Upinzani bila kubadili siasa mtapata hasara kubwa Kwa Samia..

Hakuna kitu kinaamua siasa kama 'wakati'..
Wanasiasa wazuri ni wale wanaojua nyakati zinavyobadilika na kwenda na wakati uliopo ...

Watanzania walikuwa wamechoshwa mno na siasa za Magufuli...na uongozi wake kiujumla..
Kubanwa Uhuru wa kuongea
Kufokewa na kukaripiwa
Kutoa matamko Kwa ukali..
Kuzungumza Peke yake..
Kutokukosolewa ..
Kukosekana Kwa mijadala na majadiliano..
Na mengi yaliyoenda na hayo..

Ujio wa Samia umebadili siasa Kwa ujumla..
Samia hafoki anaongea Kwa upole na kushawishi ..
Anazungumzia mazungumzo na mijadala..
Hazuii kukosolewa badala yake anakaribisha kukosolewa Kwa serikali yake..

Kikubwa zaidi ni Mwanamke ..
Watu wanamtazama Kwa 'kumhurumia'..
Na kumpa 'all benefits of the doubts'..
Na kuelewa kuwa anapambana na mfumo dume...
Watu wengi wanaju hii nchi ngumu na wanajua Samia atahangaika kuweza kumudu ...still wanafarijika na 'kurudi Kwa Uhuru wa kuongea na kukosoa'..

Sasa kama wapinzani wanafikiri siasa za kumshambulia Rais na serikali yake zinalipa bado kama enzi za JK watakuwa wanakosea sana....
Sana Sana wataonekana 'hawana adabu'
Na wanajaribu 'kumuonea' 'Rais Mwanamke' baada ya 'kidume ' JPM
'kuwakomesha hadi wakaufyata'..

Siasa za kipindi hiki zinahitaji ubingwa wa hoja kwenye mijadala ya kistaarabu..bila
Kuwa 'boa' wananchi ambao walishachoshwa na Magufuli Sana Sana wanataka 'mzunguko' wa hela urudi kama ule wa JK....

Kuleta siasa za ulalamishi..
Siasa za uwana harakati.
Na siasa za Ku target watu na kuwashambulia bila kujua ..'role halisi' ya hao watu ni siasa ambazo zinakuwa 'outdated ' so fast...

Watu wanampenda Samia sio Kwa sababu ni kiongozi bora.. wanampenda Kwa sababu wanaona 'nafuu inakuja'
Upinzani ukicheza siasa za kuleta 'distraction'wakati watu wanasubiri nafuu ije ..hasira za wananchi zinaweza washukia wao.....

Siasa inaendana na nyakati.. wapinzani wanasoma nyakati??

wapinzani waliingiza emotion issue ya JPM, na wakasahau siasa ni wakati

JPM kaondoka nao😂🙋
 
Ndio maana mleta Mada kaweka mada hapa mjielewe na kubadilika siasa za kizamani za kupinga kila kitu kwa jazba mpaka mnamuita Kiongozi dhaifu safari hii hakuzitoa
Huko Ujerumani, Amerika ya kina Baiden upinzani hawaropoki mfululizo wakati sio wake, subirini wakatiwa wa Chaguzi za serikali za mitaa 2024 na 2025
Leo tu mmeambiwa mtasikilizwa mnataka kwanza Covid 19 watolewe Bungeni
Mbeligiji arudishiwe V8 yake mafao yake na mishahara ya ubunge mwishowe na Ubunge au urais wake
Upinzani sio kila kitu kupinga hata mtu akienda chooni mnatafuta sababu
Mbona zitto hayupo hivyo au Lipumbasoma tena

kaisha lemaa!!! huyo usikute huwa anajipinga pia
 
kwa sasa hawana chaguo.

kuchukia harakati za magufuli ni kupishana na watanzania wengi,kumfagilia mama samia ni kuungana na ccm.

lakini wa sababu walinyimwa busara,hawakuweza kujua hatari ya matokeo ya majibu watakayopewa baada ya kumwomba mungu wao.
leo hii magufuli amekufa,na chadema inaelekea kuzimu.
Unajidangaya sana.
 
kwa sasa hawana chaguo.

kuchukia harakati za magufuli ni kupishana na watanzania wengi,kumfagilia mama samia ni kuungana na ccm.

lakini wa sababu walinyimwa busara,hawakuweza kujua hatari ya matokeo ya majibu watakayopewa baada ya kumwomba mungu wao.
leo hii magufuli amekufa,na chadema inaelekea kuzimu.

