Unajua kwanini katika mikutano ya Rais Samia na viongozi wa dini na machinga hakuna aliyemweleza kuhusu kupanda kwa bei za vyakula?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Upon mfumumuko mkubwa wa za bidhaa nchini, maeneo yaliyoathirika Zaidi ni nishati na chakula.

Kupanda kwa bei hizi kulipaswa kuwa agenda za kujadiliwa kabla ya kujadili siasa. Mtu mwenye njaa ni mwepesi kurubuniwa akawa mwovu lakini aliyeshiba siku zote ukumbuka mkono uliomlisha na kuulinda usidhurike.

Wamachinga wanatoka kundi la watu wa vipato vya chini lakini walipokutana na Mhe Rais walijikita kwenye hoja zakitajiri. Hakuna alimweleza Mhe. Rais Kwamba watu Wana njaa na wakiwa na njaa nivigumu kujadili nao kesho yao maana wakati wanaugulia maumivu ya njaa wanashuhudia majirani zao waliopo nafasi za juu wakila na kusaza. Kwanini machinga awakuona mfumuko wa bei kama agenda kwenye kikao Chao?

Viongozi wa dini wanaongoza nafsi zetu ziweze kwenda Mbinguni. Katika Hali ya kibinadamu tunahitaji watu walioshiba ndio tuwape neno la Mungu na kupanga nao mipango ya Mbinguni. Maana yake Nini, hakuna kiaongozi wa dini ataongoza Misa masaa manne au zaidi huku akijua wazi familia yake Haina msosi. Hakuna kiongozi wa dini atazunguka kutoa huduma ya kiroho wiki nzima bila kuacha chakula nyumbani. Nilitegemea viongozi wa dini wamwombe Rais aeleze ana mkakati Gani wa kupunguza mfumuko wa bei za bidhaa?

Machief wengi ni watu wa Hali ya chini, wanaishi vijijini na wanaona Hali halisi ilivyo. Kipaombele kwao kilipaswa kumwambia Mhe Rais tusaidie tujue Kuna mpango gani wakupunguza kupanda kwa bei ya bidhaa? Kwa Bei hizi tutaweza kula? Tukila tutaweza kujenga nyumba za bati?

Kwanini bati lipande kutoka shs 22,000 Hadi 30,000 ndani mwaka mmoja na hakuna tamko la serikali kuhusu mfumuko huu? Haya maswali na mengine hakuna aliyeuliza maana yake Mhe. Rais anaamini sisi wananchi tumeshiba na tunaendelea kufanya maendeleo kumbe tunachoweza kufanya kutumikia tumbo.

Kwa Hali hii ndipo ninapojiuliza kwanini hakuna aliyezungumzia kupanda kwa kasi Kwa Bei ya ;
1. Vyakula
2. Mafuta ya kupikia
3. Vifaa vya ujenzi kama saruji,nondo,matati na marumaru

Nani amejiuliza umuhimu wa nondo kwenye miradi mikubwa inayojengwa? Kama nondo imepanda kwa kiasi kiki hivi Bado tunaamini gharama za miradi zitabaki palepale? Je kama kuna hujuma inafanywa Kwa wenye viwanda vya nondo kupata asilimia flani Nani atadhibiti kama viongozi wa dini wasipopata maono kama haya nakumweleza Rais?

Cement inatumika kwenye miradi yote mikubwa na imepanda mara dufu means gharama za miradi nazo zinapanda relatively to price ya malighafi, kwanini cement ipande Kwa kiasi hiki? Hakuna sarbotage hapa? Nani ananufaika na hii sabortage? Kama viongozi wa dini watashindwa kupata maono haya nakumweleza Mhe. Rais Nani atamsaidia Rais kupambana na kupanda kwa hizi gharama?

Nadhani nikiamini Kwamba hizi ni hujuma nitakuwa sahihi na nikiendelea kuamini Kwamba wanaokutana na Mhe Rais wanatumia muda mwingi kumsifia kuliko kumshauri ntakuwa sahihi. Kama wao waliopewa nafasi ya kukaa na mfalme wameshindwa kumsaidia naomba Mimi binafsi Beatrice Kamugisha nimsaidie Mhe. Rais Kwamba Kuna maswali mengi kwenye mfumuko wa bei, atume vyombo vyake vikafanye utafiti na wampe majibu ni kipi kimepelekea haya na Je hakuna watu au makampuni yanatumia miradi ya kimkakati kujipatia faida kubwa? Bei ya cement, bati na nondo ingekuwa chini naamini tungejenga madarasa mengi zaidi ya tuliyojenga na tusingeona picha za watoto wakikaa chini.
 
Imagine nchi haikaliki mauaji ni kila siku,vitu vinapanda bei,magaidi fake wapo jela wakati kuna magaidi original mtaani wanaua watu,Polisi sasa wanataka watu watii shuruti bila sheria badala ya kutii sheria bila shuruti na kadhalika halafu kuna lipaka limetulia linajiita kuwa ni Chui jike🐒🐒🐒
Weka hata heshima kidogo basi.
 
