Umemsikia MUGABE alichomwambia OBAMA.?

Umemsikia MUGABE alichomwambia OBAMA.?

Whether ushoga ni genetic au si genetic is irrelevant.

The relevant thing is, in a society that aspire to be democratic, people should have the freedom to choose how they live, as long as their freedom does not interfere with other's freedom.

Mtu akiniambia ana tatizo na gay's kuji advertise na kufanya ma parade ya "public displays of affection" naweza kumsikiliza, kwa sababu hilo linaweza ku involve kuingiliwa kwa uhuru wake wa kutotaka kuona gay parades, na labda kuingilia watoto wake kuwa influenced.

Vivyo hivyo mtu akiniambia hapendi kuona straight people waki kiss in public, kwa msingi huo huo, naweza kumsikiliza. Kwa sababu kuna mambo kibao yana play hapo, habari za minors, habari za watu wenye different religious beliefs, kuna hata hoja ya kwamba straights ku kiss in public kunaweza kuwa offend gays kama gay parades zinavyoweza kuwa offend straights.

Lakini hii habari ya kuwatungia sheria watu wazima, watu wameamua wenyewe kufanya mambo yao ya kulalana kwa jinsia moja, in private, tunapata wapi ushujaa wa kuanza kuwafuatilia kwa sheria katika jambo ambalo ni private kama hili?


Sorry mkuu, nilikuwa naku-quote wewe hapo juu ila nikam-quote bwa'nchuchu.
Kifupi tu ni kwamba tunakosa kifungu mujarab cha kuwafungia hawa jamaa(mashoga) ila ukweli ni kwamba wanayoyafanya kama kuoana kwa ndoa rasmi makanisani kunaathili sana muelekeo wa jamii zetu, so some how bora tuwabane kwakuwa wanachopigia kelele kina madhara kwa jamii na hakiendani na asili ya kimaumbile.
 
Hujajibu hoja.

Ungependa hawa mashoga wakuamulie wewe utalala na nani na utalala naye vipi?
Kiranga hebu twende taratibu. Kwanza suala la nani anaamua nini kwenye jamii haliko kwa namna unavyotaka kuliweka na ndiyo maana kwa nchi kama Marekani mtoto aliye chini ya miaka 18 hawezi kuamua chochote bila idhini ya anayemsimamia lakini kinyume chake sivyo (Msimamizi anaweza kuamua chochote bila idhini ya mtoto/watoto anaowasimamia). Na ndiyo maana kuna mamlaka zilizowekwa na kukubalika na jamii husika kufanya maamuzi na kuna taratibu za kuamua mambo.

Kulingana na utaratibu uliopo, jamii husika huweza kuamua kuwa tabia fulani ni mbaya, kwa mfano hapa ni ushoga. Uamuzi huo hauwafanyi walio na tabia hizo kuwa na uwezo wa kuamulia wengine. Kwa hiyo hapa hoja tunayojadili ni ushoga, hivi wewe kwa akili zako kama mtu anapinga ushoga unadhani kuna nafasi yeyote ya yeye kukubali kuamuliwa mambo na watu wenye tabia za ushoga?

Kitu kingine, suala la mtu kuitwa mtu mzima halimfanyi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi katika kila jambo, kwa hiyo suala la kusema ni maamuzi binafsi inategemea na maamuzi yenyewe. Ndiyo maana serikali nyingi zimeharamisha madawa ya kulevya, ingawa ni uamuzi wa mtu mwenyewe kutumia.

Mimi sipendi ushoga, kwa sababu haya mambo yamepelekea sasa hivi mtu anaweza kuuliza una bwana. Wewe naona ushazoea hayo maswali, ndio maana unaona poa tu.
 
Kiranga hebu twende taratibu. Kwanza suala la nani anaamua nini kwenye jamii haliko kwa namna unavyotaka kuliweka na ndiyo maana kwa nchi kama Marekani mtoto aliye chini ya miaka 18 hawezi kuamua chochote bila idhini ya anayemsimamia lakini kinyume chake sivyo (Msimamizi anaweza kuamua chochote bila idhini ya mtoto/watoto anaowasimamia). Na ndiyo maana kuna mamlaka zilizowekwa na kukubalika na jamii husika kufanya maamuzi na kuna taratibu za kuamua mambo.

