Ukweli mchungu: Wasomi wetu hawauziki…!

Ukweli mchungu: Wasomi wetu hawauziki…!

Sitaki kubishana na wewe kwa sababu nilishatabiri kuhusu kutokea kwa watu kama wewe kwenye aya ya kwanza kwenye hii mada yangu, kwa hiyo wala sijashangaa kwa sababu najua hulka ya baadhi ya wasomi wa TZ, kwamba hawako tayari kubishana kwa hoja, bali kwa kashfa na kejeli, huo ndio usomi wetu.

Hivi unaweza kufananisha wasomi wetu au hata kuwashindanisha na wasomi wa nchi chache tu za hapa Afrika, kwa mfano majirani zetu na baadhi ya nchi za Afrika Magharibi ambao wakati sisi tukiwa tumelala usingizi wa pono wenzetu walichangamkia ajira za mashirika ya umoja wa mataifa na makampuni makubwa huko ughaibuni na kupata exposure kungali mapema.

Sijasema hakuna wasomi Watanzania huko Ughaibuni bali nimesema hatuna wasomi wengi wenye weledi na wanaoweza kuiletea sifa nchi yetu ukilinganisha na wenzetu wa nchi nyingine za Afrika....

Lakini kwa kukosa ufahamu wa kusoma mada na kuelewa umekimbilia takwimu, na hilo tu ndilo baadhi ya wasomi wetu wanalolifahamu hakuna kingine

Pamoja sana dada! Tatizo la wasomi wetu ukitoa mada za kuwapinga wanadhani wewe si msomi na hujui chochote! Na automatically unakuwa adui kwao
Elimu yetu ni ya kukariri sana ,matokeo yake watu wanafaulu kwa maksi za juu lakini maarifa hakuna! .na ndio sababu hatuwezi kushindana na wenzetu kwenye nafasi za kimataifa , wa Tz compitent wapo lakini ni wachache .
Elimu ni maarifa anayobaki nayo mtu baada ya kumaliza shule, wala si kurundika vyeti .na ukilijua tatizo linalokusumbua ujue hauko mbali kupata suluhisho lake ,bahati mbaya wasomi wetu hawataki kujua mapungufu ya elimu yao!
 
Mkuu bado namba yetu ni ndogo kulinganisha na wenzetu huko majuu na vilevile inachangiwa na ubnafsi wetumaana watu waTanzania waliopo nje tena kwenye nafasi nzuri ni wagumu kutoa information au kuwa-connect wenzao.
Ni kweli asilimia kubwa ya binadamu wana roho mbaya sana, anafikiri akimsaidia mwengine akafanikiwa yeye atapunguza kitu. Siwezi kusema ni Watanzania tu wenye tabia hiyo sina uhakika. Lakini wengi hata ninaowajua mimi mfano akiambiwa atafute Mtanzania mwenye uwezo, hata ndugu yake hawezi mpeleka sembuse wewe wa mtaani! Watu wana roho mbaya balaa!!
 
Kusema kwamba wasomi wa Tanzania hawauziki ni upembuzi butu kwasababu hujasema kwa udani wangapi wametamani kwenda huko nje wakakataliwa kwasababu ya kukosa sifa. Ungetoa hata scenario mbili au tatu ili kuijengea ushahidi hoja yako. Hata hivyo naweza kukubaliana na wewe kwa ulanganifu na nchi nyingine kama Nigeria, South Africa etc Tanzania ina wasomi kidogo katika hizo nchi inaweza kuwa na mantiki. Kwa mtazamo wangu kwa msomi mzuri aliye na uwezo mzuri soko la ndani bado lipo, hii inaweza kuwa ni sababu ya kwanini kuna wasomi wachache nje. Lakini pia idadi ya wasomi tunaozalisha kwa mwaka ni wachache, wengi wanamezwa katika soko la ndani. Mfano nchini china mwaka huu wa 2013 wanategemea kutoa wahitimu million 7 (kuanzia bachelor mpaka PhD) katika ya hawa takribani 50,000 ni PhD. Unadhani soko la ndani linatosha kuwaabsorb wote? ni lazima wafluke nje ya nchi yao. Kwa hiyo number ya graduands pia ni sababu ya diaspora.
 