Imagine nchi haikaliki mauaji ni kila siku,vitu vinapanda bei,magaidi fake wapo jela wakati kuna magaidi original mtaani wanaua watu,Polisi sasa wanataka watu watii shuruti bila sheria badala ya kutii sheria bila shuruti na kadhalika halafu kuna lipaka limetulia linajiita kuwa ni Chui jike
Kwani dhalimu wenu bado yupo?

Si mnapumua nyie?
 
Wanaogopa vichambo, lakni viongozi ni zao la jamii hivi kwel hagaya haelewi hali iliyopo mtaani!?? Kwann haisemei!!? Alafu 2025 wanakuja mtaani kuomba kura...
 
Kati ya kelele ambazo wanasiasa wameamua kuzipuuza Ni kama hizi:

1- Mfumko wa Bei
2- Maisha yamekuwa magumu.

Haitatoea awamu ambayo watu watasema Maisha yalikuwa mazuri sana.
 
Kwanzaa hakuna kiongozi wa ccm anaye weza kukutana na Wananchi bila kutanguliza bahasha Kwanzaa kwenda kuweka mambo Sawa. Yaani wakitaka kufanya mkutono sehemu ni kama vile ni setting ya movies. Wanaandaa watu wa Kuja kwenye mikutano maswali ya kuuliza wanaandikiwa na kupractice namna ya kuyauliza na kuyajibu
 
Unachekesha sema utafute somo la ukulima wa kizazi kipya (Smart Farming).Vinginevyo utaachwa kwenye mataa.
 
Kuhusu mfumuko wa bei nchini, kwa uelewa wa kawaida, kuna uhusiano wa moja kwa moja wa kupanda bei ya mafuta na kupanda bei ya vitu. Very unfortunately hili lipo nje ya control ya serikali maana mafuta yapo controlled na bei kwenye soko la dunia. Hata hivyo zipo hatua zinazoweza kuchukuliwa kupunguza hii hali lkn itapelelekea kupungua kwa mapato ya serikali
 
Imagine nchi haikaliki mauaji ni kila siku,vitu vinapanda bei,magaidi fake wapo jela wakati kuna magaidi original mtaani wanaua watu,Polisi sasa wanataka watu watii shuruti bila sheria badala ya kutii sheria bila shuruti na kadhalika halafu kuna lipaka limetulia linajiita kuwa ni Chui jike🐒🐒🐒
Una pepo wewe.....roho mbaya haijengi
 
Kuhusu mfumuko wa bei nchini, kwa uelewa wa kawaida, kuna uhusiano wa moja kwa moja wa kupanda bei ya mafuta na kupanda bei ya vitu. Very unfortunately hili lipo nje ya control ya serikali maana mafuta yapo controlled na bei kwenye soko la dunia. Hata hivyo zipo hatua zinazoweza kuchukuliwa kupunguza hii hali lkn itapelelekea kupungua kwa mapato ya serikali
Hizo njia ni pamoja na kupunguza Kodi ya mafuta?
 
Vikao vina posho ukiuliza maswali magumu kikao kinachofuata huitwi.
Sure mfano ni kwa jamaa yetu Paskali, baadhi au hata yeye anadhani pale alipomuuliza mkuu swali gumu siku ile ikulu ni sifa but kile ndicho kilimuondoa kwenye reli mpaka leo yupo hivyo so, hata viongozi wa dini nk, wote wanajua na kufahamu fika, so wanapokuwa pale wanapiga makofi na kumtunuku ila ndani ya mioyo yao hawapo pamoja naye, lengo likiwa ni funika kombe...
 
Sure mfano ni kwa jamaa yetu Paskali, baadhi au hata yeye anadhani pale alipomuuliza mkuu swali gumu siku ile ikulu ni sifa but kile ndicho kilimuondoa kwenye reli mpaka leo yupo hivyo so, hata viongozi wa dini nk, wote wanajua na kufahamu fika, so wanapokuwa pale wanapiga makofi na kumtunuku ila ndani ya mioyo yao hawapo pamoja naye, lengo likiwa ni funika kombe...
Ukijifanya Critical thinker utakula unga
 
Kati ya kelele ambazo wanasiasa wameamua kuzipuuza Ni kama hizi:

1- Mfumko wa Bei
2- Maisha yamekuwa magumu.

Haitatoea awamu ambayo watu watasema Maisha yalikuwa mazuri sana.
Wakizungumzia watakuwa wanaonyesha udhaifu wa Hangaya na ubora wa mwenda zake.... hawataki kabisa kugusia hilo maana ni timu praise. Samia ni rais asiye jitambua wa kuitambua nafasi yake nchini... anaendesha nchi kimagumashi.
 
Back
Top Bottom