Ukifa, hutatamani tena kuishi duniani!

Ukifa, hutatamani tena kuishi duniani!

kuna bandiko moja nadhani ni la Mshana Jr niliwahi kulisoma humu jukwaani kuhusu habari ya kifo, na kwamba watu huogopa kifo kwasababu hawako ndani ya hicho kifo, lakini wakiishaingia ndani ya hicho kifo hofu ile hutoweka kwasababu tayari wanakua ndani ya kifo, vile vile hata kuingia motoni au akhera inakua hivyo hivyo,

kwasababu haujaingia motoni bado unaweza kua na hofu, lakini ukisharushwo motoni ile hofu mara moja inatoweka na unakua mzoefu pale motoni:pedroP:

so,
kuogopa kua mahali usikokujua ni kwa muda tu, ila ukishaingia huko hofu ile inatoweka na unakua mzoefu na tamaa ya kua duniani au motoni inakua haipo tena. :BASED:
Hii ni Kali 😂🤣.
 
Maisha ya kimwili ni maisha ya level ya chini sana na yana mwisho wake lakini kuna maisha ya juu, nayo ni maisha ya kiroho ambapo maisha bila miili yetu yanawezekana. Kuna viumbe vinaishi bila miili, e.g. majini, malaika, mashetani, na vingi vingine.
Unauhakika hao viumbe wisivyo na miili wapo?
 
Kifo si mwisho wa mchakato wa uhai wetu, bali ni mlango mtakatifu unaofungua ukurasa wa mwanzo mpya na wa milele.

Mwili wa nyama unaporudi mavumbini na kukamilisha safari yake ya kibiolojia, roho haifi; inavua vazi hili la udongo lenye mipaka, maumivu, na machozi, tayari kuvuka ng’ambo ya mto wa uzima.

Huu ni wakati wa kiroho ambapo nishati ya kimungu iliyomo ndani yetu inarejea kwenye chanzo chake kikuu, ikiwa imeandaliwa kuanza safari mpya katika ulimwengu wa utukufu na mwanga usiotiwa giza.

Katika hatua hii, fahamu yetu haizimiki bali inalindwa na kufanywa upya, ikisafiri kwa amani kuelekea maskani ya milele ambako hakuna tena muda, uzee, wala uharibifu, bali ukamilifu wa upendo wa kimungu.
Duh, mkuu tangu ulipotupa matunguli umekuwa mtu sana! Hii shule ni kubwa sana!
 
Mkuu ngoja nikuulize. Hivi mwaka 1800 ulikuwepo duniani? Ninauhakika haukuwepo. Kama haukuwepo ulijisikiaje (ulikuwa na hisia gani) mwaka 1800?
Bado haujaelewa mantiki ya swali langu naona.

Ninachotaka kufahamu ni uhakika gani ulio nao juu ya hiki ulicho kisema?

Kwa sababu umeongea ukiwa na uhakika sana, nahitaji tu kufahamu je una experience ya hiki ulicho sema?

Je una mtu yoyote labda aliyewahi kuwa marehemu then akawa hai akakudokeza haya?
 
Kifo si mwisho wa mchakato wa uhai wetu, bali ni mlango mtakatifu unaofungua ukurasa wa mwanzo mpya na wa milele.

Mwili wa nyama unaporudi mavumbini na kukamilisha safari yake ya kibiolojia, roho haifi; inavua vazi hili la udongo lenye mipaka, maumivu, na machozi, tayari kuvuka ng’ambo ya mto wa uzima.

Huu ni wakati wa kiroho ambapo nishati ya kimungu iliyomo ndani yetu inarejea kwenye chanzo chake kikuu, ikiwa imeandaliwa kuanza safari mpya katika ulimwengu wa utukufu na mwanga usiotiwa giza.

Katika hatua hii, fahamu yetu haizimiki bali inalindwa na kufanywa upya, ikisafiri kwa amani kuelekea maskani ya milele ambako hakuna tena muda, uzee, wala uharibifu, bali ukamilifu wa upendo wa kimungu.

Toka watu wameanza kufa, huko maskani ya milele hakujajaa tuu mkuu?.
 
Back
Top Bottom