Inaonekana hunisomi, kama unanisoma hunielewi, kama unanielewa unaendekeza ubishi tu.

Nimeandika mara kadhaa kuhusu habari za minors, nikaongelea habari za watoto kama neno "minors" labda litawapiga chenga wengine.

Watoto habari za kujamiiana vyovyote haziwafai, hawatakiwi kuzijua nje special cases za madarasa ya baiolojia.

Kwa hiyo suala la watoto si suala la whether the issue is about gay people or not.

Watoto hawatakiwi hata kuwa exposed kuhusu habari za kujamiiana katika ya mtu mume na mtu mke.

Kwa hiyo kuhusu watoto huna argument, your point is moot.

Kuna post nimepost leo hii hii, less than 12 hours ago, nimeongelea kuto support gay parades wala straight people's public display of affection kwa sababu nina strong concerns kuhusu kuwa expose watoto kwenye mambo ya kujamiiana (haijalishi straight au gay) kabla ya muda wao.

You have no point there as far as I am concerned.


Kulingana na utaratibu uliopo, jamii husika huweza kuamua kuwa tabia fulani ni mbaya, kwa mfano hapa ni ushoga. Uamuzi huo hauwafanyi walio na tabia hizo kuwa na uwezo wa kuamulia wengine. Kwa hiyo hapa hoja tunayojadili ni ushoga, hivi wewe kwa akili zako kama mtu anapinga ushoga unadhani kuna nafasi yeyote ya yeye kukubali kuamuliwa mambo na watu wenye tabia za ushoga?

Swali la msingi hujalijibu.

Kuhusiana na watu wazima, kwa nini mtu mzima mmoja ampangie mtu mzima mwingine kuhusu nani anatakiwa kulala naye na anatakiwa kulala naye vipi?

Na kama unakubali mtu mzima mmoja kumpangia mwingine, kwa maana straight people wapige marufuku kisheria habari za gay relationships, kwa nini iwe sawa kwa upande huo tu na gays nao wasiwe na haki ya kupiga marufuku straight relationships?

Unataka kufanya "Mkuki mtamu kwa nguruwe, kwa binadamu mchungu"?

Swali la muhimu kabisa ni hili, je, inafaa kwa mtu mzima mmoja kumuamulia mtu mzima mwingine alale na nani na alale naye vipi?


Kama unajibu ndiyo, jibu lako haliishii kwenye gay/ straights tu.

Utajikuta umeruhusu wazungu wabaguzi waseme kwamba hawataki weusi waoe wanawake wazungu.

Au vichaa wanaotaka kuchanganya rangi za watu wote wa dunia wakataze watu weusi kuoana na watu weusi, iwe ni lazima kwa kila mtu mweusi kuoa/ kuolewa na mtu wa rangi tofauti.


Once you accept that premise, it's a slippery slope.It can take you anywhere.


Kitu kingine, suala la mtu kuitwa mtu mzima halimfanyi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi katika kila jambo, kwa hiyo suala la kusema ni maamuzi binafsi inategemea na maamuzi yenyewe. Ndiyo maana serikali nyingi zimeharamisha madawa ya kulevya, ingawa ni uamuzi wa mtu mwenyewe kutumia.

Unafananishaje madawa ya kulevya na gay relationship?

Wazungu wangeweza kutumia argument yako kusema hawa watu weusi hawajakomaa kufanya maamuzi sahihi, tuwabakishe wawe katika makoloni tu, tukiwapa uhuru ni sawa na kuwaachia watu wasio na akili timamu wajidunge madawa ya kulevya.

Unatumia kigezo gani kusema huyu mtu ana uwezo wa kufanya maamuzi yake na huyu hawezi inabidi jamii imfanyie maamuzi?

Moja ya argument inayotumiwa dhidi ya gays ni kwamba homosexuality is unnatural, sasa kama ni hivyo, na hawa ni watu unnatural, kwa nini hamuwaachi wakamalizike vizazi vyao huko kwa kuchukuana wenyewe kwa wenyewe bila uwezo wa kuzaliana?

Mnataka kuwalazimisha waende kuoa na kuolewa ili iweje? Ili wajaze dunia watu unnatural?


