Kwa hakika Allah atuongoze ktk njia iliyonyooka Sasa watu hatujidai ni waislam Bali tunajidai ni kundi flani aisee
Kwa uelewa wako.
Ila kwa kuwa ulojibiwa ni wewe napaswa kukuelimisha nanukuu swali... (kwa hiyo wewe ni Salafy..?) jibu likaja (ndio)
Labda hujui maana ya Salafy ndio maana unataka uweke tofauti na Uislamu iko hivi.....
NINI MAANA YA SALAF NA YUPI SALAFY?
Neno ﺳﻠﻔﻲ (salaf) linakusudiwa Wema waliopita na Al muhimu ni Wanafunzi na wafuasi wake mtume ﺻﻞ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ yaani SALAFI ni MASAHABA
Mtu wa kwanza kutumia neno SALAFI ni mtume ﺻﻞ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ
alipomwambia mwanae bi Faatima ﺭﺿﻲ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻨﻬﺎ
" ﻓﺎﺗﻘﻲ ﺍﻟﻠﻪ ﻭﺍﺻﺒﺮﻱ ﻓﺎﺀﻧﻪ ﻧﻌﻢ ﺍﻟﺴﻠﻒ ﺍﻧﺎ ﻟﻚ "
"Mche Allah na kuwa na Subra kwani mi ni Bora katika Salafi kwako"
-------------------------
Sahih Bukhaary - Mjeredi wa 8 hadith ya 58885
Neno salafi limetumiwa sana na WANACHUONI kuanzia wa Kale mpaka baadhi wa zama za leo
Mfano IMAM AHMAD Ibn HAMBAL ﺭﺣﻤﻪ ﺍﻟﻠﻪ
IMAM ABU HANIFAH na wengi katika wao.
Salafiyyah (wanaofuata Mafundisho ya mtume kama walivyofahamu masahaba zake) Huitwa pia AHLU HADITH, AL ATHARI, AHLU SUNNAH WAL JAMAA na mfano wake
DAAWA YA SALAFI IMESIMAMIA MISINGI GANI?
Kufuata Aqeedah (ITIKADI) mambo yaliyofungamana na imaan kama Alivyofundisha mtume na ufahamu wa masahaba
Kushikamana na Sunnah vilivyo katika kila Ibaada na kujitenga na Bid'a kbs
Salafiyyah ni watu wanahimiza sana TAWHIID na kukaa mbali kbs na Shirk kwa nguvu zote
Salafiyyah huwaigiza Mtume na masahaba zake tabia zao njema walizoshikana nazo
Manhaj (njia yao Mtume na masahaba)
............................
kwanini mtu afuate Manhaj SALAFI ni kwa sababu zifiatazo
DALILI katika QUR'AN
Allah Jalla wa'ala amesema
ﻓَﺠَﻌَﻠْﻨَﺎﻫُﻢْ ﺳَﻠَﻔًﺎ ﻭَﻣَﺜَﻠًﺎ ﻟِﻠْﺂﺧِﺮِﻳﻦَ
Kisha tukawafanya kuwa watangulizi na mfano kwa wa baadaye...
Az Zukhruf : 56
------------------------------
ﻓَﺈِﻥْ ﺁﻣَﻨُﻮﺍ ﺑِﻤِﺜْﻞِ ﻣَﺎ ﺁﻣَﻨْﺘُﻢْ ﺑِﻪِ ﻓَﻘَﺪِ ﺍﻫْﺘَﺪَﻭْﺍ ۖ ﻭَﺇِﻥْ ﺗَﻮَﻟَّﻮْﺍ ﻓَﺈِﻧَّﻤَﺎ ﻫُﻢْ ﻓِﻲ ﺷِﻘَﺎﻕٍ ۖ ﻓَﺴَﻴَﻜْﻔِﻴﻜَﻪُﻡُ ﺍﻟﻠَّﻪُ ۚ ﻭَﻫُﻮَ ﺍﻟﺴَّﻤِﻴﻊُ ﺍﻟْﻌَﻠِﻴﻢُ
Basi wakiamini kama mnavyo amini nyinyi (Kundi la Masahaba na mtume), itakuwa kweli wameongoka. Na wakikengeuka basi wao wamo katika upinzani tu. Na Mwenyezi Mungu atakutosheni kukukingeni na shari yao, na Yeye ndiye Msikizi, Mjuzi....
Al Baqarah : 137
-----------------------------
KWANINI UFUATE MASAHABA (SALAFI) ufahamu wao kwa kila JAMBO?
dalili katika sunnah
Amesema mtume ﺻﻞ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ
" ﺧﻴﺮ ﺍﻟﻨﺎﺱ ﻗﺮﻧﻲ، ﺛﻢ ﺍﻟﺰﻳﻦ ﻳﻠﻮﻧﻬﻢ، ﺛﻢ ﺍﻟﺰﻳﻦ ﻳﻠﻮﻧﻬﻢ "
"Watu bora kabisa ni Karne yangu (masahaba) kisha wataofuata (tabiin) kisha karne itakayofuata (at'bau Tabiin)
Imepokewa na Bukhaary
---------------------------------
Amesema Mtume ﺻﻞ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ
" ﻭﺍﻧﻪ ﻣﻦ ﻳﻌﺶ ﻣﻨﻜﻢ ﻓﺴﻴﺮ ﻱ ﺍﺧﺘﻼﻓﺎ ﻛﺜﻴﺮﺍ
Yeyote atakayeishi muda mrefu baada yangu ataona Makasoro mengi katika dini hii
ﻓﻌﻠﻴﻜﻢ ﺑﺴﻨﺘﻲ ﻭﺳﻨﺔ ﺍﻟﺨﻠﻔﺎﺀ ﺍﻟﺮﺍﺷﺪﻳﻦ ﺍﻟﻤﻬﺪﻳﻴﻦ
""Shikamaneni na sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa wangu waongofu"
Ameipokea Abu Dawuud na At tirmidhy