wa katiba mpya, ili chama kishinde urais wa JMT, lazima kipate angalau theluthi moja ya kura za Visiwani!(99% Waislamu), hivi huyo mgombea wenu kipenzi (Dk Slaa-Mkristo), kwa siasa zetu "zile", hizo theluthi ya kura kutoka visiwani zinatokea wapi?!.

ZZK anakubalika sana kutokana na kuendesha "strategic politics" kwa urafiki wake na January Makamba(Muislamu), atazivuna kura zote za vijana wa CCM!, kwa urafiki wake na Jussa(Muislamu), atazivuna kura zote za CUF (Wanachama wake karibia woote waislamu) kule visiwani. Kwa usomi wake, atazivuna kura zote za vijana/wasomi na wataka badiliko ya kweli with clear goals na right strategies!.Nafikiri mtakuwa mmemuelewa kwanini anataka ZITO awe Rais,Viongozi wa CHADEMA haya ndio baadhi ya mawazo ya wanachama wenu kaeni chini muyapatie ufumbuzi!VIVA CDM!
 
Mkuu wangu chama,
Ndani ya Chadema makundi yapo wala sio siri tena, Edwin Mtei, hawezi kumwambia hayo maneno mkwe wake Mbowe wala Dr Slaa, kamwambia Zitto sababu sio chaguo lake.

Mkuu Ritz
Aweda ameshaamka kauona moto anaogopa kutia mguu; Molemo ukimuuliza swali anakimbia kaanzisha uzi hoja zimemshinda; hawa jamaa wa Chadema wanafurahisha sana yaani deal zimekaa kiukweukwe na kiukandaukanda; sasa ndio itawaingia akilini kwa Zitto walimlazimisha asigombee uenyekiti.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Majungu na maneno ya kijinga ndio nyie great thinker mnaweza kujadili degree zenu za udocta engineers na wengine hazisaidii kujenga nchi.
nani asiyejuwa kupata uongozi hata kijijini panampangilio wake wewe ukisema tu mimi nataka uenyekiti wa kijiji si lazima uchaguliwe?
bara bara hayo madaraja na migodini wataaalamu ni wachina na wazungu ...viwanda mmewapa wahindi....vipesa kidogo mnavyokusanya kodi mnavitumia kupiga umbeya ............naniiiii zenu
 
Urais cdm ni tatizo kubwa, rais kupitia cdm laizma atoke kaskazini zitto aanzishe chama chake
 
Kwa nafasi na heshima yake ndani ya CHADEMA, kauli ya Mtei ni nzito na inapaswa kuchukuliwa kama kauli ya chama.Yaweza kuchukukuliwa kama kauli ya chama kwa kuwa hatukuwahi kuwa na matatizo na kauli za Nyerere,mwasisi wa CCM, alizoendelea kuzitoa hata baada ya kung'atuka katika chama na serikalini.Aliendelea kuaminiwa na sehemu kubwa ya wanannchi kwa kuwa waliamini matamko na maonyo yake yalikuwa yakisukumwa na nia njema,hekima na busaraa , huku akitishwa na kuogopeshwa na udhaifu wa upinzani kwa wakati huo.Hakika,nasi, sasa tunapaswa kuogopeshwa na kutishwa na udhaifu wa CCM. Mwenye busara na hekima ataelewa na atabadilika.
Nina hakika kabisa, ndani ya moyo wangu, kuwa kauli ya Mwasisi wa chama inawakilisha msimamo wa Katibu Dkt Slaa..Na ninaamini vile vile, kuwa huo ni msimamo pia wa Mwenyekiti Mbowe,tukirejea kauli yake aliyoitoa wakati wa uzinduzi wa M4C Dar Es Salaam ,kwamba ''siongozi chama cha wasaka urais... sasa tunajenga chama" .
Tunapoona wakuu wengine wa Chama wapo kimya, tutakosea sana iwapo tutafikiri wanaunga mkono harakati za ''watangaza nia''mapema.Hapana.
Mhusika ,sasa,anapaswa aheshimu kauli na ushauri wa Mzee wetu .Asipotendea kazi ushauri wake nina hofu hakuna mwingine atakayesikilizwa na huyu ''presidential aspirant''.Vinginevyo, tutahitaji tunahitaji kauli ya Kamati Kuu.

