Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,048
Kati ya vitu vinavyofanya sisi waafrika tuendelee kuwa maskini ni kutotumia akili zetu vizuri na pia kupenda sana madaraka/ vyeo.
Nimefuatilia kwa muda sasa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na nilichogundua ni kuwa wale wengi wanaotaka Zanzibar iwe na Serikali au Tanganyika iwe na Serikali yake wengi ni wanasiasa na wanafanya yote hayo kwa maslahi ya kisiasa ili wapate vyeo vya kisiasa na kujinufaisha binafsi.
Pili, nimegundua uwepo wa Serikali 2 au 3 unawanufaisha zaidi hao wanasiasa kwa sababu uwepo wa Serikali hizo unawahikishia kupata nafasi za kisiasa ili waendelee kunufaika na kodi za wananchi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa , Wilaya katika Serikali hizo mbili/tatu.
Mwisho katika ufuatiliaji wangu nimegundua kero hizi zinazoitwa za Muungano kama wabara kutoweza kumiliki Ardhi Zanzibar kama Wa Zanzibar wanavyomiliki Ardhi huku bara dawa yake ni moja tu yaaani Kuwa na Nchi 1 na Serikali 1 tu na Raisi 1 tu.
Ni vizuri tukiwa tunaenda kujenga daraja la kuunganisha Zanzibar na Tanzania tukafikiria pia kuwa sasa tuwe na nchi 1 na serikali 1 tu ili kuepusha sehemu kubwa ya kodi za wananchi kwenda kuhudumia Serikali 2/3 tena ambazo kiuhalisia hazina manufaa yeyote kwa mwananchi wa kawaida
Heri ya Siku ya Wafanyakazi
Nimefuatilia kwa muda sasa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na nilichogundua ni kuwa wale wengi wanaotaka Zanzibar iwe na Serikali au Tanganyika iwe na Serikali yake wengi ni wanasiasa na wanafanya yote hayo kwa maslahi ya kisiasa ili wapate vyeo vya kisiasa na kujinufaisha binafsi.
Pili, nimegundua uwepo wa Serikali 2 au 3 unawanufaisha zaidi hao wanasiasa kwa sababu uwepo wa Serikali hizo unawahikishia kupata nafasi za kisiasa ili waendelee kunufaika na kodi za wananchi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa , Wilaya katika Serikali hizo mbili/tatu.
Mwisho katika ufuatiliaji wangu nimegundua kero hizi zinazoitwa za Muungano kama wabara kutoweza kumiliki Ardhi Zanzibar kama Wa Zanzibar wanavyomiliki Ardhi huku bara dawa yake ni moja tu yaaani Kuwa na Nchi 1 na Serikali 1 tu na Raisi 1 tu.
Ni vizuri tukiwa tunaenda kujenga daraja la kuunganisha Zanzibar na Tanzania tukafikiria pia kuwa sasa tuwe na nchi 1 na serikali 1 tu ili kuepusha sehemu kubwa ya kodi za wananchi kwenda kuhudumia Serikali 2/3 tena ambazo kiuhalisia hazina manufaa yeyote kwa mwananchi wa kawaida
Heri ya Siku ya Wafanyakazi