Mimi sipendi ushoga, kwa sababu haya mambo yamepelekea sasa hivi mtu anaweza kuuliza una bwana. Wewe naona ushazoea hayo maswali, ndio maana unaona poa tu.

Sio wote wanaouliza "una bwana" wanaweza kumaanisha bwana wa ushoga, mlokole anaweza kukuuliza "u na bwana" akimaanisha kwamba , je umemkubali bwana Yesu Kristo?"

Mimi binafsi siukubali ushoga, kwa sababu nawapenda sana wanawake na sioni inakuwaje mwanamme ampende mwanamme. Lakini hilo halimaanishi kwamba siwezi kumtetea anayependa ushoga kivyake vyake bila kunihusisha mimi. Namtetea awe na haki yake kama mimi nilivyo na haki yangu.

Speaking on The NAZI progroms...

Martin Niemöller is perhaps best remembered for the quotation:

First they came for the Socialists, and I did not speak out--
Because I was not a Socialist.
Then they came for the Trade Unionists, and I did not speak out--
Because I was not a Trade Unionist.
Then they came for the Jews, and I did not speak out--
Because I was not a Jew.
Then they came for me--and there was no one left to speak for me.

Martin Niemöller: "First they came for the Socialists..."

Wataanza na gays, who knows who will be the next target if the tradition of personal freedom is not vigorously advocated for.

I don't want to be too late when they come for the diaspora crew/ Sukuma/ atheists, and no one with guts to speak for me is left.
 
Kwanza suala la nani anaamua nini kwenye jamii haliko kwa namna unavyotaka kuliweka na ndiyo maana kwa nchi kama Marekani mtoto aliye chini ya miaka 18 hawezi kuamua chochote bila idhini ya anayemsimamia lakini kinyume chake sivyo (Msimamizi anaweza kuamua chochote bila idhini ya mtoto/watoto anaowasimamia). Na ndiyo maana kuna mamlaka zilizowekwa na kukubalika na jamii husika kufanya maamuzi na kuna taratibu za kuamua mambo.

Yaani unalinganisha watoto na watu wazima wenye utashi, ridhaa, hiari, na ukomavu wa kiakili wa kuweza kujiamulia mambo yao wenyewe? Good grief! Kweli mtu ukiishiwa hoja ama unaanza kuhaha au unaishia kutoa viroja tu.

Kulingana na utaratibu uliopo,

Utaratibu gani? Upo wapi?

jamii husika huweza kuamua kuwa tabia fulani ni mbaya, kwa mfano hapa ni ushoga.

Ubaya wa ushoga, ambao ni jambo binafsi kabisa (na hususan kama wewe siyo shoga na ushoga wa wengine haukuhusu kwa namna yoyote ile) ni nini ukilinganisha, kwa mfano, na ubaya wa ulevi, uzinzi, ufisadi, na ujambazi?

Uamuzi huo hauwafanyi walio na tabia hizo kuwa na uwezo wa kuamulia wengine.

Na hao wanaoamulia wengine huo uwezo na mamlaka ya kufanya hivyo (kuwaamulia wengine) wametoa wapi?

Kwa hiyo hapa hoja tunayojadili ni ushoga, hivi wewe kwa akili zako kama mtu anapinga ushoga unadhani kuna nafasi yeyote ya yeye kukubali kuamuliwa mambo na watu wenye tabia za ushoga?

Kama huyo mtu anayepinga ushoga kamwe hatakubali yeye kuamuliwa mambo yake na watu wenye tabia za kishoga iweje yeye aone ni sawa kwake yeye kuwaamulia mambo watu wenye tabia za kishoga? Kuna mantiki kweli hapo?

Maana kama wewe hutaki kuamuliwa mambo yako na watu basi na wewe achana na hao watu. Acha kuwafuatilia, acha kuwananga, ishi maisha yako kivyako vile ambavyo upendavyo na acha wengine ambao wako tofauti na wewe waishi wapendavyo.

Hii dunia imejaa watu wa kila anuai. Kama kila mmoja wetu akiamua kuwa hampendi fulani kwa sababu huyo fulani anapenda kufanya mambo fulani fulani ndani kwenye faragha ya nyumba yake ambayo yeye hayapendi na hivyo kuanza kumuamulia nini cha kufanya na nini cha kutokufanya akiwa ndani mwake, basi hii dunia isingekalika kabisa.

