Ukweli lazima usemwe, Tunahitaji Muungano wa Serikali 1 tu

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Kati ya vitu vinavyofanya sisi waafrika tuendelee kuwa maskini ni kutotumia akili zetu vizuri na pia kupenda sana madaraka/ vyeo.

Nimefuatilia kwa muda sasa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na nilichogundua ni kuwa wale wengi wanaotaka Zanzibar iwe na Serikali au Tanganyika iwe na Serikali yake wengi ni wanasiasa na wanafanya yote hayo kwa maslahi ya kisiasa ili wapate vyeo vya kisiasa na kujinufaisha binafsi.

Pili, nimegundua uwepo wa Serikali 2 au 3 unawanufaisha zaidi hao wanasiasa kwa sababu uwepo wa Serikali hizo unawahikishia kupata nafasi za kisiasa ili waendelee kunufaika na kodi za wananchi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa , Wilaya katika Serikali hizo mbili/tatu.

Mwisho katika ufuatiliaji wangu nimegundua kero hizi zinazoitwa za Muungano kama wabara kutoweza kumiliki Ardhi Zanzibar kama Wa Zanzibar wanavyomiliki Ardhi huku bara dawa yake ni moja tu yaaani Kuwa na Nchi 1 na Serikali 1 tu na Raisi 1 tu.

Ni vizuri tukiwa tunaenda kujenga daraja la kuunganisha Zanzibar na Tanzania tukafikiria pia kuwa sasa tuwe na nchi 1 na serikali 1 tu ili kuepusha sehemu kubwa ya kodi za wananchi kwenda kuhudumia Serikali 2/3 tena ambazo kiuhalisia hazina manufaa yeyote kwa mwananchi wa kawaida

Heri ya Siku ya Wafanyakazi
 
Kuna shida sana kwenye hili dubwana Muungano. Kama hatutakubali kuweka maslahi binafsi pembeni tutakuja kugawana mbao tu siku
Mpaka leo huu Muungano umeshikiliwa na CCM na viongozi wake pekee. Maana wananchi wa kila upande wanaona unawanufaisha zaidi wananchi wa upande mwingine.

Na ukisema kuwepo Muungano wa nchi moja; Wazanzibari hawatakubali. Maana wao hawataki kupoteza utaifa wao, na nchi yao! Sasa watu kama hawa wanafaida gani kwenye huo Muungano! Zaidi tu ya kugeuka na kuwa mzigo kwa upande mwingine!!

Mimi natamani kuona siku moja kila upande unajitegemea kwa 100%. Ma siyo haya mauza uza yanayo endelea sasa.
 
Kati ya vitu vinavyofanya sisi waafrika tuendelee kuwa maskini ni kutotumia akili zetu vizuri na pia kupenda sana madaraka/ vyeo.

Nimefuatilia kwa muda sasa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na nilichogundua ni kuwa wale wengi wanaotaka Zanzibar iwe na Serikali au Tanganyika iwe na Serikali yake wengi ni wanasiasa na wanafanya yote hayo kwa maslahi ya kisiasa ili wapate vyeo vya kisiasa na kujinufaisha binafsi.

Pili, nimegundua uwepo wa Serikali 2 au 3 unawanufaisha zaidi hao wanasiasa kwa sababu uwepo wa Serikali hizo unawahikishia kupata nafasi za kisiasa ili waendelee kunufaika na kodi za wananchi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa , Wilaya katika Serikali hizo mbili/tatu.

Mwisho katika ufuatiliaji wangu nimegundua kero hizi zinazoitwa za Muungano kama wabara kutoweza kumiliki Ardhi Zanzibar kama Wa Zanzibar wanavyomiliki Ardhi huku bara dawa yake ni moja tu yaaani Kuwa na Nchi 1 na Serikali 1 tu na Raisi 1 tu.

Ni vizuri tukiwa tunaenda kujenga daraja la kuunganisha Zanzibar na Tanzania tukafikiria pia kuwa sasa tuwe na nchi 1 na serikali 1 tu ili kuepusha sehemu kubwa ya kodi za wananchi kwenda kuhudumia Serikali 2/3 tena ambazo kiuhalisia hazina manufaa yeyote kwa mwananchi wa kawaida

Heri ya Siku ya Wafanyakazi
Naunga mkono hoja Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, then "Twende kwenye Serikali Moja!"
p
 
Mpaka leo huu Muungano umeshikiliwa na CCM na viongozi wake pekee. Maana wananchi wa kila upande wanaona unawanufaisha zaidi wananchi wa upande mwingine.

Na ukisema kuwepo Muungano wa nchi moja; Wazanzibari hawatakubali. Maana wao hawataki kupoteza utaifa wao, na nchi yao! Sasa watu kama hawa wanafaida gani kwenye huo Muungano! Zaidi tu ya kugeuka na kuwa mzigo kwa upande mwingine!!

