Tip Master
JF-Expert Member
- Oct 17, 2011
- 510
- 573
- Thread starter
- #101
Hebu achaneni na mambo ya sumatra, chart, mimi niliendesha gari yangu kutoka Dar,tabata segerea mpaka Mwanza mjini Kirumba mwezi march kwa uhalisia kuna KILOMETA 1080.
Nilitoka dar saa kumi kamili alfajiri nikiendesha toyota primeo 1800cc.nikafika mwanza saa mbili usiku mwendo wa kawaida nilikuwa na familia.
ZINGATIA.
1.Hakikisha unatok dar mapema(at least 1hr before 0600am) ili usifatane na mabasi makubwa kwani ni masumbufu na yanaovertake ovyoovyo yanaweza kukuletea matatizo.
2.Barabara ya Shinyanga - Mwanza ina matuta mengi yale mabaya ya kukomoa madereva, kwa gari ndogo lazima upande kwa spidi Zero. Pana kilometa 168, lakini utatumia masaa matatu.
sent from my rollpad.
hakika wewe ndio naweza kuchukua uzoefu kwako,bro ulitumia lita ngapi mpaka kirumba