Ujumbe kwa Waislamu wenzangu

Ujumbe kwa Waislamu wenzangu

Kwa uelewa wako.
Ila kwa kuwa ulojibiwa ni wewe napaswa kukuelimisha nanukuu swali... (kwa hiyo wewe ni Salafy..?) jibu likaja (ndio)
Labda hujui maana ya Salafy ndio maana unataka uweke tofauti na Uislamu iko hivi.....
NINI MAANA YA SALAF NA YUPI SALAFY?
Neno ﺳﻠﻔﻲ (salaf) linakusudiwa Wema waliopita na Al muhimu ni Wanafunzi na wafuasi wake mtume ﺻﻞ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ yaani SALAFI ni MASAHABA
Mtu wa kwanza kutumia neno SALAFI ni mtume ﺻﻞ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ
alipomwambia mwanae bi Faatima ﺭﺿﻲ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻨﻬﺎ
" ﻓﺎﺗﻘﻲ ﺍﻟﻠﻪ ﻭﺍﺻﺒﺮﻱ ﻓﺎﺀﻧﻪ ﻧﻌﻢ ﺍﻟﺴﻠﻒ ﺍﻧﺎ ﻟﻚ "
"Mche Allah na kuwa na Subra kwani mi ni Bora katika Salafi kwako"
-------------------------
Sahih Bukhaary - Mjeredi wa 8 hadith ya 58885
Neno salafi limetumiwa sana na WANACHUONI kuanzia wa Kale mpaka baadhi wa zama za leo
Mfano IMAM AHMAD Ibn HAMBAL ﺭﺣﻤﻪ ﺍﻟﻠﻪ
IMAM ABU HANIFAH na wengi katika wao.
Salafiyyah (wanaofuata Mafundisho ya mtume kama walivyofahamu masahaba zake) Huitwa pia AHLU HADITH, AL ATHARI, AHLU SUNNAH WAL JAMAA na mfano wake
DAAWA YA SALAFI IMESIMAMIA MISINGI GANI?
Kufuata Aqeedah (ITIKADI) mambo yaliyofungamana na imaan kama Alivyofundisha mtume na ufahamu wa masahaba
Kushikamana na Sunnah vilivyo katika kila Ibaada na kujitenga na Bid'a kbs
Salafiyyah ni watu wanahimiza sana TAWHIID na kukaa mbali kbs na Shirk kwa nguvu zote
Salafiyyah huwaigiza Mtume na masahaba zake tabia zao njema walizoshikana nazo
Manhaj (njia yao Mtume na masahaba)
............................
kwanini mtu afuate Manhaj SALAFI ni kwa sababu zifiatazo
DALILI katika QUR'AN
Allah Jalla wa'ala amesema
ﻓَﺠَﻌَﻠْﻨَﺎﻫُﻢْ ﺳَﻠَﻔًﺎ ﻭَﻣَﺜَﻠًﺎ ﻟِﻠْﺂﺧِﺮِﻳﻦَ
Kisha tukawafanya kuwa watangulizi na mfano kwa wa baadaye...
Az Zukhruf : 56
------------------------------
ﻓَﺈِﻥْ ﺁﻣَﻨُﻮﺍ ﺑِﻤِﺜْﻞِ ﻣَﺎ ﺁﻣَﻨْﺘُﻢْ ﺑِﻪِ ﻓَﻘَﺪِ ﺍﻫْﺘَﺪَﻭْﺍ ۖ ﻭَﺇِﻥْ ﺗَﻮَﻟَّﻮْﺍ ﻓَﺈِﻧَّﻤَﺎ ﻫُﻢْ ﻓِﻲ ﺷِﻘَﺎﻕٍ ۖ ﻓَﺴَﻴَﻜْﻔِﻴﻜَﻪُﻡُ ﺍﻟﻠَّﻪُ ۚ ﻭَﻫُﻮَ ﺍﻟﺴَّﻤِﻴﻊُ ﺍﻟْﻌَﻠِﻴﻢُ
Basi wakiamini kama mnavyo amini nyinyi (Kundi la Masahaba na mtume), itakuwa kweli wameongoka. Na wakikengeuka basi wao wamo katika upinzani tu. Na Mwenyezi Mungu atakutosheni kukukingeni na shari yao, na Yeye ndiye Msikizi, Mjuzi....
Al Baqarah : 137
-----------------------------
KWANINI UFUATE MASAHABA (SALAFI) ufahamu wao kwa kila JAMBO?
dalili katika sunnah
Amesema mtume ﺻﻞ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ
" ﺧﻴﺮ ﺍﻟﻨﺎﺱ ﻗﺮﻧﻲ، ﺛﻢ ﺍﻟﺰﻳﻦ ﻳﻠﻮﻧﻬﻢ، ﺛﻢ ﺍﻟﺰﻳﻦ ﻳﻠﻮﻧﻬﻢ "
"Watu bora kabisa ni Karne yangu (masahaba) kisha wataofuata (tabiin) kisha karne itakayofuata (at'bau Tabiin)
Imepokewa na Bukhaary
---------------------------------
Amesema Mtume ﺻﻞ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ
" ﻭﺍﻧﻪ ﻣﻦ ﻳﻌﺶ ﻣﻨﻜﻢ ﻓﺴﻴﺮ ﻱ ﺍﺧﺘﻼﻓﺎ ﻛﺜﻴﺮﺍ
Yeyote atakayeishi muda mrefu baada yangu ataona Makasoro mengi katika dini hii
ﻓﻌﻠﻴﻜﻢ ﺑﺴﻨﺘﻲ ﻭﺳﻨﺔ ﺍﻟﺨﻠﻔﺎﺀ ﺍﻟﺮﺍﺷﺪﻳﻦ ﺍﻟﻤﻬﺪﻳﻴﻦ
""Shikamaneni na sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa wangu waongofu"
Ameipokea Abu Dawuud na At tirmidhy
Makala marefu ya kumjib muislam mwenzio lkn hayana hata nukta muhim ya kutofautisha wewe na uislam sahihi kitabu na Sunna ndo msingi wa uislm Sasa umetofautisha nn ndugu yangu Dua kubwa ALLAH ATUONGOZE na Jenga fikra ukikosea au kupatia ni katika dini sio potwe fulani hapo tutafika na Wala hatutachukiana ili ipatikane kuchukiana kwa ajili ya Allah na kupendana kwa ajili ya Allah lazima tuweze kutofautisha uislam na makundi ikiwa na lengo la kugawa waislam kwa ujadid tu,akhy huo ulioutaja ni msimamo wa ahlul Sunna Wal jamaa sio kundi fulan lijinasibishe ndo tunafata hivii hatutaeleweka ndugu zanguni!
 