Yupo mwanajamvi, anadai, eti,Barack Obama, alitangaza nia ya kuutaka urais tangu mwaka 2004!
Jibu langu kwake ni rahisi: ndani ya Tanzania,tunajenga chama, katika mazingira na nyakati tofauti kabisa na zile za Marekani .Ukweli ni kuwa mwaka 2004 tayari Chama cha Democrats kilikuwa kimewahi kushinda urais na kuongoza nchi ya Marekani ,mara nyingi kabisa na kabla ya mwaka 2004 ,nchi ya Marakani ilikuwa tayari na kiwango cha juu cha demokrsia kutokana na kuwa wananchi wengi wenye kiwango cha juu cha uelewa wa masuala ya uraia(strong civic competence).Kwetu hapa ,baadhi ya variables hizo bado zipo katika hatua zake za awali kabisa na zingine hazijawahi kabisa hata kutokea.Tutambue kuwa tunaijenga CHADEMA katika mazingira ya Tanzania huku tukiendelea kuamini katika dhana ya na misingi ya demokrasia.Zaidi tuongozwe na busara ,hekima na uwajibikaji katika kauli matendo na maamuzi yetu.
Kwa sasa tuna kazi ya kuwaonyesha wapiga kura watarajiwa wa mwaka 2015 kuwa CHADEMA ni chama makini tulivu na kisicho na viongozi wenye uroho wa madaraka.Tunajenga trust.
Kwa sasa mambo ya urais wa mwaka 2015, ashirio la upungufu ama ukosefu wa hekima na busara na uwajibikaji.
Mwenye masiko na asikie.
 
Mwasisi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA Edwin Mtei amemuonya mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuacha kutangaza mambo ya Urais sasa kwani anasababisha mpasuko ndani ya CDM na badala yake ajikite kukijenga chama mpaka muda utakapofika ili chama kitoe utaratibu.

Mzee Mtei amesema amemshauri mara kadhaa Zitto umuhimu wa kutulia kama wenzake ndani ya chama na kukijenga chama lakini mbunge huyo amekuwa mkaidi na hasikii.

Pia Mzee Mtei amesema endapo mbunge huyo ataendeleza harakati zake za kutaka umri wa Urais ushuke hadi miaka chini ya 40 ili tu yeye apate nafasi ya kugombea basi atakuwa ni mbinafsi wa kupindukia na mwenye uroho mkubwa wa madaraka.

Akijibu madai hayo ya Mzee Mtei, Zitto Kabwe amemuonya Muasisi huyo wa chama na amewataka wazee ndani ya CHADEMA kuheshimu Demokrasia na kusema anaamini ni yeye atakayeweza kuishinda CCM mwaka 2015 na anataka Mzee Mtei akiwa bado hajafa amshuhudie jinsi atakavyobadili nchi akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Source: Mwananchi Jumamosi.

My Take:
Nadhani umefika wakati sasa wa Kamati Kuu kutoa mwongozo kuhusu suala hili. Hili suala la kila mtu kujitangaza kugombea Urais sasa linataka kupoteza mwelekeo wa harakati za CHADEMA kujijenga.

Imefika wakati wa M/kiti na Katibu mkuu wa chama kuongoza Kamati kuu kutoa hitimisho la jambo hili. Simaanishi kufukuza watu Hapana! Lakini itangaze muda muafaka wa wanachama kutangaza nia, kwani binafsi naamini DEMOKRASIA BILA NIDHAMU NI FUJO.

wee zzk, kweli una hamu hadi ya kufikia kubaka hadi demokrasia, kukidhi hamu yako! kwani alicho ongea babu Mtei sio Demokrasia? una uchu mwanangu hadi umefikia upofu na uziwi dogo!
 
