Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Naweza kusema nyie ni mitambo inayozalishwa pale LUMUMBA, tunawajua sana nyie ni wazandiki wanafiki
na wanyanganyi na kamwe hamtofanikiwa, najua kuwa mnapokea madau tofauti tofauti kama Pasco anawezidi dau

Hii kamwe haitawasadia na watanzania kamwe hatutayumba siku itafika tutachukua nchi yetu

Copy to Pasco, Ritz, zomba, Nnauye Jr, chama, Ecoli, OTIS, Kata nyodo, malaria SUgu (RIP), Jenifa, peri,

usikimbie hoja mkuu,
hizo unazoleta ni porojo.
Jibuni hoja, wapi katiba ya cdm imekataza mtu kutangaza nia?
Huyo mzee mtei anazeeka vibaya, aliposema hawezi kuona cdm inaongozwa na mtu asiemfaham alimaanisha nini?
Alipohoji kwa nini tume ya katiba ina waislam wengi alikuwa anatoa ujumbe gani kwa taifa?
Kama kweli hataki mpasuko ndani ya chama, kwanini analumbana na zkk kwenye media na sio kumuita kwenye vikao vya chama?
Nani basi anahaki ya kugombea urais kupitia cdm?
Zkk hakusema lazima agombee, alisema ataomba ridhaa ya chama na kisipompitisha atampigia kampeni yeyote atakae pitishwa, sasa tatizo liko wapi?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, tupo vitani (M4C) Practially, na makamanda tutawapata huko!
sio uko nyuma na wagonjwa unaleta sound! hii ni advance to conntact! hata kupika sembe la muhogo kuna taratibu zake ili uive vizuri!
No pamoja na hayo ndugu zetu wa kwa mama mdogo ndio ambao hawaaminiki na wanabadilika any time T,so kiukweli wao hawaangaliii nani anafaaa kuongoza nchi hiii,wao wanaangalia nani ni wa dini gani,hata kama ni jiwe wako radhi walipigie kura!
 
Mkuu nakuomba ujaribu kusoma vizuri hoja yangu, usijaribu ku-derail mada. Dk Slaa naye yuko kwenye kundi ambalo koo hiyo linamuona ni expendable, wanamtumia tu kutafuta umaharufu lakini deep down hawana habari naye. Labda nikwambie kitu - kama shemeji yangu huyo angeshinda URAIS mwaka 2005 saa hizi angekuwa amekwisha fanyiwa mbinu za kumuondoa IKULU kwa kisingizio chochote kile kiwe kusingizia ugonjwa au njia mbadala ili wamsimike mtu kutoka ukoo wao, don't underrate resolve na hulka za jamaa hawa, wana mbinu nyingi SANA.

ahahahahaaa! daah mbona unachekesha?
Kwa hapa tulipo fikishwa na magamba hadi anakunywa uji wa mgonjwa! hata mbwa ruksa atawale kuliko hawa magamba! hivyo unapochangia ukae ukilijua hilo!
 
Jamani tulifurahia sana Chadema walivyoamua kunyamaza, walionekana wako Tofauti na zito. sasa wameanzia wapi kumsemesha? Kwani wao Hawajui Zitto anataka nini? Wanahitaji kumuarifu wanachomfanya?
 
usikimbie hoja mkuu,
hizo unazoleta ni porojo.
Jibuni hoja, wapi katiba ya cdm imekataza mtu kutangaza nia?
Huyo mzee mtei anazeeka vibaya, aliposema hawezi kuona cdm inaongozwa na mtu asiemfaham alimaanisha nini?
Alipohoji kwa nini tume ya katiba ina waislam wengi alikuwa anatoa ujumbe gani kwa taifa?
Kama kweli hataki mpasuko ndani ya chama, kwanini analumbana na zkk kwenye media na sio kumuita kwenye vikao vya chama?
Nani basi anahaki ya kugombea urais kupitia cdm?
Zkk hakusema lazima agombee, alisema ataomba ridhaa ya chama na kisipompitisha atampigia kampeni yeyote atakae pitishwa, sasa tatizo liko wapi?