Ukweli utabakia palepale, ingawa kuna mifano michache (ya kutafutatafuta) lakini wenzetu wanatukimbiza jamani! Lazima wa Tz tukaze buti
 
Huh!?!?! Mimi ni mbeba maboksi tu. Kwenye medani za wasomi wa spesho skul sipo kabisa aisee.

Darasa la saba nilifeli, form four nikafeli, form six ndo sikwenda kabisa.

Baada ya kumaliza form four nikaanza kupiga boksi na sasa ninakimbiza mbaya.

I am an uber-proud blue-collar prezdaa wa wabeba maboksi wa kibongo kote ulimwenguni.

Wabeba maboksi oyeeeee......

Nyani Ngabu hebu acha hizo...anyway, first of all nakukubali kwa sababu huna misifa ya kijinga kama wale ndugu zetu wa kuleeeeeeeeee.........uko very humble.
Nyani Ngabu nijuavyo mimi wewe ni MIT graduate, class of 2003 tena ulikuwa Magna Cum Laude!! I know you have a stellar career with hi-tech and resputable firm hapo Greater Boston.
Sasa watanzania wakiambiwa hawauziki sina uhakika na hilo. Ninachojua wakipewa opportunities sahihi huwa wanafunika. Mifano iko mingi huku US. Kuna watanzania nimekutana nao plae Wall Street na wanapiga mzigo hadi Goldman Saachs, Thompson Roeters, Deutsche Bank, etc. ..kuna dada mmoja mtanzania yeye ni head of Hedge Fund pale Wall street anaitwa Ninon Marapichi ni mfano wa kuigwa ana manage portfolio ya around $ 1.5 Billion USD...... na nashangaa kusikia hawauziki. Wakiwezeshwa wanaweza tena na kuwafunika hata hao wanigeria na akina Kibaki
Kitendo cha wewe Nyani Ngabu kupata admission tu hapo MIT nakukubali tosha because hiyo ndio the best and top Engineering program on the planet, anaebisha na abishe!
Go Nyani Ngabu!!
 
Nyani Ngabu hebu acha hizo...anyway, first of all nakukubali kwa sababu huna misifa ya kijinga kama wale ndugu zetu wa kuleeeeeeeeee.........uko very humble.
Nyani Ngabu nijuavyo mimi wewe ni MIT graduate, class of 2003 tena ulikuwa Magna Cum Laude!! I know you have a stellar career with hi-tech and resputable firm hapo Greater Boston.
Sasa watanzania wakiambiwa hawauziki sina uhakika na hilo. Ninachojua wakipewa opportunities sahihi huwa wanafunika. Mifano iko mingi huku US. Kuna watanzania nimekutana nao plae Wall Street na wanapiga mzigo hadi Goldman Saachs, Thompson Roeters, Deutsche Bank, etc. ..kuna dada mmoja mtanzania yeye ni head of Hedge Fund pale Wall street anaitwa Ninon Marapichi ni mfano wa kuigwa ana manage portfolio ya around $ 1.5 Billion USD...... na nashangaa kusikia hawauziki. Wakiwezeshwa wanaweza tena na kuwafunika hata hao wanigeria na akina Kibaki
Kitendo cha wewe Nyani Ngabu kupata admission tu hapo MIT nakukubali tosha because hiyo ndio the best and top Engineering program on the planet, anaebisha na abishe!
Go Nyani Ngabu!!

Hahahahaa haya bana. We nisanifu tu.
 
2286331403

Hapo kwa Donald Trump, his country house.
 
BAK uko sahihi sana mkuu, yaani mimi ninamarafiki ambao wameajiriwa UK, USA, CANADA NA SA ambao kwanza utashangaa mambo wanayoyafanya. yaani mimi nilimshangaa mama mmoja anaitwa Hulda swai yaani ukiona team yako na jins alivyo excell utashangaa. ana run centre yenye watu zaid ya 100 ambao wanafanya kazi chini yake na wote wanaperform vizuri.

Nilisikitika sana alipoambiwa arudi Tz na mkuu wa nchi watu wakamtisha ukirudi Tz utafanyiwa majungu bora uendelee kujilia bata wako huko CSIR.

Ulitaka aje amfanye kama TIDO, acha wale bata huko wakija huku majungu matupu. watabaki kusimulia walikotoka
 
Hizo ni porojo tu, Mwanafunzi wa leo anayemaliza darasa la Saba mwambie ataje tu hata mikoa 5 ya tanzania na nchi walau 10 barani afrika kama atakwambia.
Badala ya kuitanua elimu tunazidi kuishusha na leo watoto wanasoma ramani za kata, wakifika sekondari hakuna mazoezi ya vitendo hata kidogo yanayopelekea watoto kuelewa bali ni ile ya kukariri na kuona majibu yanatoka yaliyoko katika vitabu na ikitokea vinginevyo hakuna anayeweza kuelezea.

Enzi zetu wanafunzi wa darasa la nne wakipata muda katikati ya vipindi lazima kucheza na atlas sana.

Mtu lazima uulizwe kuonesha Kamchatka na Novaya Zemlya ziko wapi, up to this day nakumbuka vimiji vya Siberia huko kwa sababu tulikuwa makini kujifunza. Wenyewe. Outside of homework and teachers assignments.

Ninaposikia wanafunzi waliomaliza darasa la saba hawajui hata mikoa 5 ya Tanzania au nchi kumi za Afrika, natumaini unatania.

Why, by darasa la nne nilikuwa na kijidaftari kilichorekodi karibu nchi zote za Afrika, miji mikuu, marais, idadi ya watu, lugha kuu na hela zinazotumika.

Huku sikosi kusikiza kipindi cha RTD cha Chris Katembo "Mkoa kwa Mkoa" kikinihabarisha kuhusu tamaduni na habari za mikoa yote ya Tanzania, pamoja na kingine kilichozungumzia nchi za Afrika, "Kutoka Afrika" or something like that, Ku supplement kitabu cha "Wafanyakazi wa Afrika" cha darasa la nne, kilichofundisha kuhusu kilimo cha pamba Sudan kwa ramani za kuonesha Wadi zote, mpaka uchimbaji wa dhahabu namakaa ya mawe huko Witwatersrand.

Hivi vipindi, pamoja na vile vilivyokuwa vikitoa madarasa ya shule kwa redio, bado vipo au ni historia sasa?

Mtoto wa darasa la nne leo ukimuuliza Wadi Hadad (aka Wad al Hadad) au Witwatersrand ni nini anaweza kujibu? Labda utamuonea, unaweza kukuta hata mhitimu wa leo wa Chuo Kikuu hajui !

I will spare them Novaya Zemlya and Kamchatka for now. Lest some may not be able to locate Lake Tanganyika on the globe.
 
Mkuu bado namba yetu ni ndogo kulinganisha na wenzetu huko majuu na vilevile inachangiwa na ubnafsi wetumaana watu waTanzania waliopo nje tena kwenye nafasi nzuri ni wagumu kutoa information au kuwa-connect wenzao.

Hichi kitu ulichosema hapa ni ukweli kwa asilimia kubwa sana Mkuu.
 
Enzi zetu wanafunzi wa darasa la nne wakipata muda katikati ya vipindi lazima kucheza na Atlas sana.

Why, by darasa la nne nilikuwa na kijidaftari kilichorekodi karibu nchi zote za Afrika, miji mikuu, marais, idadi ya watu, lugha kuu na hela zinazotumika.

Nakumbuka in the early to mid 80s kulikuwa na bigjii flani hivi zilikuwa zinakuja kwenye paketi zenye vikadi vya bendera za nchi za Afrika na mabara mengine.

Watu tulikuwa tunashindana kuzikariri na kupeana vi pop quiz.
 
Enzi zetu wanafunzi wa darasa la nne wakipata muda katikati ya vipindi lazima kucheza na Atlas sana.

Mtu lazima uulizwe kuonyesha Kamchatka na Novaya Zemlya ziko wapi, up to this day nakumbuka vimiji vya Siberia huko kwa sababu tulikuwa makini kujifunza. Wenyewe. Outside of homework and teachers assignments.

Ninaposikia wanafunzi waliomaliza darasa la saba hawajui hata mikoa 5 ya Tanzania au nchi kumi za Afrika, natumaini unatania.

Why, by darasa la nne nilikuwa na kijidaftari kilichorekodi karibu nchi zote za Afrika, miji mikuu, marais, idadi ya watu, lugha kuu na hela zinazotumika.

Huku sikosi kusikiza kipindi cha RTD cha Chris Katembo "Mkoa kwa Mkoa" kikinihabarisha kuhusu tamaduni na habari za mikoa yote ya Tanzania, pamoja na kingine kilichozungumzia nchi za Afrika, "Kutoka Afrika" or something like that, KU supplement kitabu cha "Wafanyakazi wa Afrika" cha Darasa la nne, kilichofundisha kuhusu kilimo cha Pamba Sudan kwa ramani za kuonesha Wadi zote, mpaka uchimbaji wa dhahabu namakaa ya mawe huko Witwatersrand.

Hivi vipindi, pamoja na vile vilivyokuwa vikitoa madarasa ya shule kwa redio, bado vipo au ni historia sasa?

Mtoto wa Darasa la nne leo ukimuuliza Wadi Hadad (aka Wad al Hadad) au Witwatersrand ni nini anaweza kujibu? Labda unamuone, unaweza kukuta hata mhitimu wa leo wa Chuo Kikuu hajui !

I will spare them Novaya Zemlya and Kamchatka for now. Lest some may not be able to locate Lake Tanganyika on the globe.

Enzi hizo tulizijua hadi nchi zinaitwa Vanuatu na Tuvalu....

But siku hizi Mulugo hajui hata Zimbabwe na Pemba ziko wapi halafu mnawalaumu graduates wa bongo kwa kushindwa kujiamini. Kansa kubwa kuliko zote kwenye elimu ya vyuo vikuu vya bongo ni wanafunzi kuangaliziana na kuingia na makaratasi yenye majibu, Mzumbe ndio wanaongoza ligi. Graduate asiyejiamini hata kujibu exams akaingia na majibu a.k.a MIG au akakaa kwenye mtandao wa kuangaliziana darasani hawezi kuongoza Portfolio hata $10,000.

Hii nchi CCM wameifikisha pabaya sana.
 
Nakumbuka in the early to mid 80s kulikuwa na bigjii flani hivi zilikuwa zinakuja kwenye paketi zenye vikadi vya bendera za nchi za Afrika na mabara mengine.

Watu tulikuwa tunashindana kuzikariri na kupeana vi pop quiz.

Zile za "Dandy". Made in Zimbabwe.Wakati huo Zimbabwe Zimbabwe ya ukweli sio hii iliyoharibiwa na hyperinflation ya Mugabe.

Ukipata bendera ya Tanzania bonge la deal, unaweza ku exchange na mtu akakupa bendera zaidi ya kumi. Za Tanzania for some reason zilikuwa hazionekani.

Tulizijua bendera za dunia nzima, kama sio hizi chewing gum basi nyuma ya atlas kule.
 
Back
Top Bottom