Hivyo ni vyema na busara kuwa na modus vivendi ambayo itaruhusu watu walio tofauti kuishi pamoja bila kubugudhiana na mwanzo wa maelewano kama hayo ni kuheshimu wengine walio tofauti na wewe hata kama hukubaliani na wayafanyayo.

Kitu kingine, suala la mtu kuitwa mtu mzima halimfanyi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi katika kila jambo, kwa hiyo suala la kusema ni maamuzi binafsi inategemea na maamuzi yenyewe.

Maamuzi ya mtu mzima ambayo hayana madhara kwa watu wengine, tena ambayo yeye anaamua ili kujipa kitu kile roho inapenda, wengine yanawahusu nini? Wewe utafurahi ukianza kuamuliwa nani na nani awe mpenzi wako? Kama unampenda Fatuma na serikali inasema huwezi kumpenda yeye, mpende Saada, utafurahi?

Ndiyo maana serikali nyingi zimeharamisha madawa ya kulevya, ingawa ni uamuzi wa mtu mwenyewe kutumia.

Hivi kweli unalinganisha athari za madawa ya kulevya na ushoga? Kweli kabisa?

Mimi sipendi ushoga, kwa sababu haya mambo yamepelekea sasa hivi mtu anaweza kuuliza una bwana. Wewe naona ushazoea hayo maswali, ndio maana unaona poa tu.

Kama hupendi ushoga, sawa, baki ulivyo. Ila wale wanaopenda nao waache wapende wanachopenda.

Je na wao wakiamua kukulazimisha ufuate kile wapendacho wao kwa vile hawapendi kile upendacho wewe, utafurahi?

Ishini kivyenu na acheni wengine waishi kivyao. Kwa nini mnataka kuingilia maisha ya watu?
 
Sorry mkuu, nilikuwa naku-quote wewe hapo juu ila nikam-quote bwa'nchuchu.
Kifupi tu ni kwamba tunakosa kifungu mujarab cha kuwafungia hawa jamaa(mashoga) ila ukweli ni kwamba wanayoyafanya kama kuoana kwa ndoa rasmi makanisani kunaathili sana muelekeo wa jamii zetu, so some how bora tuwabane kwakuwa wanachopigia kelele kina madhara kwa jamii na hakiendani na asili ya kimaumbile.

Obviously jamii yako si yao.

Kwa nini unalazimisha jamii yako iwe yao kama mnakosana hapo?
 
mzee ana majibu magumu!!!

mungu mbariki mgabe na wazimbabwe, hata kama wamfanyie hujuma kiasi gani bado ajaonekana ni the best ever president after mandela.
 
mnamsifia mjinga huyo alichukuwa nchi ikiwa first world kaifanya third world na nusu ya wananchi wake wameishia ukimbizini kuwa manamba..poleni kwa ujinga

wewe jamaa ni mtutsi halafu pia shoga...dahh,!!
Kweli duniani kuna mambo.
 
Kwangu mimi naona hapa kumekuwa na 'ubishani' na wanaoishi magharibi na wale wanaoishi 'nyumbani'. Kwa sisi wa nyumbani, huu ni mfumo wa maisha ambao tunapata ugumu kuukubali. Sasa nyie wenzetu wa magharibi kwa sababu mmeshapata eksiposha ya kuona haya mambo ni ya kawaida, nafikiri muendelee kuwasapoti hao wa huko huko.

Huku nyumbani tuna mambo yanayotuumiza kichwa kuliko issue za ushoga...jamani kama mmesahau, maji safi ya kunywa ni issue, hospitali utata, umaskini bin ufukara usiseme, na issue za ushoga nazo zituchanganye kichwa! Binafsi yangu, nisingependa kuona uzao wangu unaingia kwenye adha hii, na mara nyingi watoto wetu ni matokeo ya jamii inayotuzunguka....kwa hili, tunaomba huu utamaduni ubakie huko huko sisi hapana....
 
