Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Mbowe kakanusha kuwa hakutamka Slaa agombee Urais 2015.Sasa mtei anaunga mkono hoja ya nani mnalisha watu maneno.
 
Ni maoni yake pia sio sheria...na mimi namuunga mkono Dk Slaa 2015
 
MWASISI wa Chadema,Edwin Mtei amemtaka Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe kumwachia Katibu Mkuu wake, Dk Willbrod Slaa fursa ya kuwania tena urais mwaka 2015 kwa madai kuwa ndiye chaguo la watu kwa sasa.

Kauli hiyo ya Mtei inakuja siku kadhaa baada ya kuunga mkono kauli ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwamba Dk Slaa awanie tena urais katika uchaguzi ujao huku yeye akijiondoa katika orodha ya viongozi watakaowania nafasi hiyo kupitia Chadema.

Akihojiwa na gazeti hili, Mtei alisema Zitto anapaswa kumwachia Dk Slaa apeperushe bendera ya chama hicho katika uchaguzi ujao kwa kuwa ndiye chaguo la wengi.

“Zitto atagombea baada ya Dk Slaa na kwa sasa amwachie katibu mkuu atupeperushie bendera ya chama katika uchaguzi ujao kwani ndiye chaguo la wengi,” alisema Mtei.
Mtei alisema yeye anasimamia msimamo wa Mbowe na kamati kuu ya chama hicho kuhusu kumpendekeza Dk Slaa kuwania nafasi hiyo.

Alisema kila mmoja ndani ya chama amekuwa na hisia na mawazo tofauti lakini msimamo wake kwa sasa ni kumtaka Dk Slaa awanie nafasi hiyo ya urais na si Zitto. “Kila mmoja na hisia na maoni yake, Dk Slaa ana yake, Freeman na yake hata mimi nina hisia zangu na Slaa ndiye pendekezo langu nataka atupeperushie bendera,” alisema Mtei. ( MWANANCHI JAN 3,2013)

Mtei anachakaa vibaya mpaka anasahau kwamba ni yeye ndie aliekianzisha hiki chama mwanzoni kama NGO ya kuwaendeleza wachagga na baadae kukigeuza na kukipa jina la chama cha DEMOKRASIA na maendeleo pia,leo hazungumzi tena lugha ya demokrasia,anaongoza vitendo vya ubakaji wa demokrasia hiyo changa chamani ama hakika hiki ni kioja cha kufungulia mwaka 2013,mtakaoishi mwishoni mwa mwaka mkikumbushe kioja hiki cha kwanza kupata kutokea mwaka huu!
 
Je mtei akishasema kuna mwimgine anaweza gombea tena!!!!hata kama ni maoni yake.
 
mwananchi sasa limekua kama tambala la deki

kivipi ??kisa limetoa habari isiyopendwa na wana chadema???.... Na vipi gazeti la tz daima ndo zuri bz linatoa habari mbaya na kejeli kwa ccm na serikali??? Na kusifia chadema??..... Kama ni uongo mbona mzee mtei mwenyewe hakanushi mnabaki ninyi tu vibaraka kutoa povu humu..
 
"Kila mmoja na hisia na maoni yake, Dk Slaa ana yake, Freeman na yake hata mimi nina hisia zangu na Slaa ndiye pendekezo langu nataka atupeperushie bendera," alisema Mtei. ( MWANANCHI JAN 3,2013)

Very good indeed


Mtei alisema yeye anasimamia msimamo wa Mbowe na kamati kuu ya chama hicho kuhusu kumpendekeza Dk Slaa kuwania nafasi hiyo.
 
Mpasuko Chadema, BABA Mkwe (Mwasisi wa Chama) Vs Mkwe (Mwenyekiti wa Chama) wanazidi kukorogana, yetu macho
 
“Kila mmoja na hisia na maoni yake, Dk Slaa ana yake, Freeman na yake hata mimi nina hisia zangu na Slaa ndiye pendekezo langu nataka atupeperushie bendera,” alisema Mtei. ( MWANANCHI JAN 3,2013)

Very good indeed

Hope tutaendelea kusikia na maoni ya wengine wengi zaidi.
 
mwananchi sasa limekua kama tambala la deki[/QU ila tanzania daima limekuwa kapeti cyo la kufunikia uchafu wenu enh, leo mnaliona siyo, busara ilikuwa mumshauri mzee wenu aache mazoea na aruhusu demokrasia cdm sio kulilalamikia gazet wakati ni kaz ya gazet kutafta habari na mtei ni source nzuri hasa kwa habari za unafiki wenu.
 
Wafuasi wa CHADEMA JF naona leo wako likizo. Au wamegoma kucoment kwenye thread tata? Kila siku tunawaambia hiki chama kina wenyewe, mnabisha oneni sasa. Mtu na mkwe wake wapepishana kwenda kwenye media kauli zimegongana. Nyie bendera fuata upepo (wafuasi bila kufikiria) mnasemaje? Peoplezzzzzzzzzzzzzzzzzz!
 
Na ukweli uko wazi mkatae mkubari dr.slaa hana mvuto kama aliokuwa nao 2010 kwa hiyo ccm wanaelekea kushinda kirahisi sana sana 2015 ... Mvuto wa zitto au lema au mnyika ni mkubwa kwa wananchi kuliko dr.slaa... Mzee mtei ,mbowe wamechemka wanauza chama mchana kweupe.....
 
Kwani kuna ulazima gani kwa zito kugombea urais kwa sasa?
MWASISI wa CHADEMA,Edwin Mtei amemtaka Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe kumwachia Katibu Mkuu wake, Dk Willbrod Slaa fursa ya kuwania tena urais mwaka 2015 kwa madai kuwa ndiye chaguo la watu kwa sasa.

Kauli hiyo ya Mtei inakuja siku kadhaa baada ya kuunga mkono kauli ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kwamba Dk Slaa awanie tena urais katika uchaguzi ujao huku yeye akijiondoa katika orodha ya viongozi watakaowania nafasi hiyo kupitia CHADEMA.

Akihojiwa na gazeti hili, Mtei alisema Zitto anapaswa kumwachia Dk Slaa apeperushe bendera ya chama hicho katika uchaguzi ujao kwa kuwa ndiye chaguo la wengi.

“Zitto atagombea baada ya Dk Slaa na kwa sasa amwachie katibu mkuu atupeperushie bendera ya chama katika uchaguzi ujao kwani ndiye chaguo la wengi,” alisema Mtei.

Mtei alisema yeye anasimamia msimamo wa Mbowe na kamati kuu ya chama hicho kuhusu kumpendekeza Dk Slaa kuwania nafasi hiyo.

Alisema kila mmoja ndani ya chama amekuwa na hisia na mawazo tofauti lakini msimamo wake kwa sasa ni kumtaka Dk Slaa awanie nafasi hiyo ya urais na si Zitto. “Kila mmoja na hisia na maoni yake, Dk Slaa ana yake, Freeman na yake hata mimi nina hisia zangu na Slaa ndiye pendekezo langu nataka atupeperushie bendera,” alisema Mtei. ( MWANANCHI JAN 3,2013)
 
Back
Top Bottom