Umejitahidi kutumia logic katika hoja hii. Lakini kuna pungufu moja muhimu katika hoja yako. Umeshindwa kujadili upande wa pili wa tatizo. Walio katika upande wa kumkataza Zitto kuendeleza tangazo lake hawajamkataza Zitto kugombea urais. Wanacholalamikia ni timing ambayo inapingana na mkakati wa kundi. Why now? Kuhusu Mtei kuhoji mambo, ni kipengele gani cha katiba ya Tanzania, au hata katiba ya Chadema, ambacho kinamkataza Mtanzania huru kuhoji kitu katika uendeshaji wa nchi kama raia binafsi?
 
ahahahahaaa! daah mbona unachekesha?
Kwa hapa tulipo fikishwa na magamba hadi anakunywa uji wa mgonjwa! hata mbwa ruksa atawale kuliko hawa magamba! hivyo unapochangia ukae ukilijua hilo!
Unajua magamba wana akili sana za kuwaharibu watu akili zao,jamani CDM inaweza kuja kuwa mkombozi wetu hapa Tanzania tuachane na magamba!
 
Sipendi ukabila lkn vijana wa kigoma ndio hulka yao wanajisikia na kujiona wao ndio bora hasahasa walioenda shule
chunguza kuanzia kafulila na zitto.. Na uzoefu kwa watu hawa wakigoma nmeupata huku kigoma nlpokuwa kikazi
 
Zitto namkubali, ila suala la kujibizana na wazee waasisi wa chama simuungi mkono. Zitto 2015.

zitto simkubali,ila mzee Mtei kufanya chama kama chake huwa sipendi sana..haswa anapoonesha hadharani anapambana na Zitto kwa gharama yoyote ile.
 
huu ushauri ni mzuri yeye zito asubiri muda utafika tu kama imeandikwa kuwa rais atakuwa tu wala hatapiga kelele
 
usikimbie hoja mkuu,
hizo unazoleta ni porojo.
Jibuni hoja, wapi katiba ya cdm imekataza mtu kutangaza nia?
Huyo mzee mtei anazeeka vibaya, aliposema hawezi kuona cdm inaongozwa na mtu asiemfaham alimaanisha nini?
Alipohoji kwa nini tume ya katiba ina waislam wengi alikuwa anatoa ujumbe gani kwa taifa?
Kama kweli hataki mpasuko ndani ya chama, kwanini analumbana na zkk kwenye media na sio kumuita kwenye vikao vya chama?
Nani basi anahaki ya kugombea urais kupitia cdm?
Zkk hakusema lazima agombee, alisema ataomba ridhaa ya chama na kisipompitisha atampigia kampeni yeyote atakae pitishwa, sasa tatizo liko wapi?

Mkuu wangu peri,
Maneno mazito haya maneno ya ujenzi kwa mustakabali wa taifa letu...Copy to Molemo, King of Kings, Mkuu chama,
 
Last edited by a moderator:
usikimbie hoja mkuu,
hizo unazoleta ni porojo.
Jibuni hoja, wapi katiba ya cdm imekataza mtu kutangaza nia?
Huyo mzee mtei anazeeka vibaya, aliposema hawezi kuona cdm inaongozwa na mtu asiemfaham alimaanisha nini?
Alipohoji kwa nini tume ya katiba ina waislam wengi alikuwa anatoa ujumbe gani kwa taifa?
Kama kweli hataki mpasuko ndani ya chama, kwanini analumbana na zkk kwenye media na sio kumuita kwenye vikao vya chama?
Nani basi anahaki ya kugombea urais kupitia cdm?
Zkk hakusema lazima agombee, alisema ataomba ridhaa ya chama na kisipompitisha atampigia kampeni yeyote atakae pitishwa, sasa tatizo liko wapi?
Tunataka kumuona ZITO katika harakati za kujenga chama kwa sasa,2010 CDM walishindwa kwa sababu kutokuwa network ya kutosha hasa vijijini,kama kweli ZITO ana nia na Urais ajiunge na Wenzake kwenye M4C,Yeye kwenye kujenga chama haonekani,anachofikria ni kugombea urais,Nitamuunga mkono Zitto kama atashiriki katika M4C katika maeneo mbalimbali ya nchi tofauti na hapo hatutamuunga mkono!
 