Kwangu mimi naona hapa kumekuwa na 'ubishani' na wanaoishi magharibi na wale wanaoishi 'nyumbani'. Kwa sisi wa nyumbani, huu ni mfumo wa maisha ambao tunapata ugumu kuukubali. Sasa nyie wenzetu wa magharibi kwa sababu mmeshapata eksiposha ya kuona haya mambo ni ya kawaida, nafikiri muendelee kuwasapoti hao wa huko huko.

Huku nyumbani tuna mambo yanayotuumiza kichwa kuliko issue za ushoga...jamani kama mmesahau, maji safi ya kunywa ni issue, hospitali utata, umaskini bin ufukara usiseme, na issue za ushoga nazo zituchanganye kichwa! Binafsi yangu, nisingependa kuona uzao wangu unaingia kwenye adha hii, na mara nyingi watoto wetu ni matokeo ya jamii inayotuzunguka....kwa hili, tunaomba huu utamaduni ubakie huko huko sisi hapana....

Mkuu umeangalia hii issue kwa busara fulani na ingawa tunaweza kutokubaliana kwa minajili ya issue yenyewe, naweza kuelewa kwa nini hatukubaliani kwa namna ile ile ulivyochambua sababu za kutokubaliana kwetu.

Kuna divide kati ya watu wa nyumbani na watu wa diaspora. Or to be precise, watu walio capture the zeitgeist na wale ambao wanaishi in the past.

Kikwete said it best, at the current rate, this is a matter of time, haya mambo yatakubalika halafu mtaona the sun still rises in the east, that it was much ado about nothing.

New York City kuna gays kibao, na kuna Jehovah Witnesses kibao. Utakuta ofisini yule pale gay, yule pale Jehovah Witness, wote wamesoma "Employee Handbook" wanajua wana uhuru gani na mipaka ya uhuru wao ni ipi, na kazi inaendelea bila rabsha, kila mtu anamuheshimu mwenzake.

Tena nyie mnaopinga haki za hao gays ndio mnawapandisha chart, sasa hivi wanataka kufanya gay rights ziwe kama ubaguzi dhidi ya watu weusi ulivyokuwa miaka ya zamani. Wanasema vyote ni ubaguzi dhidi ya minorities tu.

Watu wa diaspora, mimi kwa mfano, washaona kwamba hata kama mtu personally hufagilii mambo ya same sex relationship, kuwapa hawa watu haki zao si mwisho wa dunia.

Mimi naweza kuwa mpenzi wa Coca-Cola na sipendi Pepsi. Lakini hilo halimaanishi kwamba, kwa kuwa mimi napenda Coca na sipendi Pepsi, basi nikulazimishe na wewe upende Coca na usipende Pepsi. Kwa nini nikulazimishe kitu ambacho hukipendi?

Hapo bongo mbona tushakuwa na gay people waliopewa presidential appointments (waliokuwa presidential appointees)? Ina maana marais wetu hawakujua kwamba hawa watu ni gay?

Unaposema huku nyumbani kuna mambo yanayotuumiza kichwa kuliko issue za ushoga nakubaliana na wewe kabisa. Hapo ndipo unagusia mzizi wa beef yangu na watu kama kina Mugabe.

Mugabe kashindwa ku address issues za muhimu za kiuchumi za Zimbabwe. Zimbabwe kuna noti ipo kwenye common circulation ya Z$100,000,000,000,000. Watu wangapi wanajua kuisoma hiyo namba?

Tatizo unalolisema na mimi naliona hilo hilo. Katika nchi zetu masikini zenye matatizo hayo uliyoyataja yote, kwa nini viongozi wetu wachukue muda wao mwingi na energy kubwa sana kupinga ushoga?

Ukichunguza sana utaona ni kwa sababu wameshindwa kutatua matatizo ya kweli ya watu, sasa wanataka kutengeneza matatizo artificial ambayo ni rahisi ku rally waafrika ambao hawana elimu wala exposure.

Ukisema unaomba utamaduni ubakie huku huku, inabidi ufanye kazi kutetea utamaduni wako sio useme tu. Waafrika tumekuwa rahisi kusema lakini wavivu kufanya.

Ukitaka utamaduni wa magharibi ubaki huku huku, piga marufuku mitumba, endeleza viwanda vya nguo vya Afrika ili msivae nguo zilizokuwa designed na gay people (top designers Marekani na Ulaya ni gay people).

Pia pigeni marufuku filamu za Ulaya na Marekani, kwa sababu top producers, directors, actors financiers etc wamo hao hao gays, tena ukichunguza kwenye movies na series/ muziki siku hizi gay rights themes ziko prominent sana. Kuna mtu kachukua award ya hip hop mwaka huu kwa wimbo unaotetea gay rights. Gay rights zimefika mpaka kwenye hip hop siku hizi, hip hop is one of the most homophobic genre.

Kwa hiyo fungeni mipaka na dunia ya magharibi, anzisheni internet yenu, movies zenu, muziki wenu etc.

Otherwise mtakuwa mnafanya mchezo wa unafiki wa "Baniani mbaya, kiatu chake sawa".

Wmagharibi hamuwataki kwa sababu ya ushoga, lakini vitu vyao hamuishi kutuagizia tukirudi nyumbani.
 
Mkuu umeangalia hii issue kwa busara fulani na ingawa tunaweza kutokubaliana kwa minajili ya issue yenyewe, naweza kuelewa kwa nini hatukubaliani kwa namna ile ile ulivyochambua sababu za kutokubaliana kwetu.

Kuna divide kati ya watu wa nyumbani na watu wa diaspora. Or to be precise, watu walio capture the zeitgeist na wale ambao wanaishi in the past.

Kikwete said it best, at the current rate, this is a matter of time, haya mambo yatakubalika halafu mtaona the sun still rises in the east, that it was much ado about nothing.

Watu wa diaspora, mimi kwa mfano, washaona kwamba hata kama mtu personally hufagilii mambo ya same sex relationship, kuwapa hawa watu haki zao si mwisho wa dunia.

Hapo bongo mbona tushakuwa na gay people waliopewa presidential appointments (waliokuwa presidential appointees)? Ina maana marais wetu hawakujua kwamba hawa watu ni gay?

Unaposema huku nyumbani kuna mambo yanayotuumiza kichwa kuliko issue za ushoga nakubaliana na wewe kabisa. Hapo ndipo unagusia mzizi wa beef yangu na watu kama kina Mugabe.

Mugabe kashindwa ku address issues za muhimu za kiuchumi za Zimbabwe. Zimbabwe kuna noti ipo kwenye common circulation ya Z$100,000,000,000,000. Watu wangapi wanajua kuisoma hiyo namba?

Tatizo unalolisema na mimi naliona hilo hilo. Katika nchi zetu masikini zenye matatizo hayo uliyoyataja yote, kwa nini viongozi wetu wachukue muda wao mwingi na energy kubwa sana kupinga ushoga?

Ukichunguza sana utaona ni kwa sababu wameshindwa kutatua matatizo ya kweli ya watu, sasa wanataka kutengeneza matatizo artificial ambayo ni rahisi ku rally waafrika ambao hawana elimu wala exposure.

Ukisema unaomba utamaduni ubakie huku huku, inabidi ufanye kazi kutetea utamaduni wako sio useme tu. Waafrika tumekuwa rahisi kusema lakini wavivu kufanya.

Ukitaka utamaduni wa magharibi ubaki huku huku, piga marufuku mitumba, endeleza viwanda vya nguo vya Afrika ili msivae nguo zilizokuwa designed na gay people (top designers Marekani na Ulaya ni gay people).

Pia pigeni marufuku filamu za Ulaya na Marekani, kwa sababu top producers, directors, actors financiers etc wamo hao hao gays, tena ukichunguza kwenye movies na series/ muziki siku hizi gay rights themes ziko prominent sana. Kuna mtu kachukua award ya hip hop mwaka huu kwa wimbo unaotetea gay rights. Gay rights zimefika mpaka kwenye hip hop siku hizi, hip hop is one of the most homophobic genre.

Kwa hiyo fungeni mipaka na dunia ya magharibi, anzisheni internet yenu, movies zenu, muziki wenu etc.

Otherwise mtakuwa mnafanya mchezo wa unafiki wa "Baniani mbaya, kiatu chake sawa".

Wmagharibi hamuwataki kwa sababu ya ushoga, lakini vitu vyao hamuishi kutuagizia tukirudi nyumbani.

Kiranga ndugu yangu, hatuwezi kujifungia milango tukatae 'kuazima' ambayo yanaweza kuwa 'mema' yanayofanywa na hao mashoga. Binafsi, much as nachukia biashara nzima ya ushoga, lakini sioni ubaya wa kununua nguo aliyotengeneza shoga. Na kwa kununua nguo hiyo, sina maana na-support matendo yake (as per wewe hapa ndio baniani mbaya anahusika naona). Na haina maana katika 'kuazima' utamaduni wao basi na tukumbatie yote whether mazuri au mabaya...na tuachiwe tuchague yale tunayoyatamani na tusiyoyateka tuendelee kusema NO.

Tukirudi kwa akina mzee Mugabe, unaweza kuwa kweli ulivyom-define alivyodandia hoja kwa manufaa yake, lakini huo ndio msimamo wake kwenye issue ya ushoga. Just because uchumi wake umesimamia 'neutral' kilimani, haina maana kuwa hana msimamo wake kwenye issues nyingine, na huu ndio msimamo wake kwenye issue ya ushoga.

...Tena ukirudi usisahau zile top za designer 'naniliu', size ni 12 UK...haa haaa....
 
Just that, what do you have to say?

Hujajibu swali.


Sikulielewa swali lako mkuu. 1)Unaposema jamii yao una maanisha mashoga ni "jamii" ya watu kwa kigezo kipi?
2)Kwanini unasema tunalazimisha jamii fulani kuwa kama nyingine?
 
Kiranga ndugu yangu, hatuwezi kujifungia milango tukatae 'kuazima' ambayo yanaweza kuwa 'mema' yanayofanywa na hao mashoga. Binafsi, much as nachukia biashara nzima ya ushoga, lakini sioni ubaya wa kununua nguo aliyotengeneza shoga. Na kwa kununua nguo hiyo, sina maana na-support matendo yake (as per wewe hapa ndio baniani mbaya anahusika naona). Na haina maana katika 'kuazima' utamaduni wao basi na tukumbatie yote whether mazuri au mabaya...na tuachiwe tuchague yale tunayoyatamani na tusiyoyateka tuendelee kusema NO.

Tukirudi kwa akina mzee Mugabe, unaweza kuwa kweli ulivyom-define alivyodandia hoja kwa manufaa yake, lakini huo ndio msimamo wake kwenye issue ya ushoga. Just because uchumi wake umesimamia 'neutral' kilimani, haina maana kuwa hana msimamo wake kwenye issues nyingine, na huu ndio msimamo wake kwenye issue ya ushoga.

...Tena ukirudi usisahau zile top za designer 'naniliu', size ni 12 UK...haa haaa....

Ukishakubali kutumia vilivyotengenezwa na mashoga basi it is just a matter of time kukubali kuwapa haki zao mashoga kama alivyosema Kikwete.

Watakuandikia habari zao kwenye vitabu, watakuwekea mambo yao kwenye filamu, watakuimbia habari zao kwenye muziki, watakupa fasheni zao kwenye nguo, itakuwa a matter of time tu kabla hujakubali. Kama si wewe mwanao.


Ndiyo maana Kikwete kwa kujua hili, in not so many words kasema kwamba sie tusiotengeneza hata pini na tunaoishi kwa mitumba, hatuwezi kukataa haya mambo. Ila hatuwezi kukubali kwa haraka wanayotaka wamagharibi. Ni mambo yatakayokuja polepole na muda.

Halafu watu wataona kumbe si jambo kubwa kama ilivyodhaniwa, kwa maana ya kwamba kuna namna ha kuwapa hawa mashoga haki zao na bila kuingilia uhuru wa wasio mashoga, if at all tunaweza kuishi kama watu tuliostaarabika.

Ushoga umekuwapo tangu kabla ya utawala wa Warumi, Wayunani na Wamisri.

Mnataka kuumaliza kwa sheria leo?
 
Sikulielewa swali lako mkuu. 1)Unaposema jamii yao una maanisha mashoga ni "jamii" ya watu kwa kigezo kipi?
2)Kwanini unasema tunalazimisha jamii fulani kuwa kama nyingine?

