Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 37,340
- 56,050
Huu ni umri wa kupumzika na kutafakari yale yote uliyoyatenda katika ujana wako, kuanzia kimasomo, kimaisha, kikazi n.k
Ni umri ambao hauna tija tena katika uzalishaji; ndio maana wengi wakifikia huo umri hulazimishwa kustaafu. Swali, ni wangapi wako tayari kustaafu wakifikia huo umri?
Kustaafishwa maana yake, kwa huo umri wako hauhitajiki tena katika uzalishaji, bali unatakiwa kupisha nguvu mpya zenye ufanisi katika utendaji.
Hii inatafsiri, huo ni umri wa kukataliwa na jamii, na jamii ikikukataa unatakiwa kuwa karibu na muumba wako; sasa najiuliza swali kwa umri huo, unajenga nyumba ya nini, ikiwa jamii haikutaki na unakuwa umebakiza miaka michache ya kuonana na muumba?
Ni umri ambao hauna tija tena katika uzalishaji; ndio maana wengi wakifikia huo umri hulazimishwa kustaafu. Swali, ni wangapi wako tayari kustaafu wakifikia huo umri?
Kustaafishwa maana yake, kwa huo umri wako hauhitajiki tena katika uzalishaji, bali unatakiwa kupisha nguvu mpya zenye ufanisi katika utendaji.
Hii inatafsiri, huo ni umri wa kukataliwa na jamii, na jamii ikikukataa unatakiwa kuwa karibu na muumba wako; sasa najiuliza swali kwa umri huo, unajenga nyumba ya nini, ikiwa jamii haikutaki na unakuwa umebakiza miaka michache ya kuonana na muumba?