Hivi nyinyi wapenzi wa Chadema, bado hamjajua ZZK ndio mtaji wenu pekee wa ushindi 2015?(Sababu ni muislamu au?). Jee mnajua CCM itamsimamisha Membe?(Waislamu hawatampigia kura Membe sababu ni mkristo), sasa kwa vile huyo mgombea kipenzi wetu na Membe hawana tofauti katiuka zile kampeni za "kivile",(wote wakristo (Membe na Slaa) na hamjajua kwa mujibu wa katiba mpya, ili chama kishinde urais wa JMT, lazima kipate angalau theluthi moja ya kura za Visiwani!(99% Waislamu), hivi huyo mgombea wenu kipenzi (Dk Slaa-Mkristo), kwa siasa zetu "zile", hizo theluthi ya kura kutoka visiwani zinatokea wapi?!.

ZZK anakubalika sana kutokana na kuendesha "strategic politics" kwa urafiki wake na January Makamba(Muislamu), atazivuna kura zote za vijana wa CCM!, kwa urafiki wake na Jussa(Muislamu), atazivuna kura zote za CUF (Wanachama wake karibia woote waislamu) kule visiwani. Kwa usomi wake, atazivuna kura zote za vijana/wasomi na wataka badiliko ya kweli with clear goals na right strategies!.Nafikiri mtakuwa mmemuelewa kwanini anataka ZITO awe Rais,Viongozi wa CHADEMA haya ndio baadhi ya mawazo ya wanachama wenu kaeni chini muyapatie ufumbuzi!VIVA CDM!
duh...kwa hiyo dini ndio factor kubwa ya kupigiwa kura!!!!tumekwisha tz
 
Pengine safari hii atasikiliza huu ushauri. Ameamua kwa makusudi kuwa CONFUSER.
Dawa ya watu wa namna ni kuwatimua mapema, ni bomu zito litakalolipuka mbele ya safari.
Hana nia njema, alikuwa mpambabaji, now he has changed, likely cz has interests to protect.

Zito hajawahi kuwa mpambanaji Bali alikuwa anajijengea mazingira aka alikuwa msituni kufanya maziezi ya ku rape democracy na sasa ndio anaingia battle field mmeshuhudia nguvu aliyokuja nayo na kundi lake akiwahiwa hatoleta madhara 2015 ila akicheleweshwa ccm itadumu milele
 
kabourou,mrema,cheyo,wassira,dovutwa,lamwai,mbatia,bagenda...zitto,...namba ya vibaraka wa ccm inazidi kuongezeka
 
Kwa hiyo ndani ya Chadema ni marufuku kutangaza kugombea urais.

Hivi wewe Ritz, nyumbani kwako kukiwa na msiba alafu mmoja wa wanafamilia anaongelea kuleta mdundiko na kufanya sherehe utamwelewa?? Ishu ni kufanya right things at a right time. Sasa hivi kama chama au familia tunaelekeza nguvu kwenye kujenga chama na sio maswala ya urais...kuna faida gani tukipata huo urais na huku tuna wabunge 10???? Ni wazi ccm itaendelea kutawala. Tunampenda Zitto na tunathamini mchango wake ila kwa sasa tunajenga chama. Wakati ukifika atagombea na vikao halali vitampitisha
 
Hivi uenyekiti wa CDM Zitto alipotangaza nia akabaniwa kigezo kilikuwa umri? Wazee wa CDM hawana tofauti na wachawi..
 
Akijibu madai hayo ya Mzee Mtei, Zitto Kabwe amemuonya Muasisi huyo wa chama na amewataka wazee ndani ya CHADEMA kuheshimu Demokrasia na kusema anaamini ni yeye atakayeweza kuishinda CCM mwaka 2015 na anataka Mzee Mtei akiwa bado hajafa amshuhudie jinsi atakavyobadili nchi akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Na akitangulia kufa yeye ZITTO atataka mzee Mzee Mtei ashuhudie nini?
 
Back
Top Bottom