Yaani kifo cha JPM kimezika kabisa upinzani

Kisiasa walitakiwa wanyakue agenda zake na kumlazimisha mama aendelee nazo....walikurupuka vibaya

wangekosoa uhuru wao tu wa siasa na wananchi angehamia upande wa upinzani....na kuiacha CCM inajizoa zoa
 
Wengi sasa hivi (ukiwemo wewe na wana CCM wengi tu) wanakiri kuwa Magufuli aliharibu. Nakunukuu:
''Watanzania walikuwa wamechoshwa mno na siasa za Magufuli...na uongozi wake kiujumla..
Kubanwa Uhuru wa kuongea
Kufokewa na kukaripiwa
Kutoa matamko Kwa ukali..
Kuzungumza Peke yake..
Kutokukosolewa ..
Kukosekana Kwa mijadala na majadiliano..
Na mengi yaliyoenda na hayo..''

Mwisho wa nukuu.
Kama wakati wa Magufuli watanzania walikuwa kwenye hali mbaya namna hii (jambo ambalo ni kweli) mbona hawakufanya mabadiliko? Je, hata wakijenga hoja kipindi hiki ni nini kitawafanya watanzania wawasikilize na kuiondoa CCM?
My take: Upinzani hata uwe makini na wenye hoja namna gani, bila wananchi kujielewa na kuacha woga ni kazi bure. Kinachoendelea kuiweka CCM madarakani siyo udhaifu wa viongozi wa upinzani wala uimara wa hoja wa CCM bali wananchi wengi kutojielewa na kuwa woga.
Hapo sasa ndiyo unakosea. Kwa sababu mtu au watu au Watanzania wengi hawakubaliani na wewe hawajielewi au ni waoga. Ni matusi kama haya kwa wananchi ambayo wanawafanya wananchi wasiuchague upinzani. Huwezi kunitukana kuwa mimi sijielewi au mimi muoga, alafu utegemee niwe upande wake. Kutafuta kura lazima unyeyekee, uwe mpole, ubembeleze. Lakini nyie wenzetu mnasjiona ndiyo mnajuwa kila kitu, kumbe kujuwa kwenu hakuwezi kuwafanya mkavuka. Ni wananchi tu watakaowafanye mvuke.

Ebu jiangalieni kwanza. Angalia lugha mnayotumia kwa wapiga kura watarajiwa. Mkishaona makosa yenu, rudini kwa wananchi, mtumie lugha ya kistaha, ili wananchi wawaone kama mna ukomavu wa kuendesha nchi. Mtu yeyote anayetanguliza matusi mbele, mtu yeyote anayeifuata maiti kaburini na kuitukana, huyo mtu kwanza hana hoja na pili bado hajakomaa kupewa uongozi.
 
Kwani aliekwambia tulimchoka magufuli nani?. Ulimchoka wewe tu.
Hapo ndio unashangaa.

Mtu anajiropokea eti watanzania walikua wamemchoka JPM, mara watanzania wanampenda mama Samia. Sasa huo utafiti wa Watanzania kumchoka JPM aliufanya lini na wa Watanzania kumpenda mama Samia ameufanya lini?

Mtu anajiandikia hoja za jumla jumla(generalisation) unajua kabisa huyu akili hana.
 
Kinachoiweka CCM ni woga wa wananchi kupigania haki zao za kuchagua viongozi wanaowataka. Haya mengine mnayoandika huku ni bla bla tu.
Ishu nyingine Mkuu upinzani wetu Upo weak sana! Huu upinzani Wa Akina Mdee, Silinde, Katambi, Slaa, Sugu, Lema hauwezi kutufikisha popote, Opportunists Ndio wamejaa huko upinzani, wanachowaza wapate ubunge wajikusanyie mali! The Only thing inaweza kutusaidia ni CCM kumeguka vipande vipande ( Nusura litokee Hilo 2015, na tunakumbuka shida waliyopata kwenye uchaguzi)
 
Hapo sasa ndiyo unakosea. Kwa sababu mtu au watu au Watanzania wengi hawakubaliani na wewe hawajielewi au ni waoga. Ni matusi kama haya kwa wananchi ambayo wanawafanya wananchi wasiuchague upinzani. Huwezi kunitukana kuwa mimi sijielewi au mimi muoga, alafu utegemee niwe upande wake. Kutafuta kura lazima unyeyekee, uwe mpole, ubembeleze. Lakini nyie wenzetu mnasjiona ndiyo mnajuwa kila kitu, kumbe kujuwa kwenu hakuwezi kuwafanya mkavuka. Ni wananchi tu watakaowafanye mvuke.

