Umekopa mwenyewe, nikikudai unakasirika!

Umekopa mwenyewe, nikikudai unakasirika!

Umenikumbusha watu watatu nawadai naona hamna dalili za marejesho


Usiombe kukopesha mwanamke
 
Nilipe nisepee, nilipe nisepee, nilipe nisepee nilipeee..

Uliniaidi baada ya week 2, sasa imepita miez mitano, pesa zangu ni zaid ya laki 2, hujanirejesha hata cent 5...
I miss this song,
# belle 9.
# nilipe nisepe.
Hahaa mpk afe mtu..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nahisi kama roho ya kukopesha ilisha nitoka. maana saa hizi hata wedeni wangu wengine nimesha wasahau wengine.
[TAG]Nyani Ngabu[/TAG]huu uzi wako umekuja kunitonwesha vidonda aisee
 
Mimi kwa kawaida huwa si mchoyo kabisa.

Pia ni mtu mwenye huruma sana. Kwa mfano huwa nikiona ombaomba [silipendi hili neno sema basi tu sina neno jingine lililo zuri] barabarani huwa ninapatwa na simanzi kubwa sana.

Hususan kama ombaomba huyo ni mtoto au ni watoto. Kama nina hela mfukoni huwa nawapa tu bila hata ya kujiuliza mara mbili.

Kwa hiyo mtu akinijia na shida yake aombe nimkopeshe hela mara nyingi sana huwa sikatai.

Lakini kwa vile huwa ni mkopo basi huwa ninatoa masharti yangu. Huyo mtu akiyakidhi na kama hicho kiasi ninacho basi namkopesha.

Sasa inapotokea mtu anakuja kukukopa na kukuahidi kuwa atakulipa siku fulani, yaani anakubembeleza kweli hadi anataka kulia, na wewe kwa huruma zako unamkopa kwa masharti.

Siku ya kurudisha mkopo ikifika yeye hatokei. Ukianza kumtafuta ili akulipe anaanza kukukwepa.

Ukizidisha kumtafuta anaanza kukasirika na kukuletea jeuri.

Watu wa hivi siwapendi kabisa mimi. Kwa nini unikasirikie wakati nakudai hela zangu?

Kama hutaki nikufuatilie nilipe hela zangu na mimi wala sitakutafuta hata kwa salamu tu.

Umejileta mwenyewe na vishida vyako na kuanza kujiliza halafu unaniletejea jeuri kunilipa hela zangu.

Mijitu mingine sijui ikoje tu. Kama unadai hela uliyokopa ni ndogo nisikusumbue iweje hukuwa nayo sasa?

Shenzi pambaaf kabisa. Siku ingine ukinijia na vishida vyako ntakwambia nenda baa ukategeshe.
hii thread imfikie yule jamaa yangu ninayemdai.

Tuipende nchi yetu Tanzania.
 
Akija kukopa anakuwa mpole, akidaiwa anakuwa mkali,

'Dawa ya Deni kulipa" wahenga
 
Mtu mwenye huruma na unapenda kusaidia, halafu watu wanakuomba misaada mpaka wanataka kulia na unawapa masharti juu...hmm! Okay.
 
Mbaya zaidi wakati wa kumdai unalazimika kujieleza kwake tena. Na yeye bila haya anakuhoji na kukuonesha altenatives za kutatua shida yako ilihali halipi deni.

Kuna Mdai wangu aliwahi kuniambia kuwa niombee Mungu anifungulie milango ili nikulipe hela yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu mwenye huruma na unapenda kusaidia, halafu watu wanakuomba misaada mpaka wanataka kulia na unawapa masharti juu...hmm! Okay.

Wewe hujaelewa na si ajabu hujui tofauti ya kumpa mtu hela kama msaada na kumkopesha.

Hapa nazungumzia mikopo. Siyo misaada. Unajua maana ya 'kukopa'?

Unapompa mtu hela kama msaada hutomdai tena. Msaada haudaiwi.

Ila mtu anapokuja mwenyewe kukukopa [anakuambia naomba unikopeshe] hela kwa ahadi ya kukurudishia baada ya muda fulani, muda ukifika anapaswa na anawajibika kukurudishia ulichomkopa.

Masharti yapo kwenye mkopo. Hayapo kwenye msaada.

Hata benki au sehemu zingine zinazotoa mikopo zina masharti ya mikopo.

Kusoma na kuelewa ni janga kitaifa!!!
 
Yaani mkuu umehit palepale! Tena mwingine hapokei hata simu ukimpigia

Kama kuna mdada hapa kazini nimemkopesha magauni mawili mpaka leo kimyaa hata kusema nivumilie (dharau kwenye biashara ya mtu)

Kazi yenyewe ndo kwanza nimeanza hata kumdai naogopa nisijeonekana nina gubu!

Wanarudisha kweli nyuma maendeleo ya watu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ulimkopesha Manzi sahau kupata hela yako labda uombe nyapu

great thinker
 
Yaani mkuu umehit palepale! Tena mwingine hapokei hata simu ukimpigia

Kama kuna mdada hapa kazini nimemkopesha magauni mawili mpaka leo kimyaa hata kusema nivumilie (dharau kwenye biashara ya mtu)

Kazi yenyewe ndo kwanza nimeanza hata kumdai naogopa nisijeonekana nina gubu!

Wanarudisha kweli nyuma maendeleo ya watu!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Unajua ni bora mtu akujie na akuombe tu umpe.

Lakini siyo unakuja na gia ya kukopa halafu unaahidi utaulipa huo mkopo baada ya muda fulani.

Muda ukifika unaanza kumzungusha aliyekukopa.

Inakera.
 
Back
Top Bottom