Assalam alaykum warahmatullahi wabarakatuh

TUFANYE NINI PINDI TUKIKUTA COMMENTS ZA KUMTUKANA ALLAH NA MTUME WAKE AU UISLAMU KATIKA MITANDAO YA KIJAMII?

SHEIKH ABUL KHATWAAB ABDALLAH HUMEID حفظه الله

Naam naomba niwasilishe kile ambacho kidogo Allah alichonijaalia

Ujumbe huu mahsusi kwa watu wa mitandao.

kwenye Mitandao humu hutokea mijadala mingi inayohusu Kuuliza au kuelezea imani tofauti.

Ila sana mijadala hii huishia kwenye chuki kubwa baina ya watu ambao hata hawajuani.

Tahadhari ninayotoa kwa Ndugu zangu waislamu msipende kujadiliana na mtu ambae hataki kuelimishwa ambae amekuja kwa nia ya chuki kuhusu Uislamu wetu.

Allah anasema katika Qur'an yake

6:108.
Wala msiwatukane hao wanao waomba badala ya Mwenyezi Mungu, wasije na wao wakamtukana Mwenyezi Mungu kwa jeuri bila ya kujua. Namna hivyo tumewapambia kila umma vitendo vyao. Kisha marejeo yao yatakuwa kwa Mola wao Mlezi, naye atawaambia waliyo kuwa wakiyatenda.

Kulingana na Aya hio ni bora zaidi ukaachana na mijadala ambayo itapelekea Allah kutukanwa


Otterhound adriz FaizaFoxy
Kwanza nimekusifu sana kwa kunukuu AYA toka kwenye kitabu mnachoongozwa nacho, HONGERA. Maana kumuonya mtu, muonye kwa kutumia kitu au jambo analoliamini. Ila nikuambie kuwa, ni waislamu wachache sana wanaoweza kwenda na aya hiyo..!! Wengi hawana uvumilivu wa kidini. Na hii ndiyo sababu kubwa utasikia MTOTO KAKOJOLEA KURANI, BASI SOLUTION WANAITANA KWA TAKBIR, na haoo kwenda kuvunja kanisa..!! Sijui huyu kamtukana mtume wenu, hao wanaandamana kwenda kuvunja kanisa au kupiga mkristo yeyote..!!
Hivi si unajua kuwa yule aliyeandika kitabu cha SATANIC VERSES, bwana Salman Rushdie anasakwa hatari..!!?? Sababu ni kuwa wanaosaka hawaifuati aya hiyo..!! Juzi hapa kuna mwamba alimtwanga risasi, embu angalia idadi ya waislamu walioshangilia tukio hilo..!!
 