..Ingawa siungi mkono kinachofanywa (namna anavyofanya) na Zitto , sikubaliani pia na uamuzi wa Mzee Mtei. Mtei ni mjumbe wa vikao vya juu vya chama na huko ana nafasi ya kuyasema haya na hata kuongea na Zitto ana kwa ana. Hapa anakaribisha malumbano ya kwenye vyombo vya habari ambayo siyo ya lazima. Anawapa pia nafasi wapinzani wa CDM kujua kwamba kuna msuguano ndani ya CDM ambayo siyo nzuri kwa afya ya chama.
 
Zitto kawashika pabaya na ndio kwanza anataka kuning'inia kuongeza maumivu. 2015 mapilot wenu Dr Slaa na Mbowe watatafuta kwa kuland na ndege yenu ya Air wakabila,wadini na wakanda.
 
No pamoja na hayo ndugu zetu wa kwa mama mdogo ndio ambao hawaaminiki na wanabadilika any time T,so kiukweli wao hawaangaliii nani anafaaa kuongoza nchi hiii,wao wanaangalia nani ni wa dini gani,hata kama ni jiwe wako radhi walipigie kura!

Mkuu, aminia hao ni redio imani na wasanii wachache wa dar tu! wengi wamesha shitukia, manake wamesha ona wanaotesa/kuteseka ni waislamu wakristo na wapagani! na ufisadi hauchagui dini taifa wala rangi na lugha! Tembelea wafanyikazi na wakulima, pia mikoani uone elimu ya uraia ilivyo jikita!
 
Heshima mbele Wakuu.

Hili tatizo linaweza kuwa na mitizamo miwili: Linaweza likawa na mtizamo wa hisaikolojia, ambao si mzuri sana kwa Mhe. Zitto Kabwe, na Upande wa Kisiasa, ambao pia si mzuri kwa upande wake. Tatizo kubwa zaidi ni kwamba upande wa pili, ambao ni wa kisiasa, una athari kwa Chama pia kwa sababu hatima yake inaelekeza Zitto Kabwe afukuzwe kutoka katika chama haraka ili chama kianze mending damage miaka mitatu kabla ya uchaguzi.

Upande wa Saikolojia ni huu: Mtu mwenye inferiority complex iliyojificha katika nafsi yake--pengine kwa kujihisi anapungukiwa kitu fulani, ambacho kinaweza kuwa kujihisi ana sura mbaya, au impotent, au mapungufu mengine ambayo mtu anakuwa akijihisi kwa siri ya moyo wake, basi watu kama hawa hutafuta kufunika inferiority complex hiyo kwa kujikweza, kujitapa ama kutaka dunia ijue wao ni masihi fulani hivi. Hadi hapa tulipofikia, mimi binafsi naona dalili za Zitto Kabwe katika jitihada za kufunika inferiority complex zaidi kulipo kitu kingine.

Lakini katika matamko ya Kijana huyu, mimi binafsi naona dalili za tabia ya mtoto ambaye kakua bila father figure, na hivyo hana hofu ya mamlaka. Mtu kama huyu anaweza kuwa bomu sana katika jumuia ambayo inahitaji utii kwa mamlaka na mshikamano. Wataalam wa Management wanakiri papal system ni mfumo mzuri sana wa mafanikio ya uongozi wa kundi lolote. Matamko yanaonesha kuwa Zitto Kabwe anakosa utii na heshima kwa watu wenye mamlaka katika jamii. Huu ni mtizamo wa kisaikolojia, na unaelekeza afukuzwe kutoka kwenye chama haraka iwezekanavyo.

