Una miaka zaidi ya 65, unajenga nyumba ya nini?

Una miaka zaidi ya 65, unajenga nyumba ya nini?

Wewe jamaa either umesoma sana lakini unfortunately elimu yako hauifanyii kazi au haujasoma kabisa ndiyo maana kuna wakati unakuwa na uoni hafifu sana kwenye ishu ya makazi ambao kimantiki uoni huo ilibidi wawe nao watoto wadogo kama siyo wachanga.

Umesema nikiwa 65 natakiwa nisijenge nyumba ushauri wako nikalale nje chini ya mwembe?ok nikapange umejiuliza siku nikikosa kodi nani atanilipia hiyo kodi?je kama Mungu amenipa umri mrefu utanishauri tena nijiue kutokana na madhila ya kufukuzwa upangaji?wewe tulia tu kwenye hilo banda alilojenga mzee wako siku ndugu mligombanie ndiyo utajua ulikuwa unaandika vitu huvijui.
Ni umri wakuwa karibu na muumba wako
 
Hizi ndio akili za kiafrika sasa!

Waafrika tunajifikiria wenyewe.

Mwafrika ni mtu mbinafsi.

Mwafrika hawezi kupanga, kizazi kimoja au viwili mbele yake. 😁

Mwafrika haamini katika muda wala legacy.

Waafrika ndio jamii pekee inayoona ufahari kurithishana matatizo na umasikini.

Mtoa mada yupo sahihi ni Mwafrika halisi. Asibezwe 😄
 
Hizi ndio akili za kiafrika sasa!
Waafrika tunajifikiria wenyewe.
Waafrika hatuwezi kupanga, kizazi kimoja au viwili mbele.
Mtoa mada yupo sahihi ni Mwafrika halisi. Asibezwe 😄
Mkuu umemaliza kila kitu,

Aina ya mleta mada ukimpa issue ya kutengeneza Wealth generation anaweza kukuona kama vile hamnazo,
Halafu kila siku wanauliza kwanini Wahindi na Waarabu wanafanikiwa kimaisha?
 
Hoja yako imekaa kibinafsi sana,

Ni sawa na kusema kua una umri wa miaka 65 unapanda mti wa matunda wa kazi gani?
Hata ukijenga Nyumba ukiwa na umri wa miaka 20 tu,unaweza kufa baada ya miezi kadhaa tu na Nyumba usiifaidi,

Kama uwezo wa kujenga upo,jenga tu haijalishi una umri gani,
kwani ukijenga Nyumba wakati una umri mdogo,una uhakika gani kua utaishi kwenye hiyo Nyumba yako kwa muda mrefu?

Love the life u live
Live the life u love.
Kwa nini unajenga?
 
Kuna raha yake kuzeekea kwako tena unakua na mifugo km mbuzi,ng,ombe na kuku ...wajukuu wakija wanainjoi.Sasa unataka nizeekee kwenye nyumba ya mzee juma hata kuvaa taulo nitoke nje naona aibu 😇
Ulitakiwa ujenge kabla ya kufikisha huo umri; ukifikisha huo umri ni umri wa lala salama, ni umri wa kuwaza mambo ya mbinguni tu na si mambo ya kidunia tena.
 
Mkuu umemaliza kila kitu,

Aina ya mleta mada ukimpa issue ya kutengeneza Wealth generation anaweza kukuona kama vile hamnazo,
Halafu kila siku wanauliza kwanini Wahindi na Waarabu wanafanikiwa kimaisha?

Imagine Brother!
Inasikitisha. Mimi simlaumu mtoa mada, mtoa mada amewakilisha uhusika wa waafrika wengi sana.

Mwafrika ndie mtu pekee asieamini katika "succession plan" ya mali, ujuzi, maarifa na legacy. 😁

Sisi waafrika ndio tunaoshangaa familia za kitajiri, tunachukia matajiri na watu waliostaarabika bila kujua utajiri, ustaarabu ni urithi wa kizazi na kizazi. 😁
 
Imagine Brother!
Inasikitisha. Mimi simlaumu mtoa mada, mtoa mada amewsilisha uhusika wa waafrika wengi sana.

Mwafrika ndie ntu pekee asieamini katika "succession plan" ya mali, ujuzi, maarifa na legacy. 😁

Sisi waafrika ndio tunaoshangaa familia zabkitajiri, tunachukia matajiri na watu waliostaarabika bila kujua utajiri, ustaarabu ni urithi wa kizazi na kizazi. 😁
Upo sahihi kabisa mkuu,

Aina ya mleta mada ndio aina ya watu wanaokwapua hela za umma kwa ubinafsi tu,
hua wanawaza maisha yao tu na sio mustakbali wa nchi au mustakbali wa kizazi kitakachokuja.
 
Ulitakiwa ujenge kabla ya kufikisha huo umri; ukifikisha huo umri ni umri wa lala salama, ni umri wa kuwaza mambo ya mbinguni tu na si mambo ya kidunia tena.
🤣🤣🤣Huko mbinguni nani alisha fika na akajua kuna raha km hapa dunia ww injoi hapa hapa ya huko ni nadharia tu .jenga hata ukifa tupate kugombania mali sio unakufa kibudu unatuachia sabuwufa na kitanda 4×5.
 
Hizi ndio akili za kiafrika sasa!

Waafrika tunajifikiria wenyewe.

Mwafrika ni mtu mbinafsi.

Mwafrika hawezi kupanga, kizazi kimoja au viwili mbele yake. 😁

Mwafrika haamini katika muda wala legacy.

Waafrika ndio jamii pekee inayoona ufahari kurithishana matatizo na umasikini.

Mtoa mada yupo sahihi ni Mwafrika halisi. Asibezwe 😄
Unaacha legacy ili iwe nini, kwani ipo siku utafufuliwa? Aliyeacha legacy na ambaye hajaacha legacy, huko ahera wanaishije?​
 
Back
Top Bottom