Unaishije na mwenza mwenye tabia ngumu?

Unaishije na mwenza mwenye tabia ngumu?

Huwezi kumbadilisha mtu mzima hata siku moja unatafuta matatizo na kujaza page za washauri wa mitandaoni tu!

Labda kama wamefika huko mbali kwenye ndoa sijui watoto, apambane kwa maombi na kwa maongezi mpaka amtoemo, tofauti na hapo aachane naye! Sisi huwa hatuvulimiwi tukiwa walevi why umvumilie yeye?
Mwanaume anapswha kuvumiliwa yule ni kichwa cha familia
 
Hakika ila wapo wanaobadilika. Bidada afunguke vizuri sababu halisi ya kununiwa. Kuna uwezekano jamaa kaamua kula buyu kwasababu kaona anapuuziwa. Or the guy is cheating and is looking for a reason to turn tables on her.
Hapo ndio tatizo linapoanzia, ndio maana bidada kasema hawezi kumuacha huenda kuna jambo kafanya ndiomaana jamaa kajinunisha! kwa ninavyojua siku hizi week 3 ni kuachana kimyakimya, au unasemaje mkuu?😁
 
Tabia ni kama ngozi ya mwili, huwezi kuibadili.
Kama umeamua kumpenda mpende tu na tabia zake ili usije kuwa surprised
 
Siwezi kuwa na kichwa cha familia kinachojinunisha kama dem mimi!
Mpaka kununa kuna jambo umemkera ukimpenda mtu kuna namna utajihidi usimkele mara kwa mara hasa kama unajua ananunanuna
 
Mpaka kununa kuna jambo umemkera ukimpenda mtu kuna namna utajihidi usimkele mara kwa mara hasa kama unajua ananunanuna
Baba eeh, siwezi kuwa na mtu wa namna hiyo! full stop.
 
Hapo ndio tatizo linapoanzia, ndio maana bidada kasema hawezi kumuacha huenda kuna jambo kafanya ndiomaana jamaa kajinunisha! kwa ninavyojua siku hizi week 3 ni kuachana kimyakimya, au unasemaje mkuu?😁
Kwa mahusiano ya nje ya ndoa wiki tatu ni muda mfupi sana aisee. Yote kwa yote, kikubwa ni sababu hasa inayowafanya mnuniane.
 
Hapo inabidi umpate mvumilivu kwakweli, kila mtu ana sector yake ya kuvumilia! Naweza kuvumilia kikojozi, mlevi.. ila sio mnunaji.. pole toto😛
Naomba turudiane, kwa kweli siwezi kuishi bila wewe Seran
 
Kwa mahusiano ya nje ya ndoa wiki tatu ni muda mfupi sana aisee. Yote kwa yote, kikubwa ni sababu hasa inayowafanya mnuniane.
Sababu kama ni ya msingi, ila kama kila kitu kidogo ananuna means kwa mwezi tuna week moja tu ya kufurahia?
 
Back
Top Bottom