Ulinzi wa Rais Samia alipotua Dar leo

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,232
113,610
Mengi yalizungumzwa kuhusu ulinzi wa Rais Magufuli. Wengi wakakosoa kwamba analindwa na maaskari wanaovaa magwanda ya kijeshi jeshi huku wameshikilia mabunduki makubwa.

Ni viongozi wengi tu duniani hulindwa hivyo. Hata Rais wa Marekani hulindwa na wanausalama wenye mabunduki makubwa na wanaovaa magwanda ya kijeshi jeshi.

Hao huitwa Counter Assault Team. Hao ndo wapiganaji ikitokea Rais anashambuliwa kwa silaha. Wale wanaovaa suti kazi yao si kupigana na adui. Kazi yao ni kuhakikisha rais yuko salama kwa kumkinga [taking the bullet for the president] au kumuondosha kwenye eneo lenye hatari.

Leo Rais Samia katua kwenye uwanja wa ndege Dar.

Chini naweka video. Lakini kabla yake, naweka screenshots za video zinazoonyesha hao watu wa counter assault walikuwepo na mabunduki yao.

Kuna watu walishaanza kusema eti Rais Samia hana walinzi kama hao kama ilivyokuwa kwa Magufuli.

Pia, Rais huwa hajipangii ulinzi wale mwenyewe. Ulinzi wake hupangwa na wataalamu kulingana na vigezo vingi ikiwemo eneo alipo, hali ya usalama wa eneo kwa ujumla, na mambo mengineyo.

Ona huyu na huo mbunduki wake:
B8553B89-ED26-4883-B8A1-1961C81C7226.jpeg


E1DDF6B5-8CE8-47D4-9B51-D784FCC692AD.jpeg


Huyu pia ni mwingine akiwa pembezoni kidogo.
4A39F407-3DD8-4512-BD5A-A5AD9A6B0DE6.jpeg


Video hii hapa;

 
Ulinzi wake si jukumu lake kupanga hakuna Rais yeyote anaelindwa na manati hata Papa analindwa na Bunduki itakuwa huyu anaetaka kutuamisha yeye ni bora na simple kuliko aliyepita?

Ogopa sana mtu anayepost kitu kwa kutaka like na postive feedback muogope sana huyo mtu mwenye ufahamu atajua nazungumzia nini
 
Huyo uliyezungumshia ktk picha za screen shots, mimi naona ni kama huyo huyo mtu mmoja ktk position tofauti tofauti...

Anyway it doesn't matter.

And it's normal kwa Rais kulindwa na kuhakikisha usalama wake, though kwa Mwendazake it was too much. Ni kama vile alikuwa haamini ktk Mungu..

Na huyu mama (in my opinion) anapaswa kuongezewa ulinzi zaidi kwa sbb baadhi wahafidhina wa CCM hawataki na hawakutaka ashike madaraka haya baada ya Mwendazake kwenda zake...

So likely, they can do anything to harm Madam President Samia Suluhu Hassan...
 
Huyo uliyenzungumshia ktk screen shots hizo Mimi naona ni huyo huyo mtu mmoja tu ktk position tofauti tofauti...

Anyway. It's normal kwa Rais kulindwa na kuhakikisha usalama wake. Na huyu anapaswa kuongezewa ulinzi zaidi kwa sbb baadhi wahafudhina wa CCM hawataki na hawakutaka ashike madaraka haya baada ya Mwendazake kwenda zake...

So likely, they can do anything to harm Madam President Samia Suluhu Hassan...
Hapana. Kuna mmoja nimeweka screenshots mbili.

Lakini kuna mwingine tofauti na huyo, nimeiweka screeshot yake pia.

Na kuna ingine ya mwingine pia.
 
Hapana. Kuna mmoja nimeweka screenshots mbili.

Lakini kuna mwingine tofauti na huyo, nimeiweka screeshot yake pia.

Na kuna ingine ya mwingine pia.
It's OK, only if those are security procedures & protocols..

Hata hivyo kwa Mwendazake it was too much. Nadhani hofu ya kivuli cha "mabeberu" ilikuwa inamtesa sana hata kujiona hayuko salama muda wote...

I don't know how did they succeed to fix him despite such tense security...
 
Back
Top Bottom