Tatizo baadhi yenu huwa mnakejeli sana, mnajiona mnajua kila kitu, mnajiona nyie ndo mko sahihi wengine ni wajinga na wamepotoka, nyie ndo wenye haki zaidi ya wengine.

Hayo ndo hufanya watu watuoe lugha chafu.
Ila hii kitu ni nzuri hasa kwa sisi tunaopenda kujifunza uislam.
Hivi umeelewa ulichoandika, na je umesoma vizuri, kilichoandikwa ukaelewa.

Hivi ni imani gani, wanajiona wao hawako sahihi, nenda pale msimbazi center, Wamezuia kuingia Wakristo wenzao wale wana maombi.
 
Kwanza nimekusifu sana kwa kunukuu AYA toka kwenye kitabu mnachoongozwa nacho, HONGERA. Maana kumuonya mtu, muonye kwa kutumia kitu au jambo analoliamini. Ila nikuambie kuwa, ni waislamu wachache sana wanaoweza kwenda na aya hiyo..!! Wengi hawana uvumilivu wa kidini. Na hii ndiyo sababu kubwa utasikia MTOTO KAKOJOLEA KURANI, BASI SOLUTION WANAITANA KWA TAKBIR, na haoo kwenda kuvunja kanisa..!! Sijui huyu kamtukana mtume wenu, hao wanaandamana kwenda kuvunja kanisa au kupiga mkristo yeyote..!!
Hivi si unajua kuwa yule aliyeandika kitabu cha SATANIC VERSES, bwana Salman Rushdie anasakwa hatari..!!?? Sababu ni kuwa wanaosaka hawaifuati aya hiyo..!! Juzi hapa kuna mwamba alimtwanga risasi, embu angalia idadi ya waislamu walioshangilia tukio hilo..!!
Wengi hao hawana elimu ni wakurupukaji hao Uislamu haujatufundisha ivo

Pia kuna aya hii inotufundisha jinsi ya kulingania watu



( ادْعُ إِلَىٰ سَبِيلِ رَبِّكَ بِالْحِكْمَةِ وَالْمَوْعِظَةِ الْحَسَنَةِ ۖ وَجَادِلْهُم بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ ۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ ۖ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ )

النحل (125) An-Nahl

Waite waelekee kwenye Njia ya Mola wako Mlezi kwa hikima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
 
Hivi umeelewa ulichoandika, na je umesoma vizuri, kilichoandikwa ukaelewa.

Hivi ni imani gani, wanajiona wao hawako sahihi, nenda pale msimbazi center, Wamezuia kuingia Wakristo wenzao wale wana maombi.
Nimeelewa ndo maana nikatia neno ndgu, mimi na wewe hatujaishi pamoja hivyo naongelea nilivhokutana nacho na nnachokiona.

Huenda wewe ndie hujaelewa kilichoandikwa.

Wote hujiona wako sahihi lakini sio kufikia hatua ya kubeza na kukebehi imani ya watu wengine, ndicho nilichokiandika hapo ndgu. Umejibu kihisia zaidi bila akili.
 
Makala marefu ya kumjib muislam mwenzio lkn hayana hata nukta muhim ya kutofautisha wewe na uislam sahihi kitabu na Sunna ndo msingi wa uislm Sasa umetofautisha nn ndugu yangu Dua kubwa ALLAH ATUONGOZE na Jenga fikra ukikosea au kupatia ni katika dini sio potwe fulani hapo tutafika na Wala hatutachukiana ili ipatikane kuchukiana kwa ajili ya Allah na kupendana kwa ajili ya Allah lazima tuweze kutofautisha uislam na makundi ikiwa na lengo la kugawa waislam kwa ujadid tu,akhy huo ulioutaja ni msimamo wa ahlul Sunna Wal jamaa sio kundi fulan lijinasibishe ndo tunafata hivii hatutaeleweka ndugu zanguni!
Duh ndugu kwani nilisema nakusudia kutofautisha mbona tunaelewana kinyume nilichomaanisha Uislamu ni kufuata Qur'an na Sunnah kwa ufahamu wa Salafy kinyume chake ni kujihangaisha tu
 
