Unaweza kumtambua mchezaji gani?

Unaweza kumtambua mchezaji gani?

Hivi hizo nakala kuna sehemu zipo na mwenye hilo jarida yupo au ndo ishakuwa urithi
 
Alikuwa kipa alifanya kosa moja baada ndumilakuwili kumwambia angalia mpira huo akimaanisha audake sasa yeye lodilofa akaacha kuudaka akaanza kuuangalia mwishoe mpira ukaingia wavuni likawa goli wamefungwa. Kilichofatia hapo ikabidi wachezaji wenzie wa born town wamshushie kipigo. Yeye alijitetea kwamba ameambiwa aungalie mpira sio audake.

Mkuu kipa wa Born Town alikuwa Rasta, lodi alikuwa ni beki 5. Hiyo mechi naikumbuka, nadhani lodi ndo alimwambia Ras aangalie huo mpira, badala ya kuudaka Ras akauangalia unavyoingia golini.
 
Nakumbuka kuna game moja lilitokea varangati kali sana, sasa kwenye mikono HuiHui akawapiga roba jamaa wawili kwa mpigo halafu anawauliza "Kwani vipi wajameni".

Noma sana enzi hizo, kuna kipindi Mzee Meko alienda kwa Madiba kufanya majaribio na timu ya kule, sasa siku ya mechi ya Born Town vs Bush Stars ikabidi arudi kutoa sapoti, alifika mechi iko half time, ila mambo aliyoyafanya kipindi cha pili ilikuwa maajabu sana, nadhani kuna watu aliwachania mikeka, maana watu walikuwa wana uhakika Born Town atashinda game.

Hizi mechi nili bet sana enzi hizo
 
Wamiliki wa hayo magazeti wakiamua kurejea kuyachapisha kama archives watapata fedha nyingi.

Asante mleta uzi.
 
Wamiliki wa hayo magazeti wakiamua kurejea kuyachapisha kama archives watapata fedha nyingi.

Asante mleta uzi.

Mkuu Sani wamejaribu kurudi hapa karibuni lakini imeshindikana, sidhani kama wameendelea kutoa.

Unajua tunaozielewa hizi story ni sisi Old School ambao kwa sababu ya majukumu kusema upate muda wa kununua gazeti la katuni ni kazi sana, utakuta tunaishia kushangilia tukiona thread kama hivi tunakumbushana imetosha.

Na sasa hivi ulimwengu wa digital katuni watu wanazisoma FB, JF, WhatsApp na kwingineko kwenye mitandao.
 
Back
Top Bottom