Ulinzi wa Rais Samia alipotua Dar leo

Ulinzi wa Rais Samia alipotua Dar leo

Wajameni kama wameletwa na bosi wao jana hiyo hiyo mama awafurushe?

Ukweli mchungu mama anakubalika sana. Kama ni kujilinda zaidi ni dhidi ya wale ambao bado hawataki kuamini hii ni awamu ya sita.

Hiiiiii bagosha!
Ukiondoa hao, mama anaweza kutembea kwa mguu kutoka Posta mpaka kibaha bila ulinzi wowote na asidhurike. Sanasana vijana watakuwa pembeni yake kumsindikiza kwa furaha.
 
Ukiondoa hao, mama anaweza kutembea kwa mguu kutoka Posta mpaka kibaha bila ulinzi wowote na asidhurike. Sanasana vijana watakuwa pembeni yake kumsindikiza kwa furaha.

Tunaomwunga mkono mama tuko wengi sana kuliko hao walioshupaza shingo wakiota ndoto za awamu ya tano.

Mama na aendelee kutupa raha kwa kutuondoshea wasaka fursa wote wa awamu ya tano wanaotaka kuendelea kusaka fursa kwenye awamu ya sita pia.
 
Hivi una akili timamu wewe? Unafanana na yale matoto majingajinga yanayolia hovyo hovyo hata kuku akidonoa chakula chake!
Haha ngosha jamaa amekuchoma sana mpaka unamfananisha na matoto ya kisukuma yanayolialia hivyo
 
Sidhani Kama umeelewa uzi! Ipo hivi Kuna watu humu walikuwa wakiusema vibaya ulinzi wa hayati haswa hao jamaa wenye mitutu!,alipoingia rais Samia kwa Mara ya kwanza alikuwa akionekana na ulinzi wa kawaida I mean hao ambao hawana mitutu.. wakaanza kusifu na kumsema vibaya hayati na Kama ulifatilia hata jana ktk hotuba ya mbowe aliligusia swala hili la hayati kuwa na ulinzi ule!

Sasa mama pia ambae alikuwa anaonekana anaulinzi smart Sasa nae anaowalinzi walewale wenye mitutu! Sasa napo waseme.. watu hawataki kukubaliana na mabadiliko haya ya safu ya ulinzi wa rais ilifika kipindi wakaanza kuzusha kuwa ni wakutoka nchi za nje!!!
Watanzania tunamtindo wa kuzusha mambo hata Kama hatuna hakika.

Binafsi sikuwahi kuwa na shaka na ulinzi huu isipokuwa nilichokuwa najua ni kwamba ulinzi wa rais unaprotokali zake inapobidi kuwepo hao jamaa basi watakuwepo na pale ambapo haibidi basi hawata kuwepo.

Hivyo Basi kwakuwa mama pia ameonekana kuwa na ulinzi huo sasa tufunge mjadala na kukubaliana na mabadiliko haya ya ulinzi wa rais maana wao mpk kufanya hivyo ndio wanaojua hali yao ya kwanini wafanye hivyo na sio sisi waonaji tu.
Magufuli afwile go
 
Mbowe jana nae kalizungumza ilo kwa upande wa Hayati naye anaamini eti ao ni wanajeshi wa nchi nyingine...
Mbowe yupi ? Yule aliyebadili gia angani ? Bado mnamsikiliza tu ? Kweli mmekosa kazi.
 
Jiwe alisemwa sana juu ya wale walinzi wake wenye mitutu huku wakisema mama hana ulinzi wa namna hiyo!

Ktk moja ya uzi humu nilikomenti ya kuwa waache fikra hizo hii inamaana ulinzi wa rais umebadilika lkn watanzania wengi bado hawajabadilika kukubaliana na hilo!

Wanataka marais waliopita na wasasa wawe na ulinzi uleule kitu ambacho ni very lisk maana hata adui kila siku nae huwa anabadilika!.

Mama akiwa anarejea kutoka Uganda walinzi wa aina ileile waliokuwa wakisemwa vibaya wakati wa hayati wameonekana wakiwa na mama pia video hii hapa.


Haya wale wasemaji waliokuwa wakinena mara hivi mara vile nafikiri ni muda wa kulifunga hili na kufanya vyengine.

Mbona hao ni FFU? Wale wa MEKO si walikuwa Makhirkhiri wa Rwanda?
 
Mbona hao ni FFU? Wale wa MEKO si walikuwa Makhirkhiri wa Rwanda?
Hata kuangalia napo tufundishane mkuu hebu angalia vizuri video ffu wapo lkn na hao jamaa wapo wanaanza kuonekana rais akiwa kwenye red carpet weka jicho lako makini hasa pembezoni huko ndo utawaona.
 
Kwani kuna mtu anawaza Rais alindwe na marungu na mapanga? au kombeo?
 
Viongozi asilimia kubwa duniani wanalindwa na walinzi wenye silaha

Ova
 
Mengi yalizungumzwa kuhusu ulinzi wa Rais Magufuli. Wengi wakakosoa kwamba analindwa na maaskari wanaovaa magwanda ya kijeshi jeshi huku wameshikilia mabunduki makubwa.

Ni viongozi wengi tu duniani hulindwa hivyo. Hata Rais wa Marekani hulindwa na wanausalama wenye mabunduki makubwa na wanaovaa magwanda ya kijeshi jeshi.

Hao huitwa Counter Assault Team. Hao ndo wapiganaji ikitokea Rais anashambuliwa kwa silaha. Wale wanaovaa suti kazi yao si kupigana na adui. Kazi yao ni kuhakikisha rais yuko salama kwa kumkinga [taking the bullet for the president] au kumuondosha kwenye eneo lenye hatari.

Leo Rais Samia katua kwenye uwanja wa ndege Dar.

Chini naweka video. Lakini kabla yake, naweka screenshots za video zinazoonyesha hao watu wa counter assault walikuwepo na mabunduki yao.

Kuna watu walishaanza kusema eti Rais Samia hana walinzi kama hao kama ilivyokuwa kwa Magufuli.

Pia, Rais huwa hajipangii ulinzi wale mwenyewe. Ulinzi wake hupangwa na wataalamu kulingana na vigezo vingi ikiwemo eneo alipo, hali ya usalama wa eneo kwa ujumla, na mambo mengineyo.

Ona huyu na huo mbunduki wake:
View attachment 1742313

View attachment 1742314

Huyu pia ni mwingine akiwa pembezoni kidogo.
View attachment 1742316

Video hii hapa;

Kwa haraka haraka wanaonekana around 7. Anyways, ulinzi mkali kwa rais ni kawaida hao wanaoshangaa ni kwa ajili ya propaganda zao tu!
 
Gharama zote na matumizi ya ndege kubwa.Angekuwa Magufuli angetumia usafiri wa barabara na angesimama baadhi ya maeneo kukagua miradi ya maendeleo na kuongea na wananchi.Tutamkumbuka sana JPM.Aendelee kupumzika kwa amani
Hapo na bado tutamkumbuka sana tu huyu mwamba
 
Wabeba mabegi hawapo kwa mama, zile helicopter juu hazipo mbona? Tena moja ya polisi nyingine ya jeshi
 
Back
Top Bottom