Umuhimu wa kutozima Simu usiku

Umuhimu wa kutozima Simu usiku

Nimepokea simu nyingi za matatizo ya ndugu na jamaa zangu muhimu USIKU. Kuna yale ambayo unajikuta wewe ndio msaada wao na yale ya KIFO ambayo yatakufanya uwahi sehemu ya tukio.
Mfano Muislam akifariki usiku basi mapema kesho yake anazikwa, unapozima simu taarifa hizo utapata wakati washazika na utajiona mjinga wakati ungewahi hata kuzika.
Kuzima simu USIKU NI UPUMBAVU.
Uko sawa,Asante boss
 
Uzime usizime simu ilipangwa hivyo pindi tu tangu uzaliwe. Kwa iyo siyo eti kwasabab usizime simu usiku. Hata huko kuzima simu usiku na gari kupaki na kuwasha taa ilishapangwa long time time pindi tu ulipozaliwa. Chochote ufanyacho kilipangwa. Hata wewe kuandika hii sreedi leo ilishapangwa long time.
Kwahiyo tulage bata tuu tukipata nafasi kama Kwenda peponi ama jehanam pia ni mipango iliyopangwa zamani
 
Nakumbu Uncle alifariki usiku wa saa 6 pale sinza, mama mkubwa anakaa G'mboto, asbh kajiandaa anaenda zake Kisarawe ofisini kwake. Anafika minaki ndiyo anapatikana wakamuuliza vipi mbona hukupatikana usiku kucha. Akajibu nilizima simu wakati huo watu wa Moro wameshafika kitambo. Tukamuuliza unazimaje simu mtu mzima wewe umeona sasa.
Tabu tupu
 
Huwa nazima simu usiku kwasababu sipendi usumbufu usiku,usiku ni muda wa kulala na kuipumzisha akili,nitafute mchana kutwa lakini si usiku.

Suala la mama kuumwa usiku hiyo ni emergency ambayo haikutarajiwa,hata kama simu ikiwa on halafu akaumwa usiku na mnakaa mikoa tofauti,utafanya nini?,mwanadamu tumeumbwa na tulipewa akili ya kupambanua mambo,mama yako anaumwa na anajua uko mbali inapaswa ajiongeze kwa watu wa karibu yake au majirani,sidhani kama mama yako hana hata ndugu anayeishi naye!.

Huwa nazima simu usiku kwa kuepusha habari mbaya za ghafla zitakazopelekea kukosa usingizi,kama tujuavyo usingizi ni muhimu na ndiyo maana tukapewa masaa 24,yaani 12 kupiga kazi na 12 kupumzika!,kama kutakuwa na taarifa mbaya ni bora nikutane nayo asubuhi nikishaamka maana akili itakuwa fresh!.

Kwangu mimi kuzima simu usiku ni jambo zuri kuliko kuiacha on.

Ya kwamba una hofia majambazi?,hebu jiulize kwa jiografia ya nchi yetu hii na mikoa tunayoishi,umepata tatizo la kuvamiwa na majambazi usiku ukapiga simu polisi watafika kwa wakati huo?,hii nchi tunajuana sana na wala tusidanganyane,umpigie uenda jirani yako atakusaidia nini na wazee wana mijegeje mikononi?.

Kwa kifupi hatuzimi simu usiku ili itulinde,bali tunazima simu usiku ili kuepusha usumbufu na kupata muda mzuri wa kupumzisha akili.
Sawa mkuu
 
Unaweza arrange namna ya kuondoka kabla hujaenda kazini, kuna pesa nk, wanaweza fika hospitali dawa zikakosekana wakahitaji pesa ili utatue changamoto hiyo.
Unawaza kwa MAKALIO
Unawaza Kwa matako. Na unaongea assumption.

Kwani unadhani ikitokea wakapiga simu na hupatikni unafikiri hizo dawa hazitanunulikaa.Au wewe ndo umeshika uhai wake? Kwamba bila wewe kununua dawa Kwa kurusha Hela,Dawa haziwezi kupatikana.

Kweli unatumia matako kufikiria.Na kuwaza assumption ambazo hazipo.
 
Wewe acha tu kuna wakati nawaza mengi mpaka nasemms mungu akismua kuchukua basi anichukuwe mimi

Anakujaga na kurudi, mwezi mmoja tu anarudi.ingawa hawezagi maliza huo mwezi ila hata mimi siwezi muruhusu amalize zaidi ya mwezi mjini.
Mjini ni kukaa ndani hana kazi so anakosa mazoezi anaweza develop magonjwa ya uzembe.
Ila kijijini ni full mazoezi anakimbizana na wafanyakazi wake mashambani, mara kanisani, mara kwenye hisa, mara mifugo yake siku nzima yupo busy hayo ndo mazoezi yenyewe.
MTOTO pekee wa mama.Hongera.
 
Uzime usizime simu ilipangwa hivyo pindi tu tangu uzaliwe. Kwa iyo siyo eti kwasabab usizime simu usiku. Hata huko kuzima simu usiku na gari kupaki na kuwasha taa ilishapangwa long time time pindi tu ulipozaliwa. Chochote ufanyacho kilipangwa. Hata wewe kuandika hii sreedi leo ilishapangwa long time.

Kwa mantiki hio basi unamaanisha hata jamaa kuzima simu au kuwasha simu usiku ilishapangwa.

Au hio “kupangwa” inachagua tu baadhi ya mambo.

NB: Ilipangwa na nani?
 
Kuendekeza Michepuko ndo hasara yake hyo hakuna kitu kingine chochote.
 
Sisi wenye vimeo inakuwa shida kubwa mno kuacha simu on usiku.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom