Wewe hujaelewa na si ajabu hujui tofauti ya kumpa mtu hela kama msaada na kumkopesha.
Hapa nazungumzia mikopo. Siyo misaada. Unajua maana ya 'kukopa'?
Unapompa mtu hela kama msaada hutomdai tena. Msaada haudaiwi.
Ila mtu anapokuja mwenyewe kukukopa [anakuambia naomba unikopeshe] hela kwa ahadi ya kukurudishia baada ya muda fulani, muda ukifika anapaswa na anawajibika kukurudishia ulichomkopa.
Masharti yapo kwenye mkopo. Hayapo kwenye msaada.
Hata benki au sehemu zingine zinazotoa mikopo zina masharti ya mikopo.
Kusoma na kuelewa ni janga kitaifa!!!