Ulichoma mtaji mara ngapi mpaka kuja kutoboa kibiashara?

Ulichoma mtaji mara ngapi mpaka kuja kutoboa kibiashara?

Nakumbuka kuna center moja nilikamata sehemu. Kila mtu ananiambia daah hapa mwanangu umeula kwa eneo hili utapiga business mpaka uchoke. Weee..! 😀 Mbata! Mbata! Kofi! Teke! Mtamaa..! Kichwa chini miguu juu hata miezi 6 haikuisha dadek😄
😂 hizi biashara zina mambo mengi sana, kuna muda kuwa na mtaji sio suluhisho la kufanikiwa.
 
Nakumbuka kuna center moja nilikamata sehemu. Kila mtu ananiambia daah hapa mwanangu umeula kwa eneo hili utapiga business mpaka uchoke. Weee..! 😀 Mbata! Mbata! Kofi! Teke! Mtamaa..! Kichwa chini miguu juu hata miezi 6 haikuisha dadek😄
😀😀😀😁😁nimecheka kiboya sana
 
Mtu akikuona leo hii unavyokula bata, maisha mazuri, usafiri mkali na biashara kubwa mjini, anaweza kudhani umefika hapo ulipo kirahisi rahisi tuu. Mimi mwenyewe nilikua nadhani hivyo!

Cha ajabu ni kwamba kila ninapojaribu kutia mguu kwenye biashara nachezea za uso mbaya kabisa najikuta natoka kapa. Mpaka muda huu nimeshajaribu zaidi ya aina 5 tofauti za biashara kuanzia bar, stationary, usafirishaji, kilimo, ufugaji nk na zote hakuna hata moja iliyofanikiwa walau hata kurudisha mtaji!

Nimebaki najiuliza nyie wenzetu mliofanikiwa kutoboa kibiashara je na nyie mwanzo mlichoma mitaji kama sisi? Hebu tupeni akili na sisi tutoboe.

NB: Usije na hoja za "fanya kazi kwa bidii".
Tatizo haukushirikisha wazee wa kimila kwenye biashara machuma ulete niyakufikia, kuna kutupiana majini mazongo na kuna kutupiana mikosi salala, unafungua duka unaona wenzio wanasonga wewe hamna, wateja wanakupita wengine unawafuata kwa nguvu hamna hawaji kwako

Nenda stand saa kumi usiku stand nzima inanuka udi
 
Acha kabisa mkuu. Nimechoma milioni 80 kwenye dhahabu. Imeniacha mbendembende. Daah...! Bahati mbaya napoteza hela na umri ndio umeenda 40+.

Nimegundua ndio maana wakinga wakishika biashara moja ya duka ni hiyo hiyo hawabadiriki.

Hivi najitafuta kwa upya. Duka nililipukutisha kuingiza kwenye dhahabu. Hivi ndio napambania kulirudishia. Bidhaa sina japo biashara ipo. Hapa ili nirudi sawa natakiwa angalau milioni 40 kwa uchache 20 mpya niitupie humo.

Ila unajua nini? Lazima niyarudie madini yanipe hela.
Mkuu bado hujachelewa 40+kijana Bado na una afya halafu pia ni mpambanaji Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi ufanikiwe Sana na kwenye madini Rudi unayadai Sana na utafanikiwa.
 
Nimeshuhudia biashara ya mtu mmoja mlokole inafanikiwa sana, sema yule mtu anatoa zaka, alafu kwenye maombi usiseme alafu anaishi maisha matakatifu sana.

Aisee umwambie mtu aache uzinzi, anaona Bora aende upande wa pili.
Siri yake hapo ni kutoa Zaka/sadaka.

Imeandikwa *mjaribuni kwa matendo yaliyo Mema"

Usione tabu kutoa fungu la kumi (10%) kwa unachoingiza

Umepata faida 100k siku ya Leo toa 10k wape watoto wa mtaani wapate Chakula, WAzee walemavu, na wenye shida

Mi huwa sipeleki Hela kanisa Hawa watu ndio Naona baraka zinakuja Moja kwa moja.

Na nishafanya sana hii kitu na nikaja pata Hela ndefu somewhere. Sometimes huwa hata nasahau niliowasaidia.

Mtu anakuja unamuona kabisa ana shida ila unamkaushia sio vizuri unazikosa baraka zako.
 
