Ukiwa na Uelewa na Ufahamu mpana na wa kutosha wa masuala mbalimbali, ukinyimwa, kukataliwa au kusubirishwa ulichoomba hutojiskia vibaya

Tlaatlaah

JF-Expert Member
May 18, 2023
8,166
11,569
Mathalani umeomba kazi ya kukuongezea kipato, umeomba mkopo benki au kausha damu, umeomba kura kwenye uchaguzi, umeomba ruhusa kazini au shuleni, umeomba urafiki wa kike au wa kiume, umeomba uchumba au ndoa nakadhalika. Uelewa na Ufahamu wako ukijitosheleza basi utajikuta unajiandaa vizuri sana kupokea matokeo yote yatakayo kuja, ambayo ni aidha kukubaliwa, kukataliwa au kusubirishwa, kwasabb ombi linaweza kukubaliwa, kukataliwa au kusubirishwa.

Na ipo siri moja tu ya kutojiskia vibaya endapo utakataliwa, kunyimwa au kusubirishwa ulichokiomba. Nayo ni Uelewa na ufahamu wa kutosha juu ya jambo lenyewe unaloomba.

Na ili ukomae na uimarike vizuri zaid katika hali hiyo na uione kama sehemu ya maisha yako, ni lazima kukataliwa, kunyimwa au kusubirishwa mara nyingi zaidi.

Na hapo ndipo utakua jasiri zaidi, hodari na mzoefu zaid wa kukataliwa, kunyimwa au kusubirishwa na kwahivyo hautakua ukijiskia vibaya ukinyimwa, ukikataliwa, au kusubirishwa chochote popote.

Sasa sikuizi vijana wakikataana au kusubirishana kidogo tu mathalani kwenye mahusianao, asi, matokeo yake wanadungana visu, wanachinjana, wanakunywa sumu au kujinyonga.

Hii inasababishwa zaidi na kutokua na uelewa na ufahamu mpana na wa kutosha juu ya walichoombana, kunyimana au kusubirishana, lakini zaidi sana kutokua na uzoefu wa kukataliwa, kunyimwa au kusubirishwa mara nyingi zaidi 🐒

kwahiyo omba mara nyingi zaidi uwezavyo, nyimwa au kataliwa mara nyingi zaidi, subirishwa sana ili hatimae uwe mzoefu na jasiri wa kunyimwa, kukataliwa na kusubirishwa, lakini pia kubaliwa mara chache zaidi ili uinjoy raha ya kukubaliwa.

Ukikua utalewa 🐒
 
Hii inasababishwa zaidi na kutokua na uelewa na ufahamu mpana na wa kutosha juu ya walichoombana, kunyimana au kusubirishana, lakini zaidi sana kutokua na uzoefu wa kukataliwa, kunyimwa au kusubirishwa mara nyingi zaidi 🐒

kwahiyo omba mara nyingi zaidi uwezavyo, nyimwa au kataliwa mara nyingi zaidi, subirishwa sana ili hatimae uwe mzoefu na jasiri wa kunyimwa, kukataliwa na kusubirishwa, lakini pia kubaliwa mara chache zaidi ili uinjoy raha ya kukubaliwa....

ukikua utalewa 🐒
mtumishi leo unatufundisha umalaya

kwanini niwe na uzoefu wa kusubirishwa, mungu si alisema tuwe na mmoja tu?
 
mtumishi leo unatufundisha umalaya

kwanini niwe na uzoefu wa kusubirishwa, mungu si alisema tuwe na mmoja tu?
Unaweza omba upate IST mwaka huu 2024 ukasubirishwa hadi 2027..


lakini pia unaweza omba upate kiwanja mwezi December 2024 atakufanyia wepesi ukapata mapema zaidi labda June 2024..

Unaweza omba upate mchumba ukakataliwa kumbe umeepushwa na jumba bovu hakua sahihi kwako akakuongoza kwingineko n.k

usishupaze shingo sana ukikataliwa, ukinyimwa au kusubirishwa lipo kusudi la yote hayo kwajili yako

subira yavuta kheri sio mzaha ni kweli kabisaa
 
Mtumishi mfano ulikuwa kweny kazi fulani unapiga pesa ,ghafla ukaondolewa wala hakufanya kosa kama la kinidhamu yaani imetokea umepelekwa kwingine...Kufikaq huko mshahara ukashuka kama nusu halafu hata posho zikakata kabisa,je hapo unasemaje kwa maoni yako?

Vijana wengi hata mirija ya pesa ikikata basi anaweza kujimaliza
 
Unaweza omba upate IST mwaka huu 2024 ukasubirishwa hadi 2027..


lakini pia unaweza omba upate kiwanja mwezi December 2024 atakufanyia wepesi ukapata mapema zaidi labda June 2024..

Unaweza omba upate mchumba ukakataliwa kumbe umeepushwa na jumba bovu hakua sahihi kwako akakuongoza kwingineko n.k

usishupaze shingo sana ukikataliwa, ukinyimwa au kusubirishwa lipo kusudi la yote hayo kwajili yako

subira yavuta kheri sio mzaha ni kweli kabisaa
kukataliwa kunatosha kuthibitisha mungu hayupo

mungu anakubalije mja wake akataliwe, anyimwe, asubirishwe? wakati kasema kila mmoja ana ubavu wake wa milele

shtuka
 
Mwana CCM mwenzangu, uzi mzuri huu… unawafaa vijana ila ndio hautawaona hapa! Wapo huko wanalia lia 😅

Anyways, kumbe kuna muda UVCCM zinachaji?

ndezi sana 🤣

sasa we binti u18 unafanya nn humu aise umeacha kujisomea 🤣

nyie ndio wale JK alisema muache viherehere
 
Tatizo wengi wanakosa stamina ya hisia zao. Kuna mdau hapo juu kasema Emotional intelligence bila hiyo ni kuteseka tu.
Yes, emotional stability ni muhimu sana kwa mwanadamu....

For sure kua na uwezo wa kudhibiti hisia zako katika mambo mbalimbali ni jambo la maana sana popote pale ulipo....

Mfano leo hii vjana wengi wameathirika na tatizo la nguvu xa kijinsia kwasabb hawakujengewa au kufunzwa namna ya kudhibiti hisia zao.

matokeo yake kijana akiona upaja tu wa mwanamke mshedede au mnara unapanda hewani kwa kasi ya 4g chap maramoja anakimbilia sabuni bafuni na kujichukulia Sheria mkononi....
au akiangalia tuvideo twa ngono Lazima amalize hawezi kujizuia kabisaa ni dhaifu sana...

Ziko namna nyingi za kudhibiti hisia na mihemko yenye kuleta madhara kwako au kwa wengine 🐒
 
Mathalani umeomba kazi ya kukuongezea kipato, umeomba mkopo benki au kausha damu, umeomba kura kwenye uchaguzi, umeomba ruhusa kazini au shuleni, umeomba urafiki wa kike au wa kiume, umeomba uchumba au ndoa nakadhalika. Uelewa na Ufahamu wako ukijitosheleza basi utajikuta unajiandaa vizuri sana kupokea matokeo yote yatakayo kuja, ambayo ni aidha kukubaliwa, kukataliwa au kusubirishwa, kwasabb ombi linaweza kukubaliwa, kukataliwa au kusubirishwa.

Na ipo siri moja tu ya kutojiskia vibaya endapo utakataliwa, kunyimwa au kusubirishwa ulichokiomba. Nayo ni Uelewa na ufahamu wa kutosha juu ya jambo lenyewe unaloomba.

Na ili ukomae na uimarike vizuri zaid katika hali hiyo na uione kama sehemu ya maisha yako, ni lazima kukataliwa, kunyimwa au kusubirishwa mara nyingi zaidi.

Na hapo ndipo utakua jasiri zaidi, hodari na mzoefu zaid wa kukataliwa, kunyimwa au kusubirishwa na kwahivyo hautakua ukijiskia vibaya ukinyimwa, ukikataliwa, au kusubirishwa chochote popote...

Sasa sikuizi vijana wakikataana au kusubirishana kidogo tu mathalani kwenye mahusianao,
basi, matokeo yake wanadungana visu, wanachinjana, wanakunywa sumu au kujinyonga.

