Unaishije na mwenza mwenye tabia ngumu?

Unaishije na mwenza mwenye tabia ngumu?

Ili umbadilishe
Huwezi kuachana na mtu kisa mlevi tu halafu Kila mtu atazikwa kivyake
Ndoa nyingi zinavunkika sanabu ya matarajio makubwa before
Mama zetu ss wakubwa walivumilia sana ndo mana tukakua wakiwa pamoja
Wewe una achana na mtu Leo kisa hajakupeleka cocokula mihogo?
Kwann pasiwe na street children na masingle mothers ?????
Huwezi kumbadilisha mtu mzima hata siku moja unatafuta matatizo na kujaza page za washauri wa mitandaoni tu!

Labda kama wamefika huko mbali kwenye ndoa sijui watoto, apambane kwa maombi na kwa maongezi mpaka amtoemo, tofauti na hapo aachane naye! Sisi huwa hatuvulimiwi tukiwa walevi why umvumilie yeye?
 
Nilipataga dogo mmoja wa hivi! Usije ukajichanganya mamaake! Hutoipenda! Hawa ndio wale hata mtoto akilia hakusaidii kumbembeleza kisa kanuna, ukipika hali, akirudi analala sebleni au harudi kabisa, usimvumilie mpuuzi wa namna hii kama hamjaingia kwenye ndoa inakuwa 2x!
Dogo alipoteza nafasi nzuri sana,naomba hiyo nafasi unipe mimi,sitakuangusha.
 
Hello wakuuu

Tupeane mbinu mnaishije na mwenza au mpenzi mwenye tabia ngumu ambapo unakuta io tabia inakukera au zinakukera sana na umejaribu kuongea nae mara kwa mara lakini haachi,,,na unakuta unampenda ila hiyo tabia ndo inakukwaza sana
Kuishi na mwenza mwenye tabia ngumu kunahitaji uvumilivu mkubwa, akili, na uwezo wa kulinda amani yako ya nafsi bila kupoteza mwelekeo.

Hatua ya kwanza na muhimu zaidi ni kukubali ukweli kwamba huwezi kumbadilisha mtu mzima, hivyo unapaswa kuacha kutumia nguvu zako kwenye kubadili namna unavyomgusa au unavyomjibu badala ya kuhangaika kubadili hulka yake.

Katika mawasiliano, ni vyema kuchagua vita vya kupigana kwa kupuuzia makosa madogo madogo, na pale dhoruba inapovuma, epuka kulumbana naye papo hapo....

Subiri hasira zitulie kisha zungumza kwa utulivu ukitumia kauli zinazoonesha hisia zako badala ya kumnyooshea vidole.

Pamoja na hayo, ni lazima uweke mipaka thabiti na mistari nyekundu dhidi ya tabia zisizovumilika kama vile matusi au vipigo, huku ukijifunza kusema hapana ili kuzuia kuonewa.

Mwisho kabisa, linda afya yako ya akili kwa kutochukulia tabia zake kama shambulio la kibinafsi kwako, tafuta muda wa kufanya mambo yanayokupa furaha nje ya mahusiano, na usisite kutafuta ushauri wa kitaalamu au kufanya tathmini ya mustakabali wa maisha yako ikiwa usalama wako wa kiakili au kimwili upo hatarini.
 
Huwezi kumbadilisha mtu mzima hata siku moja unatafuta matatizo na kujaza page za washauri wa mitandaoni tu!

Labda kama wamefika huko mbali kwenye ndoa sijui watoto, apambane kwa maombi na kwa mapngezi moaka amtoemo, tofauti na hapo aachane naye! Sisi huwa hatuvulimiwi tukiwa walevi why umvumilie yeye?
Sawa.
Lakini wewe una uhakika hakuna wanakesh walevi wanaovumiliwa na wenza wao? Mm nawajua wengine Hadi wapo sober na jamaa hawanywi kabisa
 
Sawa.
Lakini wewe una uhakika hakuna wanakesh walevi wanaovumiliwa na wenza wao? Mm nawajua wengine Hadi wapo sober na jamaa hawanywi kabisa
So far unawajua wangapi au ni huyo jamaa tu? Tena utakuta anamvumilia kwasabau fulani, labda mke wa ndoa au hana pesa, mwanaume huwa havumilii mwanamke ilimradi tu! Huenda huyo mke wake ana tatizo la kiroho au kisaikolojia basi! Tofauti na hapo hamvumiliagi nyinyi!
 
Kuishi na mwenza mwenye tabia ngumu kunahitaji uvumilivu mkubwa, akili, na uwezo wa kulinda amani yako ya nafsi bila kupoteza mwelekeo.

Hatua ya kwanza na muhimu zaidi ni kukubali ukweli kwamba huwezi kumbadilisha mtu mzima, hivyo unapaswa kuacha kutumia nguvu zako kwenye kubadili namna unavyomgusa au unavyomjibu badala ya kuhangaika kubadili hulka yake.

Katika mawasiliano, ni vyema kuchagua vita vya kupigana kwa kupuuzia makosa madogo madogo, na pale dhoruba inapovuma, epuka kulumbana naye papo hapo....

Subiri hasira zitulie kisha zungumza kwa utulivu ukitumia kauli zinazoonesha hisia zako badala ya kumnyooshea vidole.

Pamoja na hayo, ni lazima uweke mipaka thabiti na mistari nyekundu dhidi ya tabia zisizovumilika kama vile matusi au vipigo, huku ukijifunza kusema hapana ili kuzuia kuonewa.

Mwisho kabisa, linda afya yako ya akili kwa kutochukulia tabia zake kama shambulio la kibinafsi kwako, tafuta muda wa kufanya mambo yanayokupa furaha nje ya mahusiano, na usisite kutafuta ushauri wa kitaalamu au kufanya tathmini ya mustakabali wa maisha yako ikiwa usalama wako wa kiakili au kimwili upo hatarini.
Ahsante sana mkuu
 
So far unawajua wangapi au ni huyo jamaa tu? Tena utakuta anamvumilia kwasabau fulani, labda mke wa ndoa au hana pesa, mwanaume huwa havumilii mwanamke ilimradi tu! Huenda huyo mke wake ana tatizo la kiroho au kisaikolojia basi! Tofauti na hapo hamvumiliagi nyinyi!
Ndoa inaanzia kujuana?
Kuwa marafiki?
 
Weka Wazi Hizo Tabia Sasa Tufunguke
Apostle Kuna Muujiza Huku Umetokea
Ameishi Miaka 20 Na Mpenzi Mtata
Baada Ya Kutumia Mafuta Ya Upako
Mpenzi Ameacha Tabia Mbaya



Apostle Oops Piga Makofi Kwa......

Semaa Amen

Hello wakuuu

Tupeane mbinu mnaishije na mwenza au mpenzi mwenye tabia ngumu ambapo unakuta io tabia inakukera au zinakukera sana na umejaribu kuongea nae mara kwa mara lakini haachi,,,na unakuta unampenda ila hiyo tabia ndo inakukwaza sana
 
Hello wakuuu

Tupeane mbinu mnaishije na mwenza au mpenzi mwenye tabia ngumu ambapo unakuta io tabia inakukera au zinakukera sana na umejaribu kuongea nae mara kwa mara lakini haachi,,,na unakuta unampenda ila hiyo tabia ndo inakukwaza sana
ni muhimu sana kuvumiliana, kusameheana na kuchukuliana.

tusichokea kuambiana ukweli waziwazi, kusahihishana kwa upendo, kuelekezana kwa upole, kurekebishna kwa furaha na heshima huku tukiwa na subra:NoGodNo:
 
Back
Top Bottom