Ebu jiangalieni kwanza. Angalia lugha mnayotumia kwa wapiga kura watarajiwa. Mkishaona makosa yenu, rudini kwa wananchi, mtumie lugha ya kistaha, ili wananchi wawaone kama mna ukomavu wa kuendesha nchi. Mtu yeyote anayetanguliza matusi mbele, mtu yeyote anayeifuata maiti kaburini na kuitukana, huyo mtu kwanza hana hoja na pili bado hajakomaa kupewa uongozi.

unadhani kuna wapinzani hapo mkuu!!!

hilo ni genge la wahuni wenye roho za chuki na hasira.
tizama mpuuzi mmoja anadai ahakikishiwe usalama ndipo arejee,wakati alikiwepo hapa hap miezi kadhaa iliyopita,hakuguswa wala kutomaswa.
 
Ishu nyingine Mkuu upinzani wetu Upo weak sana! Huu upinzani Wa Akina Mdee, Silinde, Katambi, Slaa, Sugu, Lema hauwezi kutufikisha popote, Opportunists Ndio wamejaa huko upinzani, wanachowaza wapate ubunge wajikusanyie mali! The Only thing inaweza kutusaidia ni CCM kumeguka vipande vipande ( Nusura litokee Hilo 2015, na tunakumbuka shida waliyopata kwenye uchaguzi)

IMG_0401.png

hapa moja ya kiongozi wa upinzani anajaribu kupaka rangi ukuta,usionekane.

ameshindwa kabisa kabisa kusoma alama za nyakati.matokeo yake michango ya wananchi hapo chini imekuwa migumu sana kwa upande wake.
 
Hapo sasa ndiyo unakosea. Kwa sababu mtu au watu au Watanzania wengi hawakubaliani na wewe hawajielewi au ni waoga. Ni matusi kama haya kwa wananchi ambayo wanawafanya wananchi wasiuchague upinzani. Huwezi kunitukana kuwa mimi sijielewi au mimi muoga, alafu utegemee niwe upande wake. Kutafuta kura lazima unyeyekee, uwe mpole, ubembeleze. Lakini nyie wenzetu mnasjiona ndiyo mnajuwa kila kitu, kumbe kujuwa kwenu hakuwezi kuwafanya mkavuka. Ni wananchi tu watakaowafanye mvuke.

Ebu jiangalieni kwanza. Angalia lugha mnayotumia kwa wapiga kura watarajiwa. Mkishaona makosa yenu, rudini kwa wananchi, mtumie lugha ya kistaha, ili wananchi wawaone kama mna ukomavu wa kuendesha nchi. Mtu yeyote anayetanguliza matusi mbele, mtu yeyote anayeifuata maiti kaburini na kuitukana, huyo mtu kwanza hana hoja na pili bado hajakomaa kupewa uongozi.
Kwanza elewa. Mimi siko kwenye siasa kwa namna yoyote. Natoa maoni yangu kama raia asiye na chama wala upende wowote kwenye siasa za Tanzania. Upande wangu ni ''haki na fursa sawa kwa kila raia''. Kingine: naamini nchi inaweza kuendeshwa kwa mfumo wa chama kimoja na ikaenda vizuri iwapo wananchi wanajitambua na siyo woga! Kinachotakiwa ni wananchi kujua haki zao. Hili la kusema watanzania wengi ni waoga na hawajitambui ni kitu kilicho dhahiri na siyo tusi hata kidogo. Ni ukweli mchungu. Ila ''chawa'' wanaoishi kwa siasa kama wewe hili ni faida kwako hivyo hutataka liondoke. Bila hata kuzungumzia siasa, kuna haki nyingi za msingi zinakiukwa lakini wananchi wengi wamelala fofofo kama hakuna kinachotokea. Wewe hutakubali kwa sababu ujinga wetu wananchi ndiyo kula yako.
 
Jamaa umeandika vema. Yyte atakaeanza kumkosoa mama watu watamuona ana nongwa na ni muonevu na watahoji kwa nn aliufyata kwa mbabe jiwe? Mfano ni yule dada kule tweeter ambae watu walimbatiza jina la Ferain baada ya kumkosoa mama huku kwa jiwe akiwa ameufyata na vijitivii vyake vya mkononi kupigwa ban.


