Umesoma shule ya bweni wewe?

Umesoma shule ya bweni wewe?

Dah, aliyepitia Kigoma sec tuliita SUMU na cku nimerudi home likizo nakuta tena sumu cku ile ile niliyofika, kuita jina nililozoea kidogo ilete taharuki nyumbani
 
Makumira High School tulikuwa tunaikwepa hii hitu Tunaenda Canteen kwa Mama Kadogoo au kwa Rich au kwa Solo Sahani ya Wali Sh Mia tu...
 
Kama umesoma shule ya bweni ya serikali basi hili ni jambo la kawaida sana utazoea na kupiga shule kwa furaha. Pale Tosamaganga tulikuwa tunaita Bondo, kuna jamaa aliapa kwamba akijapata ajira atapiga marufuku ugali na maharage nyumbani kwake eti kwa kuwa tulikuwa tunakula mchana na jioni chakula hicho hicho kwa mwaka mzima.

Asikudanganye mtu kikipikwa chakula hicho kwake sasa hivi anakula!!

Tatizo siyo hiyo Nguna, hiyo sahani ya plastic tu. Kabla hujamaliza term, Bwana Afya atakuwa ameipiga ban. Kwa sababu, hao bacteria wanaozaana hapo basi. Lakini, Mungu mkuu akawalinda waja wake, hata tumbo halikungurma. Phuuuu
 
Dah, aliyepitia Kigoma sec tuliita SUMU na cku nimerudi home likizo nakuta tena sumu cku ile ile niliyofika, kuita jina nililozoea kidogo ilete taharuki nyumbani

Lazima ilete taharuki kwani utakuta mzazi kafight kwa nguvu zote mpaka kuupata huo ugali na wewe unakuja kuuita sumu!
 
Dah, aliyepitia Kigoma sec tuliita SUMU na cku nimerudi home likizo nakuta tena sumu cku ile ile niliyofika, kuita jina nililozoea kidogo ilete taharuki nyumbani

Hahah, made my night mkuu.
 
Kama umesoma shule ya bweni ya serikali basi hili ni jambo la kawaida sana utazoea na kupiga shule kwa furaha. Pale Tosamaganga tulikuwa tunaita Bondo, kuna jamaa aliapa kwamba akijapata ajira atapiga marufuku ugali na maharage nyumbani kwake eti kwa kuwa tulikuwa tunakula mchana na jioni chakula hicho hicho kwa mwaka mzima.

Asikudanganye mtu kikipikwa chakula hicho kwake sasa hivi anakula!!

Mzumbe sec hii kitu noma tuliita ngema, kila siku mchana toka uingie shule mpaka unaondoka, vinginevyo ukazamie sherehe za dini Mzumbe university au ubalozini.....hahahaha tumetoka mbali.
 
Malangali Secondary Early 1960s wapi Comrade wangu Joseph Mungai Governor na Professor Peter Msola enzi hizo Tukimwita Chif Msola!
 
Makumira High School tulikuwa tunaikwepa hii hitu Tunaenda Canteen kwa Mama Kadogoo au kwa Rich au kwa Solo Sahani ya Wali Sh Mia tu...


Umemsahau necha.

Mama Mzungu sasa ni mgonjwa hawezi kwenda skuli wanasema ni miguu.

Na wewe ulikuwa uking'ang'ania gamba kwenye mgao wa slesi?
 
Pale Mazengo ilikuwa kawaida kwenye maharage kukutana na top layer ya utando wa mafuta mekundu na wale wadudu kenye mchuzi wa maharage. Nimemkumbuka Head Master Mkoba na second wake Mkwizu, duh long time sana!
 
Umenikumbusha enzi za MALANGALI HIGH SCHOOL (A-level) tulikuwa tunaita Ngunga.....siku ya nyama j.tano na jpili ndo ilikuwa ahueni yetu ila siku nyingine zote za mandondo ilikuwa majanga matupu.
 
Busima wengi walitokea sehemu za nyamatare, kibini na ile mitaa karibu na kambi ya jwtz ya zamani maeneo ya sda church, ama kweli tumetoka mbali sana.

Mkuu ujakosea na wengine walitokea maeneo ya Kigera umepita pale nini
 
maua seminary tulikuwa tunauita Bondo, wali tulikuwa tunauita Chena
 
Mkuu ujakosea na wengine walitokea maeneo ya Kigera umepita pale nini

Mkuu nimepitia hapo miaka flani kipindi hicho ikiwa bado ni co-education, nakumbuka ule mlima ulioko nyuma ya madarasa ukiwa kama unataka kuteremka kuelekea shule ya msingi nyamatare, kuna vijana walikua wanafanya vituko sana mle.
 
Pale Mazengo ilikuwa kawaida kwenye maharage kukutana na top layer ya utando wa mafuta mekundu na wale wadudu kenye mchuzi wa maharage. Nimemkumbuka Head Master Mkoba na second wake Mkwizu, duh long time sana!

Mkuu lini umepita pale complex? Dah huwa nkikumbuka bweni la COSOVO aka white house
 
Bad luck to me, i have never experience this things, i wish ningesoma nyumbani tanzania. Mnaniumiza zaidi mnaposimulia habari za national service. NATAMANI. But i'm old now and i can not redo it.
 
Mkuu nimepitia hapo miaka flani kipindi hicho ikiwa bado ni co-education, nakumbuka ule mlima ulioko nyuma ya madarasa ukiwa kama unataka kuteremka kuelekea shule ya msingi nyamatare, kuna vijana walikua wanafanya vituko sana mle.

Ok mkuu nimekupata hata mie nilipita hapo wakati huo mkuu alikuwa Salvatory SB Magesa umenikumbusha mbali sana mkuu hasa kipindi cha umiseta.....!!!
 
Back
Top Bottom