Unaweza kumtambua mchezaji gani?

Unaweza kumtambua mchezaji gani?

Mimi chama langu lilikuwa Mafichoni United.......chini ya striker hatari sana Huihui
 
Mnachanganya mkuu mapung'o alikuwaga kwenye jarida la bongo humu staa wao alikuwa mzee meko na shati lake la maua anapiga vyenga golini kwake hadi kwa wapinzani
Kobelo alikuwa havai shati kweli?
 
Hapo kwa walio simama kutokea kushoto

Namuona Komled kipepe na Lodilofa

Kwa walio mstari wa mchini namuona Madenge akiwa anatoa tabasamu zuri kabisa..
Lodi lofa alikuwa anachezea town star, hapo kuna kipepe, golikipa madenge, mapung'o mzee kobelo wengine nimewasahau
 
Hapo namuona striker mkali mzee meko na mlishaji wake mido kisheti hui hui
 
Pia alikuwepo bob mazishi huyu alikuwa anacheza rafu sana (Uruguay )
Umenikumbusha kuna siku nilikua naongea na mwanangu hawa wa maskuli busi nikamwambia akileta mchezo leo ni uruguay uruguay tu akabaki anashangaa hilo neno enzi yetu lilikuwa maarufu, fujo, zali nk.
 
Sana huyu mwandishi wa vile vijarida (magazeti) alienda wapi? alikuwa mbunifu balaa. halafu watu tulivyokuwa tunapendana mmoja akinunua mnaazimana maana wengine tulikuwa hatuna kitu, utakuta gazeti limechoka lakini unakaukia kucheka.
John kaduma. Alisha fariki alikuwa mchoraji wa kiwango cha juu.
 
Umenikumbusha kuna siku nilikua naongea na mwanangu hawa wa maskuli busi nikamwambia akileta mchezo leo ni uruguay uruguay tu akabaki anashangaa hilo neno enzi yetu lilikuwa maarufu, fujo, zali nk.
Yaah waqt huo ukiambiwa jamaa wanacheza Uruguay ujue pagumu hapo zamani raha sana.
 
Nimefurahi sana, nimekumbuka mbali sana...nilivosoma comments mbili tatu nikaamua niweke na Radio Tanzania , duh nikarudi mbali sana ...kama kuna mwingine anazo zingine aweke
 
Back
Top Bottom