Update: Mashtaka dhidi ya makampuni manne ya simu

Update: Mashtaka dhidi ya makampuni manne ya simu

Pambana kiongozi .... Nikiwakumbuka Airtel walichonufanyia 2015 napata hasira Sana.... MPAKA Leo Sina line yao KABISA na niliwashawishi watu wengine wawili ambao Mimi ndio nilifanya wawe na line zao wajitoe...

Ilikuwa hivi...Mimi nilikuwa napata 140,000# per month Kama communication allowance lakini inarushwa kwa mfumo wa Airtel aitime...

Kwasababu ya matumizi madogo na asante kwa vifurushi basi mara nyingine simu inakuwa hata na 400,000#ila airtime tu...

Sasa siku moja nikajiloga, usingizi umekata saa Tisa nikawaza nijiunge na bandle la internet niangalie movie...ilikuwa kuamkia jumamosi, nikajiunga bwana Bwana.....movie zikanoga nikaangalia Hadi saa nne asubuhi....

Nacheki salio ili nijiunge Tena nakuta Nina elfu 48 na chenchi kadhaa Kama salio .... Aisee nililaani Airtel, nikajilaani kea kuamka usiku....hi kitu iliniuma Sana mno .... Unaingiliaje airtime ya mtu bila kumjulisha......

Hao kwanza wapigwe faini za kutosha, Kama kuwagaia wananchi logistically Ni ngumu the pesa iende serikali I ifanye kitu Cha kumbukumbu....

Umefanya Jambo la kishujaa Sana, ingekuwa nchi yet inaweka historian ungewekwa kwenye upande wa mawasiliano.
 
Tabutupu,

Please revisit your skewed comments, vije, au na wewe ni stake holder wa moja ya makampuni tajwa.
 
Tatizo ndio lipo hapa tunachanganya mambo na kuweka kila kitu kwenye kapu moja kwenye mkataba ‘value of exchange’ ndani ya kampuni moja tu la simu vifurushi havilingani let alone huduma tofauti za biashara tofauti.

Muhimu hapo kuna mambo matano yanayoangaliwa kwenye ‘consensus in idem’ ili kampuni iwe na makosa lazima kuwe na ushahidi wa legal error (by contractual tests).

Kwenye vifurushi legal errors tatu ndio ambazo zinahusika:

Subject matter: wewe unadhani unanunua muda na data ambazo zinatakiwa zitumike mpaka ziishe, wakati wao wana offer minutes na data za kutumia ndani ya masaa waliyokuwekewa.

Bei; wewe unadhani hiyo ni bei ya data na minutes pekee; wao wanauza kifurushi ambacho kimeambatana na minutes, data and time limit kwa bei hiyo.

Nature: Wewe unadhani minutes na data ni independent, wao wanauza vyote ivyo kutumia ndani ya muda waliokuwekea umalize; usimalize juu yako.

Ni hivi ivyo vifurushi vingekuwa vimetangazwa vingine na wanachofanya ndio kungekuwa na tatizo la ‘legal error’, lakuweza kwenda mahakamani kwa madai ya consensus in idem.

Sasa tena ku compare sijui restaurant ambao wamekupa muda tu kwa ku book meza na kutumia, ukiisha na ujamaliza chakula ni haki yako kuondoka nacho similary Tanesco wanauza units ambazo hazina time limit.

In any contract the devil is in the details unatoa nini na kupewa nini which is exclusively that (unless were statute law provides other inclusive terms) lakini sio nani mwingine ana fanya nini.
Kindly revisits you law books!
 
Hongera sana mkuu,una moyo wa kusaidia wanyonge kweli,maana hizo kampuni za simu ni wezi wa mchana
 
Hongera sana kwa kutulinda walaji wa huduma hii,kwani tumeumizwa mno,na sasa inatosha.
->Isajili kabisa "communications consumer protections against"
 
Bundles ni bidhaa kama chips mayai ambapo unaponunua tu kanuni za mkataba zina apply.

Uwezi kwenda kununua zege usipomaliza ukamfuata muhudumu akurudishie chenji kisa umeshiba kati kati it doesn’t work that way.

Hivi vyuo vyetu avifundishi masuala ya contract law
kwahyo ni sahihi nikinunua zege muuzaji anipangia muda wa kulila?
 
Kaka hii vita ni kubwa sana zaidi ya unavyofikilia yaani big company zote za simu asee nikuomba mungu maana apo watamwaga pesa ya nguvu kukupinga na ata kujaribu kukupiteza atleast ingekua kampuni 1 ila zote nne
All the best kaka sisi mchakato wa kesi ukianza tutafurika uko mahakamani
wakimuhurumia sana watamwekea mlungula mezani aachane na kesi
 
Tunahitaji consumer protection groups na activists kama huyu zaidi.
 
Bundles ni bidhaa kama chips mayai ambapo unaponunua tu kanuni za mkataba zina apply.

Uwezi kwenda kununua zege usipomaliza ukamfuata muhudumu akurudishie chenji kisa umeshiba kati kati it doesn’t work that way.

Hivi vyuo vyetu avifundishi masuala ya contract law
Wewe unit zako za umeme unazonunua unapewa expire date?,naomba jibu tafadhali.
 
Mkuu, ukimalizana na makampuni ya simu naomba ushughulikie issue ya mahoteli yanayohudumia wasafiri wa mabasi. Yaani chips kavu tunauziwa 3000 kweli? Mkuu tunaomba utusaidie katika hili pia
 
Aidha, niliitwa na ndugu wa TCRA kitengo cha walaji. Nilifanya nao majadiliano kuhusu mambo haya na kuwaeleza nia yangu ya kuhakikisha Mtanzania analindwa. Nimeelewana nao vizuri.

Zaidi, wanaandaa kikao ambacho kitakuwa kati yangu, TCRA kitengo cha walaji, na makampuni yote ya simu. Mimi nilikusudia kuyashitaki makampuni manne(the big 4) lakini wao wamependekeza kikao kijumuishe wote. Ni jambo zuri na nimelipokea.
  • TCRA hawakuliona hilo kabla?
  • Kitu gani kimewafanya wakuite wakati suala lilikuwa baina yako na makampuni ya simu?
  • Je TCRA wana maslahi gani binafsi toka kwa makampuni hayo?
  • Nini kiliwafanya wakusubiri uanzishe mchakato na wao wadandie kwa mbele?
  • TCRA wakuajiri kwakuwa nimeona una uchungu na wananchi masikini kuliko wao.
 
kwahyo ni sahihi nikinunua zege muuzaji anipangia muda wa kulila?
Wewe unit zako za umeme unazonunua unapewa expire date?,naomba jibu tafadhali.
Nimeelezea post # 84 not all sales agreements are equal

It depends on the offer, muuza chips biashara yake aina masharti ya kula na wala TANESCO awauzi vifurushi isipokuwa independent units.

Tumuombe huyu brother afike mahakamani, atatupa mrejesho.
 
Hivi mnalazimishwa kujiunga vifurushi? Mbona haya ni masuala yaliyo wazi sana kibiashara? Vifurushi ni mkataba wa hiari wenye vigezo na masharti yake unayoyakubali kuyazingatia!!!
Huwezi mnyanganya sahani kisa muda wa lunch umeisha, halafu sio contract Law Ni "Law of Contract"
B
 
Back
Top Bottom