Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,180
- 7,355
Kama kweli nia yetu ya dhati ni kumpata kiongozi mzuri ni lazima tuangalie ni yapi viongozi waliopita bila kujali vyama yaliwafanya washindwe na kuangamiza Taifa na yapi yaliwafanya waweze kuongoza na kuliendeleza taifa kama limeendelea.
Uzoefu unaonyesha tatizo kubwa la viongozi wetu wengi ni kukataa sio tu kufuata ushauri bali hata kusikiliza. Sasa kila mmoja ampe kijana mwenzetu ZZK anayetaka kwa udi na uvumba kwenda ikulu je ana fit wapi.
Anashaurika
anasikiliza ushauri wa kitaalamu
ana busara na hekima
anaweza kutumia elimu yake kutatua matatizo yetu au kujikweza na kudharau kila mmoja
anaweza kufanya kazi na wengine hata pale wanapotaofautiana kwa personal issues?
anaweza kuvumilia wenzake
anaweza kutoa maamuzi magumu
je ni kigeugeu kwa asilimia ngapi unaweza kuamini anachosema ndicho ? kumbuka amesha sema zaidi ya mara moja kuwa hata gombea ubunge nk
Je ni mwadilifu wa kweli au ngonjera tu
Je ni mfitini na mchonganishi
Je anaweza kweli kutoka rohoni kushinda vishawishi hasa vya rushwa nk nk
mkubwa Mkandara
Je ZZK ataingia ikulu akijua fika team ya kumwingiza ikulu anaichafua na kuitibua kila kukicha
Je wote tunaamini ushindi wa kisiasa ni team work ?
Je ZZK hata kama ni mzuri vipi ni kweli anaweza kushinda mwenyewe??
Je ni nani yuko tayari kufanya kazi na kiburi cha ZZK
Kutumiwa au kutotumiwa hilo analijua mwenyewe kwa nini ZZK hataki kwenda vijijini kujenga Chama ila anasubiria tu safari ya Ikulu
Kama ni swala la kutumikia chama anajifananisha na nani???
Je ZZK anaona kutoka moyoni nafasi ya mwanachama wa kawaida au anawaona kama vyombo tu vya kumpeleka ikulu
Kwa kauli zake mwenyewe anajenga chama au anakivuruga??
Kama ni elimu ni wangapi wamesoma ndani ya CDM?
Je ZZK anakumbuka kuwa amelelewa na kukuzwa kama wengine.
Tujijenge kama viongozi na kuomba hekima kama suleiman ya kuongoza watanzania.
Jambo moja ambalo linanifanya nisihofie wala kuona kama kauli za kukurupuka za ZZK zina madhara yeyote ni kwa sababu nimezizoea. Siku zote amekuwa akiongea vitu vinavyosababisha utata, lakini CDM imekuwa na buffering capacity kubwa juu ya hayo. Kwa hiyo hata sasa simwoni wala sioni tishio lolote la kauli zake.
La pili ni kwamba, nina uhakika 100% kuwa ZZK hatakuwa raisi wa kwanza wa nchi kupitia CDM, iwe 2015 au zaidi ya hapo.
Pamoja na hayo yote, bado namuona ZZK kama mtendaji mahiri na kiongozi shupavu wa baadae wa chama au hata nchi. Siku CDM ikiingia ikulu, naamini ZZK atakuwa na nafasi ya kiutendaji na kimaamuzi, hapo ndipo atakapotuthibishia kuwa yeye ni mchapakazi, mbunifu na mwadilifu (kama nimuonavyo mimi)