Enzi zetu wanafunzi wa darasa la nne wakipata muda katikati ya vipindi lazima kucheza na atlas sana.
Mtu lazima uulizwe kuonesha Kamchatka na Novaya Zemlya ziko wapi, up to this day nakumbuka vimiji vya Siberia huko kwa sababu tulikuwa makini kujifunza. Wenyewe. Outside of homework and teachers assignments.
Ninaposikia wanafunzi waliomaliza darasa la saba hawajui hata mikoa 5 ya Tanzania au nchi kumi za Afrika, natumaini unatania.
Why, by darasa la nne nilikuwa na kijidaftari kilichorekodi karibu nchi zote za Afrika, miji mikuu, marais, idadi ya watu, lugha kuu na hela zinazotumika.
Huku sikosi kusikiza kipindi cha RTD cha Chris Katembo "Mkoa kwa Mkoa" kikinihabarisha kuhusu tamaduni na habari za mikoa yote ya Tanzania, pamoja na kingine kilichozungumzia nchi za Afrika, "Kutoka Afrika" or something like that, Ku supplement kitabu cha "Wafanyakazi wa Afrika" cha darasa la nne, kilichofundisha kuhusu kilimo cha pamba Sudan kwa ramani za kuonesha Wadi zote, mpaka uchimbaji wa dhahabu namakaa ya mawe huko Witwatersrand.
Hivi vipindi, pamoja na vile vilivyokuwa vikitoa madarasa ya shule kwa redio, bado vipo au ni historia sasa?
Mtoto wa darasa la nne leo ukimuuliza Wadi Hadad (aka Wad al Hadad) au Witwatersrand ni nini anaweza kujibu? Labda utamuonea, unaweza kukuta hata mhitimu wa leo wa Chuo Kikuu hajui !
I will spare them Novaya Zemlya and Kamchatka for now. Lest some may not be able to locate Lake Tanganyika on the globe.