1. Mashoga ni jamii ya watu wanaopenda ushoga.

2.Mnalazimisha jamii fulani kuwa kama nyingine kwa sababu mnalazimisha wanaopenda ushoga kuishi kama wasiopenda ushoga.

Je, kwa msingi huo huo wa kulazimishana, wanaopenda ushoga wakiwalazimisha nyie msiopenda ushoga mpende ushoga mtajisikiaje?

Unaona habari ya "Mkuki mtamu kwa nguruwe, kwa binadamu mchungu" hapo?
 
1. Mashoga ni jamii ya watu wanaopenda ushoga.

2.Mnalazimisha jamii fulani kuwa kama nyingine kwa sababu mnalazimisha wanaopenda ushoga kuishi kama wasiopenda ushoga.

Je, kwa msingi huo huo wa kulazimishana, wanaopenda ushoga wakiwalazimisha nyie msiopenda ushoga mpende ushoga mtajisikiaje?

Unaona habari ya "Mkuki mtamu kwa nguruwe, kwa binadamu mchungu" hapo?


Samahani sana mkuu, let's go back to the basics. 1)"jamii" maana yake nini?
2)ushoga ni disorder. Ila wao wanataka ugonjwa wao uwe life style. That's b.u.l.l sh*t.
 
Samahani sana mkuu, let's go back to the basics. 1)"jamii" maana yake nini?
2)ushoga ni disorder. Ila wao wanataka ugonjwa wao uwe life style. That's b.u.l.l sh*t.

Jamii ni watu wenye ujamaa kwa namna fulani, jamii ya mashoga ina ujamaa kwa ushoga.

Ushoga ukiwa ni disorder au si disorder si muhimu, kitu muhimu ni kwamba usimnyime mtu haki ya kufanya anachotaka.

Halafu, kama ushoga ni disorder, hilo litakufanya uwe muonevu zaidi kuwanyima watu wenye disorder haki zao.

Utakuwa kama unataka kumnyima mlemavu haki ya kuwa na wheelchair, unamlazimisha atembee bila wheelchair kama wasio ulemavu!
 
Ukishakubali kutumia vilivyotengenezwa na mashoga basi it is just a matter of time kukubali kuwapa haki zao mashoga kama alivyosema Kikwete.

Watakuandikia habari zao kwenye vitabu, watakuwekea mambo yao kwenye filamu, watakuimbia habari zao kwenye muziki, watakupa fasheni zao kwenye nguo, itakuwa a matter of time tu kabla hujakubali. Kama si wewe mwanao.


Ndiyo maana Kikwete kwa kujua hili, in not so many words kasema kwamba sie tusiotengeneza hata pini na tunaoishi kwa mitumba, hatuwezi kukataa haya mambo. Ila hatuwezi kukubali kwa haraka wanayotaka wamagharibi. Ni mambo yatakayokuja polepole na muda.

Halafu watu wataona kumbe si jambo kubwa kama ilivyodhaniwa, kwa maana ya kwamba kuna namna ha kuwapa hawa mashoga haki zao na bila kuingilia uhuru wa wasio mashoga, if at all tunaweza kuishi kama watu tuliostaarabika.

Ushoga umekuwapo tangu kabla ya utawala wa Warumi, Wayunani na Wamisri.

Mnataka kuumaliza kwa sheria leo?

Sawa ulikuwepo toka enzi na enzi, kwa nini leo ndio uwe issue ya kutulaza macho?....Tukirudi kwenye vijiji vya nyumbani, hawa mashoga wapo ila hawaonekani? Kwa nini rate kubwa imejaa mijini kama sio issue za kuiga tu? (majority)...Kama ni za kuiga, basi na tuzipige vita kwa nguvu zote......

Kikwete ameshikwa kigugumizi kwa 'kuogopa' kuudhi wakubwa..huu ni mtazamo wangu...Kama tukiamua kusema NO basi itakuwa NO kweli....Ni mara ngapi tumeshuhudia watu wakipandwa na mahasira kisa imani yake imesemwa vibaya, then kwa nini tusiseme NO kwenye issue hii...Kwa hiyo hata wakituletea mambo yao kwenye vitu tunavyotaka, tunaweza kusema hapana....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom