Wanachofanya ni utobu wa adabu wale watu,hata kama wanamazuri yao lakini mabaya yao nao wasemwe pia.
Sio kisa wanajifanya wanakataza bidaa basi waachwe tu hata kama wanakuwa hawana adabu,hapana.
Huyu abdallah humeyd juzijuzi katoka kumuita othman maalim kwamba ni mtu muongo kweli kweli,kisa othman maalim katoa kisa cha nabii mussa ambacho pengine hakikuthibiti.
Anapomuita mtu kama othman maalim kwamba ni muongo tena kwa kejeri na kiburi hiyo ni ishara ya utovu wa nidhamu wake kwa mashekhe wenzie.
Hata kama hawakubaliani katika mambo lakini adabu lazima itangulie,so nahitimisha kwa kusema kwamba genge la kassim mafuta na wenzie achilia mbali faida wanazotoa lakini wana ukosefu mkubwa wa adabu kwa waislamu wenzao.
Upo sahihi sheikh.....Adab tul khitilaf.....kuna masiala ambayo kwamba maulama walikhitalafiana na kuna masiala ambayo kwamba maulama wa madhehebu yeto manne(wahanifa~imam Abu hanifa, wahambaria~imam ahamad ibn hambari, mashafy~imam shafy, malkia~imam malk) walikubaliana
Hivyo kwenye masiala ambayo kwamba yana khilafu ndani yake tukhitalafiane kwa adabu kwa sababu kimsingi hatujaanza kukhitalifiana ummat Muhammad (saw) tulio zama hizi Bali hata wema waliotangulia wamekhitalafiana
Ikiwa hawa wakisema wafuata fahamu za wema waliotangulia hata kundi lile pia lafuata wema waliotangulia
Au wema waliotangulia(salaf) ni kundi lile tu?na kundi lile sio wema wema waliotangulia?
Ikiwa wewe wamfuate imam Ahmad Mimi nikamfuata imam shafy, kwani wote si ni wema waliotangulia jamani??
Inabidi pia tufahamu fahamu za wema waliotangulia tunazozifuata pia wema waliotangulia pia kuna masiala walikhitalafiana
Ama wale wanaosema sisi tufuata dalili (kitabu na sunna) hali ya kuwa wote wafuata dalili kwani hizo dalili wazifuata wao tu wengine hawazifuati dalili
hamna muislam anaemfuata imam(awe ni imam shafy, malk,hamad, Abu hanifa) Bali waislam wote tunamfuata ALLAH na mtume (saw) wake Bali tunaafikiana na (fiqi) au fatwa au jinsi hawa maimam walivyokuwa wakihukumia mambo ya kisheria kwa kufuata kitabu na sunna
Pia nukta nyingine ambayo in shaa Allah ningependa niigusie ni kuwa kukhitalafiana sio kukosana wala uadui wala chuki Bali ni kuwa jawabu tofauti na mwenzako
Mfano kwa madhehebu ya imam shafy swalatul jumaa inaswihi Kama swala itakuwa na waumini wasiopungua 40 Kama sikosei lakini kuna madhehebu inaswihi hata kwa waumin 12
Mola ndio mjuzi siku tukirudi kwake tutajua nani alikuwa karibu na haqi lakini in shaa Allah wote wawe karibu na haqi maana mwenye kujitahidi kwaajili Allah atalipwa
Binafsi nawapenda ndugu wote katika imani na najua wale hawafanyi vile kwa sababu wanadalili zao na wale wafanya vile kwa sabab wanadalili zao na najua masiala ya khilafu yalianza toka kwa maswahaba na hayatoisha sema nikiona kitu nisichokijua huwa najitahidi nijue dalili yake
Binafsi spendelei kumuona muislam akitanguliza itikadi nyingine mbele tofauti na ya karma tawhid hadi ikampelekea kuanza kuwabagua waislam wenzake na kuanza kuwatia waumin katika kufuru...huwa spendi hata kusema wale ni Mara wabakwata Mara answari Mara masalafy sema sometimes inakukuta umefika huko lakini waislam wote ni ndugu jamani tupendane mahaba ya juu pia tuwe na adabu katika kukhitalafiana
Assalam alaykum warahmatullah wabarakatul