Hii inasababishwa zaidi na kutokua na uelewa na ufahamu mpana na wa kutosha juu ya walichoombana, kunyimana au kusubirishana, lakini zaidi sana kutokua na uzoefu wa kukataliwa, kunyimwa au kusubirishwa mara nyingi zaidi 🐒

kwahiyo omba mara nyingi zaidi uwezavyo, nyimwa au kataliwa mara nyingi zaidi, subirishwa sana ili hatimae uwe mzoefu na jasiri wa kunyimwa, kukataliwa na kusubirishwa, lakini pia kubaliwa mara chache zaidi ili uinjoy raha ya kukubaliwa....

ukikua utalewa 🐒
Umenyimwa nini Tlaatlaah Mbadiba🤸‍♂️🤸‍♂️🤸‍♂️🤸‍♂️🤸‍♂️🤸‍♂️🤸‍♂️
 
Mtumishi mfano ulikuwa kweny kazi fulani unapiga pesa ,ghafla ukaondolewa wala hakufanya kosa kama la kinidhamu yaani imetokea umepelekwa kwingine...Kufikaq huko mshahara ukashuka kama nusu halafu hata posho zikakata kabisa,je hapo unasemaje kwa maoni yako?

Vijana wengi hata mirija ya pesa ikikata basi anaweza kujimaliza
maoni yangu ni kwamba,
yawezekana vigezo, sifa , uwezo na nyota yako apo kazini vinangara zaidi ya ulowakuta hapo ofisini na hivyo unatishia na kuwapa kimuhemuhe kwamba wakikuacha apo ulipo, haita chukua muda utachukua nafasi zao ....
Kwahiyo unahatarisha nafasi za watu mkuu nenda pole pole kujipambanua.....

Jambo la pili ni kwamba,
huenda wew umekua ni kikwazo cha wao kuendelea kupiga pesa ndefu na kwamba wew ni mtu wa utaratibu na misimamo sana, hupendi konakona hata kwa wakubwa zako ofisini pako...

Jambo la Tatu,
huenda kuna uchawi na ushirikina ndani yake, na hivyo vinawapa ujasiri wa kukuhamisha na kukushusha mshahara na cheo bila wew kuripoti wala kulalamika panapohusika. Wamekufunga mdomo na misuli ya uchumi wako kichawi ukae kimya uone ni jambo la kawaida tu...

Jambo la nne,
Ukiwa kazini, ukitaka kufurahia maisha na kudumu katika status ya juu daima au kwa muda mrefu, na kwa uhakika basi pata kazi kwa haki, fanya kazi kwa bidii na upate kipato halali na sahihi kwa kazi na nafasi ulonayo...

Lakini kupata kwa uchawi na ushirikina na kujipatia kipato kisicho halali huwez enjoy maisha wala kua na uhakika wa kudumu apo kazini, daima utakua mtumwa wa hirizi. Huwez kua na Amani....

hayo ni kwa uchache sana. Endelea kumtegemea Mungu, jishushe kwa kwa wakati huu unaponyanyasika bila sababu, na kwa wakati muafaka Mungu mwenyezi atakupandisha juu, kwani ndipo unapostahili 🐒
 
Namshukuru Mungu kwa kunipa uwezo wa kusubiri na uvumilivu.
Kama kuna taji hakika nitavikwa!
Nifah you are always positive when I see your comments on other topics and platforms,

halafu uko mwepesi mno Kumshukuru Mungu and thus ni kitu nxuri sana aise,
hiyo nguvu ya subra na ustahimilivu ni Baraka zake kwako, bila hivyo ni ngumu sana kusubiri na kua mstahimilivu...
 
Nifah you are always positive when I see your comments on other topics and platforms,

halafu uko mwepesi mno Kumshukuru Mungu and thus ni kitu nxuri sana aise,
hiyo nguvu ya subra na ustahimilivu ni Baraka zake kwako, bila hivyo ni ngumu sana kusubiri na kua mstahimilivu...
Amen,
Nashukuru sana.
 
Back
Top Bottom