Wapinzani this time watakua ni loosers. Ishara nyingne niionayo ni bunge. Wabunge washasoma alama za nyakati na sasa wamejitwisha kazi ya upinzani kukosoa serikali na mama kaahidi hilo. So upinzani hautakua na hoja tena maana kila kitu kinafanyika. Mfano ji akina GWAJIMA, NAPE, GAMBO, MAKAMBA MUHONGO N.K
Amka utakojoa kitandani
 
Ukimkosoa Mama kwa hoja hana ujanja wowote , pamoja na yote huyu ni miongoni mwa walioharibu Katiba mpya hadharani na gizani , faili lake lipo , tunamwangalia tu atakachofanya
Suala ka katiba mpya binafsi naamini ni suala la wananchi au watu wasio na maslahi kabisa ya kisiasa kama kina Warioba.

Nakuhakikishia, hata leo CHADEMA au ACT wakifanikiwa kuingia madarakani kwa katiba hii hii ya 1977, hawataibadilisha. Zitabaki danadana tu.

Hakuna mwanasiasa mwenye madaraka asiyependa madaraka makubwa kama hayo yaliyomo kwenye katiba ya 1977.

Mimi naamini zaidi kwenye madaraka na maamuzi ya wananchi.
 
Hakuna kitu kinaamua siasa kama 'wakati'..
Wanasiasa wazuri ni wale wanaojua nyakati zinavyobadilika na kwenda na wakati uliopo ...

Watanzania walikuwa wamechoshwa mno na siasa za Magufuli...na uongozi wake kiujumla..
Kubanwa Uhuru wa kuongea
Kufokewa na kukaripiwa
Kutoa matamko Kwa ukali..
Kuzungumza Peke yake..
Kutokukosolewa ..
Kukosekana Kwa mijadala na majadiliano..
Na mengi yaliyoenda na hayo..

Ujio wa Samia umebadili siasa Kwa ujumla..
Samia hafoki anaongea Kwa upole na kushawishi ..
Anazungumzia mazungumzo na mijadala..
Hazuii kukosolewa badala yake anakaribisha kukosolewa Kwa serikali yake..

Kikubwa zaidi ni Mwanamke ..
Watu wanamtazama Kwa 'kumhurumia'..
Na kumpa 'all benefits of the doubts'..
Na kuelewa kuwa anapambana na mfumo dume...
Watu wengi wanaju hii nchi ngumu na wanajua Samia atahangaika kuweza kumudu ...still wanafarijika na 'kurudi Kwa Uhuru wa kuongea na kukosoa'..

Sasa kama wapinzani wanafikiri siasa za kumshambulia Rais na serikali yake zinalipa bado kama enzi za JK watakuwa wanakosea sana....
Sana Sana wataonekana 'hawana adabu'
Na wanajaribu 'kumuonea' 'Rais Mwanamke' baada ya 'kidume ' JPM
'kuwakomesha hadi wakaufyata'..

Siasa za kipindi hiki zinahitaji ubingwa wa hoja kwenye mijadala ya kistaarabu..bila
Kuwa 'boa' wananchi ambao walishachoshwa na Magufuli Sana Sana wanataka 'mzunguko' wa hela urudi kama ule wa JK....

Kuleta siasa za ulalamishi..
Siasa za uwana harakati.
Na siasa za Ku target watu na kuwashambulia bila kujua ..'role halisi' ya hao watu ni siasa ambazo zinakuwa 'outdated ' so fast...

Watu wanampenda Samia sio Kwa sababu ni kiongozi bora.. wanampenda Kwa sababu wanaona 'nafuu inakuja'
Upinzani ukicheza siasa za kuleta 'distraction'wakati watu wanasubiri nafuu ije ..hasira za wananchi zinaweza washukia wao.....

Siasa inaendana na nyakati.. wapinzani wanasoma nyakati??
Umeongea ukweli..japo sina wasiwasi. Upinzani upo na watu smart sana kama Mbowe
 
Umeongea ukweli..japo sina wasiwasi. Upinzani upo na watu smart sana kama Mbowe
Upinzani siyo chama ni wananchi.

Ukitaka kuwa na upinzani imara zungumza matatizo ya wananchi na wao watakuwa upande wako.

Na mtawala ukitaka kupoteza imani ya watu, endekeza danadana za uongo, chuki, unafiki na usiwasikilize wananchi.
 
Upinzani siyo chama ni wananchi.

Ukitaka kuwa na upinzani imara zungumza matatizo ya wananchi na wao watakuwa upande wako.

Na mtawala ukitaka kupoteza imani ya watu, endekeza danadana za uongo, chuki, unafiki na usiwasikilize wananchi.
Hakuna serikali isiyokuwa na madudu yanayoonekana wazi. Mambo ya kuongelea ni mengi, na mama sio malaika
 
Back
Top Bottom