Duh ndugu kwani nilisema nakusudia kutofautisha mbona tunaelewana kinyume nilichomaanisha Uislamu ni kufuata Qur'an na Sunnah kwa ufahamu wa Salafy kinyume chake ni kujihangaisha tu
Ndugu yangu fahar yangu ni kuwa na wewe muislam ndugu yangu sio kuwa pamoja kwasabb ya usalafy hicho mie ndo nachotofautiana na ndugu zangu wengi
 
Duh ndugu kwani nilisema nakusudia kutofautisha mbona tunaelewana kinyume nilichomaanisha Uislamu ni kufuata Qur'an na Sunnah kwa ufahamu wa Salafy kinyume chake ni kujihangaisha tu

Nisemapo mimi ni Salafy elewa Mimi ni muislam ninaefuata Qur'an na Sunnah kwa ufahamu wa wema waliotangulia
 
Ndugu yangu fahar yangu ni kuwa na wewe muislam ndugu yangu sio kuwa pamoja kwasabb ya usalafy hicho mie ndo nachotofautiana na ndugu zangu wengi
Labda unipe katazo kwa hili nililosimamia ili nifuate hiyo FAHARI YAKO ndugu
 
Nisemapo mimi ni Salafy elewa Mimi ni muislam ninaefuata Qur'an na Sunnah kwa ufahamu wa wema waliotangulia
Hata napoghafilika ujue nimeghafilka ktk uislam sio ktk potwe fulqni ndugu zanguni makundi ya usalafi yanatokana na nn mpaka tutupiqne maneno ikiwa Letu lote liwe moja
 
Hata napoghafilika ujue nimeghafilka ktk uislam sio ktk potwe fulqni ndugu zanguni makundi ya usalafi yanatokana na nn mpaka tutupiqne maneno ikiwa Letu lote liwe moja
Makundi ya Usalafi ni yepi maana mimi siyajui nilichokueleza ndicho ninachokijua labda unielimishe kwayo...?
 
Mie ndugu yangu nakutambua Kama wewe muislam unayefuata kitabu na Sunna sio kuwa wewe salafy
Qur'an na Sunnah hawa wote wanafuata
=Ikhwaan MUSLIMEEN
=Maibadhi
=Shia
=Masufy
=Hawarijii
Je hao wote itafaa kufuatana nao kigezo cha kuwa wanasema ni Waislamu....
 
Makundi ya Usalafi ni yepi maana mimi siyajui nilichokueleza ndicho ninachokijua labda unielimishe kwayo...?
Akhy we tambua mie nduguyo ktk Imani ambaye kinachoniongoza ni kitabu na Sunna hivyo Aya mengine uenda ni tofaut ya kimapokeo na mafuumu mbali mbali ya uelewa wa dini hivyo tustahimiliqne
 
Qur'an na Sunnah hawa wote wanafuata
=Ikhwaan MUSLIMEEN
=Maibadhi
=Shia
=Masufy
=Hawarijii
Je hao wote itafaa kufuatana nao kigezo cha kuwa wanasema ni Waislamu....
Dah shekhe bhas kunakoendea unaweza ukaniitq shia bure hivyo kubwa Allah atuongoze inshaallah
 
Akhy we tambua mie nduguyo ktk Imani ambaye kinachoniongoza ni kitabu na Sunna hivyo Aya mengine uenda ni tofaut ya kimapokeo na mafuumu mbali mbali ya uelewa wa dini hivyo tustahimiliqne
Allahu mustaan yuko mtu anasema kama usemavyo kuwa wewe ni muislam ila anaamini
=Utume unaendelea,
=Yuko anaamini utume kwa Mtume Mohammed Swalallahu aleyh wasalaam hakustahili kupewa yeye.
=Yuko anaamini Qur'an haijakamilika.

Je hawa wote kwako ni sawa kwa kuwa wanasema ni Waislamu
 
Dah shekhe bhas kunakoendea unaweza ukaniitq shia bure hivyo kubwa Allah atuongoze inshaallah
Haaa haaa haaa Allahu mustaan kwani shia si muislam mbona unamtenga ndugu huko si kuvunja umoja katika Uislamu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom