Uliza chochote kuhusu Rwanda

Lakiini naamini, ukijifunza kutengeneza na ukawa na mtaji wako, Tanzania ngombe wapo wa uhakika.
Hasa ukizingatia nyie huko, mnao ngombe wanaokula majani ya asili,
Ujirani mwema sio kutumiana majeshi tu, ila ilitakiwa Rwanda itume wataalamu wa kutengeneza Ikivuguto huku Tanzania kwenye hizi jamii za Wafugaji kama Wasukuma Wanyaturu nk. Ili Watu wajipatie kipato na pia Wananchi tuburudike na Ikivuguto.

Maziwa yetu utakuta yamejazwa maji hadi ile ladha ya Maziwa inapotea kabisa.
 
Hii Certificate of import Unapata kwa kupeleka samples Au ni taratibu gani Unafanya,Au mpaka mzigo ukiwa boda
Mzigo ukiwa border, washikaji wanafanya kila kitu. Kikubwa tu uhakikishe mali yako ni safi na salama kwa kuliwa na binadamu.
Nadhani ukiwa na nia, unaweza tembelea mpaka wa Rusumo, na maeneo jirani kwa uhakika zaidi. Hata ukiwa na stock yako karibu, wanaweza kununua huko.
 
Rwanda haina jukumu hilo mkuu.

Tanzania yenyewe au wafanyabiashara wa kitanzania, wakiiona Rwanda kama jirani, wanaweza kushea mengin, na hilo likiwemo.
Hao wataaramu wapo,viongozi wakiongea wanaweza.

Na isitoshe, Rwanda kwa sasa ina kiwanda cha kutengeneza maziwa ya unga. na hakika Haijitoshelezi. Hivyo, kwa ujilani mwema,Watanzania wana soko la uhakika la maziwa, viongozi pande zote wakiafikiana.
 
jibu no.2 nitakupinga kidogo, uzoefu wa vita wa jwtz ni mkubwa kuliko hata wa rwanda, nisiingie sana ndani ila ukweli huo unaujua ww mwenyew..hilo jeshi la rwanda limepigana vita gani zaidi ya hayo makundi ya uasi?? toa mfano jeshi la rwanda limeshinda vita gani
 
Vipi swala la rushwa (ufisadi ) limekaaje uko ni kama Tz
Rushwa popote ipo, asikudanganye mtu. Kilichopo au tofauti kubwa, ni kwamba wanyarwanda wengi wameelimika, wanajua haki zao. Na kila kiongozi, ana mkubwa wake. Kwa hiyo, kuna wengine ukiombwa rushwa, ukipeleka malalamiko, haki yako utapata.

Ngazi za uongozi zimejengeka kiasi kwamba mambo ya usiri ni kidogo sana.
Na kwa sasa, kuna mfumo wa huduma zote za kiserikali, umerahisisha sana mambo ya huduma, hivyo rushwa huku ni kidogo sana ukilinganisha na TZ.
tembelea irembo.gov.rw lugha weka kiingeleza, angalia mfano wa huduma zitolewazo. Na hapo, unaomba online, unapata online. Rushwa hapa itatoka wapi.
 
Kuna dhana niliiskia Watanzania walisema kwamba ukiona Mnyarwanda, lazima atarudi kwao kupata mimba ya Mnyarwanda mwenzie, je kuna ukweli hapo?
Halipo hivo. Wanyarwanda ni wastaarabu sana. Hata kama ni kahaba, huenda akawa anafanya kutokana na maisha magumu. Mpaka ageuke, ujue umeshindikana.
 
Mi ni raia wa kawaida mkuu. Nimeongea kama mimi, na ni maoni yangu wala siyo uhalisia. Kwa hiyo, ntaishia hapo
 
Mi ni raia wa kawaida mkuu. Nimeongea kama mimi, na ni maoni yangu wala siyo uhalisia. Kwa hiyo, ntaishia hapo
sawa tuendelee...

3. ni kitu gani hasa wanyarwanda wanakupenda kutoka tz?? mfano sisi tunapenda wanawake wa kirwanda..

4.ww binafsi ukiambiwa uchague pa kwenda kuishi kati ya nchi za maziwa makuu utaichagua ipi na kwa nn??
 
Wewe kwenu ni Rwanda, sio Tanzania.
 
safi ila mauaji ya 1994 wahutu ndio waliuliwa wengi ndio maana walishindwa vita pia mauaji walianzisha watutsi kwa kuuua marais wahutu mara kadhaaa na waliporudia mwaka 1994 wahutu waliona enough is enough , wakaamua kulianzisha
 
sawa tuendelee...

3. ni kitu gani hasa wanyarwanda wanakupenda kutoka tz?? mfano sisi tunapenda wanawake wa kirwanda..

4.ww binafsi ukiambiwa uchague pa kwenda kuishi kati ya nchi za maziwa makuu utaichagua ipi na kwa nn??
3. Ukiachana na watu wenye akili finyu, ambao ni wachache, watanzania ni wakalimu, mnapendwa kwanza kwa hilo.
-Samaki wa ziwa Victoria, ni Fahari yenu
-Tikiti maji, ndo usiseme
-Kwa misambwanda, na mi Tanzania naipa maua yake πŸ˜‰ πŸ˜‰ πŸ˜‰ πŸ˜‰
-Mchele unaonukia vizuri,


4. Binafsi, ukiachana na nchi yangu, ntachagua Tanzania.
- Kwa sababu ya hali ya hewa, kwa sababu ya ukalimu wa watanzania. Japo vijana wengi wenu matapeli tu, hawaaminiki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…