Ni ngumu kuachwa hasa na mtu unaempenda. Wengine wanakuambia tumefika mwisho wa barara, gari yetu ya mapenzi haiendelei na safari. Kuna wanaotoa visingizio, unakuta miezi mitatu hamjaonana wala kuwa na maongezi ya kueleweka. Kila siku atadai yuko busy. Mmh huu u busy mbona unapata muda wa kuoga kula na kulala kama mimi bado ni wa muhimu kwako.
Awe mwanamke au mwanaume. Kama amefikia hatua hiyo, ingawa ni ngumu lakini kubali matokeo. Kumbuka yeye ni mtu mzima ana sababu zake katika maamuzi hayo.
Sasa kuna wale wa binafsi wanaotishia kunywa sumu, kulia, kujiumiza. Mpenzi wewe unafarijika kuwa nae lakini ukumbuke kuwa uwepo wako kwake si faraja tena.