Unaweza kumtambua mchezaji gani?

Unaweza kumtambua mchezaji gani?

Timu inaingia uwanjani na torori la fisi walioning'iniziwa mfupa kwa mbele.Dereva madenge.
 
Mkuu Sani wamejaribu kurudi hapa karibuni lakini imeshindikana, sidhani kama wameendelea kutoa.

Unajua tunaozielewa hizi story ni sisi Old School ambao kwa sababu ya majukumu kusema upate muda wa kununua gazeti la katuni ni kazi sana, utakuta tunaishia kushangilia tukiona thread kama hivi tunakumbushana imetosha.

Na sasa hivi ulimwengu wa digital katuni watu wanazisoma FB, JF, WhatsApp na kwingineko kwenye mitandao.
hapo ukimaliza upande mechi unahamia kwenye pambano LA zena na betina ... balaa lake si kitoto
 
Huu Uzi unanifanya niwe na huzuni sana maana kuna watu wengi sana walitangulia mbele ya haki tangu kipindi hicho.RIP
 
Mapung`o star wa timu na no9 tegemezi
Yule mzee wa kuruka vichwa yupo wapi hapi
 
Hahahaha!, enzi hizo school bus tunaiona kwenye movie Kama"war bus",
Pitieni na huh Uzi mpate mengi zaidi.
Unakumbuka nini katika enzi za gazeti la Sani?
Umezipata wapi mkuu,nami nikajikumbushe kidogo ......... (yaani kama vipi niwekee link niingie)

Zamani ilikua raha tupu

Sana huyu mwandishi wa vile vijarida (magazeti) alienda wapi? alikuwa mbunifu balaa. halafu watu tulivyokuwa tunapendana mmoja akinunua mnaazimana maana wengine tulikuwa hatuna kitu, utakuta gazeti limechoka lakini unakaukia kucheka.

Nimefurahi sana, nimekumbuka mbali sana...nilivosoma comments mbili tatu nikaamua niweke na Radio Tanzania , duh nikarudi mbali sana ...kama kuna mwingine anazo zingine aweke

kuna kaisi nyongise na zoba pia old is Gold

Hivi hizo nakala kuna sehemu zipo na mwenye hilo jarida yupo au ndo ishakuwa urithi
 
Ndumilakuwili kwa wizi alkua hatari yale majarida ndo yalkua na mechi kwa urefu zaid daah nilkua naokota vigazeti vya sani naigiliza kumchora kipepe na rungu lake yaan ilkua raha sana but now days hamna kitu ka hyo hdi sometym nilkua nahisi kama hao watu wapo hai
 
Komredi kipepe, mzee meko, kobelo, madenge,
 
Professional footballer alikuwa akicheza soka la kulipwa Bondeni(South Africa) anaitwa Meko. Anapiga penati balaa yaani anazunguka kama feni akiachia mkwaju kipa anaona maluelue tu.
 
Hahahaha!, soka ka siku hizi limekiwa soft sana, enzi hizo mabeki watata ndio wanapata namba!
Yaah kuna picha moja imeandikwa kutoka maktaba inamuonyesha almarhumu mohamed "machela "kajole alikuwa beki wa simba kafyeka nyasi mbele ya mrussia mmoja nyasi zimeruka juu yule kishoka kabaki kushangaa ilikuwa mechi ya kirafiki kisha muandishi pale juu kaandika "NANI KAZISAHAU VURUMAI ZA KAJOLE ?zamani forward khatari alikuwa anachezewa rafu anaumia kisha beki analia anaulizwa unalia nini? Beki anajibu nimemkosa! waqt huo forward anabebwa na machela kupelekwa nje.
 
Back
Top Bottom