Mtizamo wa kisiasa unaashiria kuwa katumwa kuleta Chaos katika chama. Nao pia unaelekeza afukuzwe katika chama haraka. Kwa hivyo Zitto Kabwe afukuzwe kutoka Chadema na chama kiendelee na mikakati yake pakiwapo utii na mshikamano miongoni mwa viongozi na wanachama. Hili litatimua vumbi, lakini upo muda wa kutosha kutuliza vumbi hilo. Zitto aondolewe Chadema.
Mkuu nakuunga mkono 100% ukiangalia maelezo ya Mkuu Bahatisha kwenye hii quote
Mambo ya ZITO KABWE NI HAYA1
1:Zitto ahusishwa na Rostam | Gazeti la MwanaHalisi
2:Usalama wa Taifa wavamia CHADEMA | Gazeti la MwanaHalisi
Jitahidini kumjua zito,muone mambo yake!
Huyu bwana haaminiki hata kidogo unless CDM imeamua kuunga mkono maovu ya CCM, yaani wizi ufisadi, rushwa, dhuluma za mali za watanzania, na mengine mengi ukiongeza siku hizi hata mauwaji!!!! Huyu bwana anakuja na style ya waliosambaratisha chama cha NCCR mageuzi na sasa wamekaa wenyewe TISS ndio vinara!!! Tunahitajika kuwa na mtazamo wa mbali ili tuweze kukomboa nchi hii iliyofanywa kuwa wanyonge Tanzania!!!


 
usikimbie hoja mkuu,
hizo unazoleta ni porojo.
Jibuni hoja, wapi katiba ya cdm imekataza mtu kutangaza nia?
Huyo mzee mtei anazeeka vibaya, aliposema hawezi kuona cdm inaongozwa na mtu asiemfaham alimaanisha nini?
Alipohoji kwa nini tume ya katiba ina waislam wengi alikuwa anatoa ujumbe gani kwa taifa?
Kama kweli hataki mpasuko ndani ya chama, kwanini analumbana na zkk kwenye media na sio kumuita kwenye vikao vya chama?
Nani basi anahaki ya kugombea urais kupitia cdm?
Zkk hakusema lazima agombee, alisema ataomba ridhaa ya chama na kisipompitisha atampigia kampeni yeyote atakae pitishwa, sasa tatizo liko wapi?
Tatizo siyo muda muafaka
 
Zitto asilaumiwe, zilaumiwe pesa za ccm wazomhonga kuhakikisha chadema haifiki mbali. Mtei anavyomshauri mla rushwa km zitto ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa.
Mkeo akitembea nje ya ndoa utamlaumu nani? Mke au jamaa aliyetembea naye? Kwangu mimi Mke ndio wa kulaumiwa, kwanini asipambane na vishawishi? So kwanu mimi Zitto mwenye ndio wa kulaumiwa. CCM wanatishwa na Dr Slaa kwanini wasimpe hizo pesa na badala yake wapeleke kwa Zitto? He must have shown his weakness na ndio maana wakamdaka
 
Tatizo si Zito kutangangaza nia ya kugombea u- Rais. Tatizo ni dhamila ya dhati ya Mh. Zito. Je ni kweli anautaka u-Rais ama anatumika kubomoa chama.

Kuna Msemo mmoja wa Mwl. JK alitamka wakati wa harakati za uhuru kuwa " Wakati tunagombea uhuru watu wengi walituunga mkona lakini kunabadhi nyalikuwa na malengo ya kupora duka la Kharasingah na wengine Land Rover ya DC''. Mwl alimaanisha kumbe kwenye harakati za ukombozi wapo wengi ndani ya kundi wenye malengo tofauti na kinachowaunganisha.

Mh. kumbuka "Whey they use you live big today: tomorrow you bury in-a casket "
 
Back
Top Bottom