Huwa nazima simu usiku kwasababu sipendi usumbufu usiku,usiku ni muda wa kulala na kuipumzisha akili,nitafute mchana kutwa lakini si usiku.
Suala la mama kuumwa usiku hiyo ni emergency ambayo haikutarajiwa,hata kama simu ikiwa on halafu akaumwa usiku na mnakaa mikoa tofauti,utafanya nini?,mwanadamu tumeumbwa na tulipewa akili ya kupambanua mambo,mama yako anaumwa na anajua uko mbali inapaswa ajiongeze kwa watu wa karibu yake au majirani,sidhani kama mama yako hana hata ndugu anayeishi naye!.
Huwa nazima simu usiku kwa kuepusha habari mbaya za ghafla zitakazopelekea kukosa usingizi,kama tujuavyo usingizi ni muhimu na ndiyo maana tukapewa masaa 24,yaani 12 kupiga kazi na 12 kupumzika!,kama kutakuwa na taarifa mbaya ni bora nikutane nayo asubuhi nikishaamka maana akili itakuwa fresh!.
Kwangu mimi kuzima simu usiku ni jambo zuri kuliko kuiacha on.
Ya kwamba una hofia majambazi?,hebu jiulize kwa jiografia ya nchi yetu hii na mikoa tunayoishi,umepata tatizo la kuvamiwa na majambazi usiku ukapiga simu polisi watafika kwa wakati huo?,hii nchi tunajuana sana na wala tusidanganyane,umpigie uenda jirani yako atakusaidia nini na wazee wana mijegeje mikononi?.
Kwa kifupi hatuzimi simu usiku ili itulinde,bali tunazima simu usiku ili kuepusha usumbufu na kupata muda mzuri wa kupumzisha akili.