Jambo moja kubwa na mhimu sana ambalo hulijui kuhusu bongo, ni kwamba amani na utulivu, uzalendo na maisha yenye unafuu kidogo kwa bongo ndicho kinachowafanya wabongo wengi watamani kufanya kazi ndani ya nchi na hata kubaki nchini kwao.
Tofauti na hizo nchi nyingine unazozifia kama vile Kenya, Nigeria, Ethiopia, na nyinginezo nyingi ambazo zina matatizo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, kiasi cha kwamba watu wengi mara tu baada ya kuhitimu masomo yao hukimbilia nje ya nchi kwa ajili ya kutafuta kazi zenye unafuu. Lakini kwa ninavyoelewa kuna wabongo wengi sana wazuri sana academically na wenye uwezo mkubwa sana, waliogundua vitu vingi na vikubwa mno.
Tunazo Mbilinyi's principles of Economy ambazo ziligunduliwa na Professor mbilinyi, tuna Mpemba Effect ya kwenye Physics ambayo hivi sasa inatumiwa viwandani na kwenye sayansi za mambo ya maji, tuna biological research nyingi sana zinafanywa na watu wa botany pale UDSM na SUA zenye results ambazo hazijawahi kuwepo pengine popote duniani. Sasa utaonekana ni kituko unaposema Tanzania watu wamefundishwa kukariri.
Kwa taarifa yako elimu ya Tanzania ni mojawapo ya classic education katika Africa. Na hivi sasa elimu yetu tunaiuza sana tu. Maana katika universities zetu sasa hivi tunapokea wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali duniani yakiwemo; Zambia, Botswana, Zimbabwe, Uganda, Kenya na hata Africa kusini.
Tuna changamoto kubwa tu ya mazingira na hasa accomodation kwa foreign students. Otherwise, naweza kusema we are the best. Suala la watanzania wangapi wapo nje kikazi hicho si kipimo cha uwezo wetu na elimu yetu. Maana uzalendo kwa nchi yetu ndiyo hasa sababu kubwa ya sisi kutokuwa nje ya nchi.