Nilichojifunza,
Ili utoke kwa haraka lazima uwe na mentor au mtu mzoefu ambaye atakuwa tayari kukuonyesha njia na kukupa siri za game. Asiye na wivu.

Ila kama unataka ukomae mwenye uwe mvumilivu sana.
Mimi niliwahi kupuuza ushauri wa mentor. Nikajikuta natumia 700K nikaambulia 120K. Kosa ni dogo tu la kuleta ujuaji kwa kupuuzia ushauri wa Mentor. Nilikuwa nalima. Ila hilo zao formula yake nilipuuzia kakitu kadogo sana. Ula yeye alifanya akatumia 400K akapata 2M.
Mlilima kitu gani boss
 
Biashara ni ngumu sana binafsi naona mtu ni bora uajiriwe tu, watu ni wachawi sana hawataki upige hatua hii ni hadi kwenye kilimo wakiona shamba lako limestawi vizuri unapigwa kombora hatari.

Kuamini ushirikina ni ujinga.
 
Acha kabisa mkuu. Nimechoma milioni 80 kwenye dhahabu. Imeniacha mbendembende. Daah...! Bahati mbaya napoteza hela na umri ndio umeenda 40+.

Nimegundua ndio maana wakinga wakishika biashara moja ya duka ni hiyo hiyo hawabadiriki.

Hivi najitafuta kwa upya. Duka nililipukutisha kuingiza kwenye dhahabu. Hivi ndio napambania kulirudishia. Bidhaa sina japo biashara ipo. Hapa ili nirudi sawa natakiwa angalau milioni 40 kwa uchache 20 mpya niitupie humo.

Ila unajua nini? Lazima niyarudie madini yanipe hela.

Pole sana. Kwenye dhahabu ulikua upande gani mchimbaji, broker/dealer, muuza madawa/vifaa au?

I know a thing or two naweza shauri.
 
".....kuanzia bar, stationary, usafirishaji, kilimo, ufugaji nk na zote hakuna hata moja iliyofanikiwa walau hata kurudisha mtaji!..."

Hizo biashara hazilipi kivile hasa kama uliweka watu. I bet stationary ulienda kwa mkumbo baada ya kuangalizia. Inahitaji location sahihi sana, wateja wawepo sio wakupitie au wakufuate. Hiyo sio online business kwamba mtu akiona nguo nzuri ataifuata from Mbezi to Tabata.

Usafirishaji ukute ulinunua bodaboda nyingi kama kichaa wakati wewe sio mkorofi na strict, au ulinunua gari la abiria. Ulisafirisha nini hasa.

Kilimo. Hapa ukute ulilima kilimo cha uti wa mgongo ukapinda mgongo. Kilimo ni biashara, ni hesabu, ni utaalamu. Na hakitaki mtaji mdogo kama ni kibiashara, labda kama unafanya kilimo cha kubeti.

Ufugaji haurudishi hela haraka kama unavyotaka, na hauna hela kubwa kivile kama una mtaji kidogo.

Bar sijui wanaendeshaje naona wanaleta matako makubwa na wanayabadili baada ya muda kidogo.

Hapa nahisi una matatizo makuu mawili. Kuwekeza kwenye biashara common kwa Mtanzania ila hazina return nzuri kwa mtaji mdogo, zile biashara za kupatia hela ya kula. Na kukimbia biashara kabla hujaizoea.

Exactly. Kilimo cha acre 10 sijui 20 sio biashara ni kutafuta hela ya kula tu. Huyu bado hajaanza biashara bado anajitafuta hajui nini anataka kufanya.
 
Kila biashara ina KSF zake boss kama zinapelea kimbia. Kwa sisi tuliopo kwenye biashara miaka mingi nikikaa nawewe wiki tu nishajua biashara gani utatoboa na gani utafeli.

Mfano kuna biashara ambazo pesa kubwa ndio KSF, kuna nyengine connection, kuna nyengine exposure, kuna nyengine bidii, etc etc.

KSF = Key Success Factor
 
Kila biashara ina KSF zake boss kama zinapelea kimbia. Kwa sisi tuliopo kwenye biashara miaka mingi nikikaa nawewe wiki tu nishajua biashara gani utatoboa na gani utafeli.

Mfano kuna biashara ambazo pesa kubwa ndio KSF, kuna nyengine connection, kuna nyengine exposure, kuna nyengine bidii, etc etc.

KSF = Key Success Factor
Tunaomba mifano wa KSF.
 
Back
Top Bottom