Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Hayo ni mawazo yako japo huajafanya tathmini yeyote ya kisayansi ukaujua ukweli.CCM kwenye upinzani wanahaha Dr.Slaa peke yake na si mwingine.Mfano rahisi tu ni kwamba itokee tu Slaa leo aseme anaacha siasa,ccm watafanya sherehe kubwa.Slaa ndio kikwazo cha kweli kwa chama tawala.
Na ukweli uko wazi mkatae mkubari dr.slaa hana mvuto kama aliokuwa nao 2010 kwa hiyo ccm wanaelekea kushinda kirahisi sana sana 2015 ... Mvuto wa zitto au lema au mnyika ni mkubwa kwa wananchi kuliko dr.slaa... Mzee mtei ,mbowe wamechemka wanauza chama mchana kweupe.....
 
Akili yako iko sawa na afya ya tumbo lako.Pole kwa mawazo feki.Hakika wewe ni gamba.
Wafuasi wa CHADEMA JF naona leo wako likizo. Au wamegoma kucoment kwenye thread tata? Kila siku tunawaambia hiki chama kina wenyewe, mnabisha oneni sasa. Mtu na mkwe wake wapepishana kwenda kwenye media kauli zimegongana. Nyie bendera fuata upepo (wafuasi bila kufikiria) mnasemaje? Peoplezzzzzzzzzzzzzzzzzz!
 
Ni maoni yake jamni hata mimi naunga mkono oni lake kuwa kwa sasa Zito akae pembeni ampishe Dr. Slaa atupeperushie bendera 2015. hata hivyo ni chaguo la wengi
 
wafuasi wa chadema jf naona leo wako likizo. Au wamegoma kucoment kwenye thread tata? Kila siku tunawaambia hiki chama kina wenyewe, mnabisha oneni sasa. Mtu na mkwe wake wapepishana kwenda kwenye media kauli zimegongana. Nyie bendera fuata upepo (wafuasi bila kufikiria) mnasemaje? Peoplezzzzzzzzzzzzzzzzzz!

wakija hapa ni matusi tu...watakuambi we ni masalia ..... Chadema kinaelekea kufa tena kifo kibaya chama hata hakijapewa madaraka wanaanza kugombaniani madaraka je wakipewa nchi itakuwaje???.... Nani leo aje ajitokeze et ndani ya chadema kuna demokrasia hakuna ....zitto alitangaza nia mzee mtei,mbowe povu liliwatoka....
 
mwasisi wa chadema,edwin mtei amemtaka naibu katibu mkuu wa chama hicho, zitto kabwe kumwachia katibu mkuu wake, dk willbrod slaa fursa ya kuwania tena urais mwaka 2015 kwa madai kuwa ndiye chaguo la watu kwa sasa.

Kauli hiyo ya mtei inakuja siku kadhaa baada ya kuunga mkono kauli ya mwenyekiti wa chadema, freeman mbowe kwamba dk slaa awanie tena urais katika uchaguzi ujao huku yeye akijiondoa katika orodha ya viongozi watakaowania nafasi hiyo kupitia chadema.

Akihojiwa na gazeti hili, mtei alisema zitto anapaswa kumwachia dk slaa apeperushe bendera ya chama hicho katika uchaguzi ujao kwa kuwa ndiye chaguo la wengi.

“zitto atagombea baada ya dk slaa na kwa sasa amwachie katibu mkuu atupeperushie bendera ya chama katika uchaguzi ujao kwani ndiye chaguo la wengi,” alisema mtei.

Mtei alisema yeye anasimamia msimamo wa mbowe na kamati kuu ya chama hicho kuhusu kumpendekeza dk slaa kuwania nafasi hiyo.

Alisema kila mmoja ndani ya chama amekuwa na hisia na mawazo tofauti lakini msimamo wake kwa sasa ni kumtaka dk slaa awanie nafasi hiyo ya urais na si zitto. “kila mmoja na hisia na maoni yake, dk slaa ana yake, freeman na yake hata mimi nina hisia zangu na slaa ndiye pendekezo langu nataka atupeperushie bendera,” alisema mtei. ( mwananchi jan 3,2013)

slaa tosha urais 2015
mbowe tosha uenyekiti chadema 2013
 
Mtei anachakaa vibaya mpaka anasahau kwamba ni yeye ndie aliekianzisha hiki chama mwanzoni kama NGO ya kuwaendeleza wachagga na baadae kukigeuza na kukipa jina la chama cha DEMOKRASIA na maendeleo pia,leo hazungumzi tena lugha ya demokrasia,anaongoza vitendo vya ubakaji wa demokrasia hiyo changa chamani ama hakika hiki ni kioja cha kufungulia mwaka 2013,mtakaoishi mwishoni mwa mwaka mkikumbushe kioja hiki cha kwanza kupata kutokea mwaka huu!
Ungeandika tofauti na Ulichokiandika, ningeshangaa. Ningejua kweli mwaka 2013 Umekuja na Miujiza ya Kuwafungua mpaka wale waliofungwa vifungo vya akili.
 
Hahaa dah nmecheka sana..mpaka 2015 tutashuhudia mengi hii ndo kwanzaa 2013.. Issue ya kutoa maoni jamani ni haki ya mtu. Ila tuacheni story za vijiweni kuhusu democrasia na haki..there is no such a thing..hata mbinguni hatutakuwa sawa, maandiko yanasema patakua na viti vya wazee 12 ambao treatment yao itakua ya tofauti, usifikiri utakua sawa na Ibrahim hata kama ukifika mbinguni! So ambacho hakitokei kw Mungu usikitegemee duniani.. Mzee Mtei hata kama katoa maoni, yale yanabadilika kua maelekezo, kila taasisi duniani ina wenyewe na tuna haki tofauti katika hizo taasisi hata kama malengo ni sawa, hata obama pale democrat wapo wanaofikiri kilichompitisha ni utashi wake peke yake ama kupendwa outside the party not tht way at all, wapo watu smart behind ambao obama angefail wao ndo wangepata pigo kubwa. Nachoona hapa huyu mzee mtei ananikumbusha sinema flan za kimafioso, jambazi unakuta kazeeka afu yupo kwene wheelchair haongei sana anatoa maelekezo madogo tu lakini effect yake inashuka mpak chini.
 
Hawa wakwe wanajua kuwa Zitto akichukua watakufa njaa, ulaji uko kwa babu. Na vile babu anauchu wa madaraka atakubali masharti yote ya marienge.
 
“Zitto atagombea baada ya Dk Slaa na kwa sasa amwachie katibu mkuu atupeperushie bendera ya chama katika uchaguzi ujao kwani ndiye chaguo la wengi,,” alisema Mtei. ( MWANANCHI JAN 3,2013)

....ok, kwahiyo Chadema itamtangaza rasmi Dr Slaa kuwa mgombea urais 2015, na wakati huohuo kumteua Zitto kuwa mgombea urais wa 2020 provided Dr Slaa atashindwa 2015, mmmh. Hili Ni Bonge la Domo-Krasia.....
 
slaa tosha urais 2015
mbowe tosha uenyekiti chadema 2013

...Kijana mbona hauna heshima kwa Mwasisi wako wa Chama?ebu malizia pia kuwa "Zitto Zuberi Kabwe Tosha Urais 2020"....
 
Kijana Zitto anapaswa kutoa Kauli ya kuahirisha kugombea 2015, na aunge mkono chaguo la CHAMA chake na wananchi ambao wanamsubiri kwa hamu Dr. Slaa. uamzi huu utamjenga kisiasa na kurudisha imani ya wananchi kwake ambayo inaonekana kupungua!
 
....ok, kwahiyo chadema itamtangaza rasmi dr slaa kuwa mgombea urais 2015, na wakati huohuo kumteua zitto kuwa mgombea urais wa 2020 provided dr slaa atashindwa 2015, mmmh....

chukua hatua ..........
 
...Mbons hauna heshima kwa Mwasisi wako wa Chama?ebu malizia pia kuwa "Zitto Zuberi Kabwe Tosha Urais 2020"....

Tayari mwasisi ameshamuunga mkono Zitto for 2020, hata mimi kwakweli 2020 Mungu akiniweka hai, na Zitto akaendelea kuwa kuwa CHADEMA kunitoa kwenye kambi yake mtatumia katapila!
 
Last edited by a moderator:
Zitto asilaumiwe, zilaumiwe pesa za ccm wazomhonga kuhakikisha chadema haifiki mbali. Mtei anavyomshauri mla rushwa km zitto ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa.

Mnajifari ee kwa kupeana likes, sasa Zitto ameingiaje wakati yeye hajasema neno tangu wenye chama waanze kupanga safu za uongozi wa chama chao?
 
Back
Top Bottom