Mimi natamani kuona siku moja kila upande unajitegemea kwa 100%. Ma siyo haya mauza uza yanayo endelea sasa.
Hakuna cha kupoteza utaifa wala nini. Anafaidika nini kuwa mzanzibari? Tena kwa sasa Wazanzibar wengi ndo wanamiliki ardhi kuanzia kigamboni, ilala, temeke na hata maeneo ya Tanga

Hizo stori za kusema watapoteza utaifa wao ni maneno ya kisiasa tu yanayotumiwa na wanasiasa ili kulinda kula yao
 
Ni vizuri tukiwa tunaenda kujenga daraja la kuunganisha Zanzibar na Tanzania tukafikiria pia kuwa sasa tuwe na nchi 1 na serikali 1 tu ili kuepusha sehemu kubwa ya kodi za wananchi kwenda kuhudumia Serikali 2/3 tena ambazo kiuhalisia hazina manufaa yeyote kwa mwananchi wa kawaida
Hilo daraja litakuwa na manufaa gani kiuchumi, na nani atagharamia, Tanganyika au Zanzibar?!
 
Kitu nilichogundua na ambacho wanaopinga kwanza uwepo wa muungano ni aina fulani ya wanasiasa wa kitwana!, hawa wanawalisha sumu wazanzibari kuhusu muungano ilihali wao wanavuna na kutunza gharani.

Raia wasiyo na elimu, wenye ujinga na wapumbavu hao ndiyo chakula cha wanasiasa, mfano ukiwa Unguja unaweza sikia mtu (fools) anapiga kelele watanganyika warudi kwao 😄!, Ukimuuliza kwa nini, utasikia hapa siyo kwenu, na wewe kwenu wapi? 😁.

Bahati mbaya sana wazee waliondoka pasipo kumaliza tasjuni ya muungano nadhani wangekuwepo leo ingekuwa na serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania hakuna cha SMZ wala nini.
 
Na ungana Nawewe 100% Zanzibar ilitakiwa iwe kama Mkoa wa Tanzania ama Kwa njia za kidplomasia, au Kwa kutumia nguvu tu.
zenji hawatokubali na tumechelewa sana kwanza achana na serikali pamoja na viongozi tuje kimila na watu binafsi hatupendani na ule utengano wa bahari ndo kabisa ikawa kama watu wa mbali.


Wapo wanaopigia kelele serikali za majimbo hapa bongo ndani ya bara tu hatupendani kila mtu anajiona anaonewa mara hivi mara kile .


Ukitaka kujua siasa mbaya kaangalie serikali ya majimbo ya kenya na watu wake walivyo plus ukabili wamekuwa wakibaguana mda.

Haya yote solutuon yake n nn?

Ni bora watu wakaishi na pia kumshukuru Raisi ya kwanza Nyerere kuna vitu katumia akili sana mwanzoni sana ...
 
Kwa Wazanzibari huo ni muhali !!
Hawataki kabisa kusikia habari hiyo !!
Tukiamua twende kwenye serikali moja, then we just go ahead!, watu wanaitwa Wazanzibari ni ndani tuu ya muungano, nje ya muungano, hakuna Wanzanzibari wala Watanganyika, kuna Watanzania tuu.
P
 
Uchaguzi ujao pawekwe na kipengele Cha kupigia kura kuhusu muungano,yaani unapigia kura ,Kama ni unataka muungano wa serikari 1,au 2 ,au 3 ,unaweka vema (✓) pale unapopataka. hapo tutakuwa tumepata muafaka sahihi wa hili Jambo!! au ikiwezekana waweke na kipengele Cha kuvunja muungano .
 
Kati ya vitu vinavyofanya sisi waafrika tuendelee kuwa maskini ni kutotumia akili zetu vizuri na pia kupenda sana madaraka/ vyeo.

Nimefuatilia kwa muda sasa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na nilichogundua ni kuwa wale wengi wanaotaka Zanzibar iwe na Serikali au Tanganyika iwe na Serikali yake wengi ni wanasiasa na wanafanya yote hayo kwa maslahi ya kisiasa ili wapate vyeo vya kisiasa na kujinufaisha binafsi.

Pili, nimegundua uwepo wa Serikali 2 au 3 unawanufaisha zaidi hao wanasiasa kwa sababu uwepo wa Serikali hizo unawahikishia kupata nafasi za kisiasa ili waendelee kunufaika na kodi za wananchi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa , Wilaya katika Serikali hizo mbili/tatu.

Mwisho katika ufuatiliaji wangu nimegundua kero hizi zinazoitwa za Muungano kama wabara kutoweza kumiliki Ardhi Zanzibar kama Wa Zanzibar wanavyomiliki Ardhi huku bara dawa yake ni moja tu yaaani Kuwa na Nchi 1 na Serikali 1 tu na Raisi 1 tu.

Ni vizuri tukiwa tunaenda kujenga daraja la kuunganisha Zanzibar na Tanzania tukafikiria pia kuwa sasa tuwe na nchi 1 na serikali 1 tu ili kuepusha sehemu kubwa ya kodi za wananchi kwenda kuhudumia Serikali 2/3 tena ambazo kiuhalisia hazina manufaa yeyote kwa mwananchi wa kawaida

Heri ya Siku ya Wafanyakazi
Kawaambie wazanzibar ndio hawataki serikali moja.
 
Back
Top Bottom