MM leo mbona umewaamkia vibaya Chadema? Chadema wamefanya kazi kubwa mno katika nchi hii. Ndio chama kilichoasisi vita dhidi ya ufisadi. Chadema walipeleka hoja za ufisadi Bungeni. Wabunge wa CCM wakamzomea Dr. Slaa. Akishirikiana na wanachama wenzake, hasa Tindu Lisu, wakawataja timu ya watu 11 watuhumiwa wa ufisadi. Chadema pia wamejitahidi kurekebisha kasoro ya kukaa mjini, wanajitatangaza vijijini kupitia operation Sangara.
Chadema pia wamehimili misukosuko ya CCM wakisaidiwa na TLP na hata CUF: rejea wakati wa kifo cha Wangwe. Hata Mpendazoe ambaye amepata nguvu ya kupiga vita ufisadi ni kwa sababu ya kazi iliyoanzishwa na Chadema. Ndio maana ni vema CCJ ishirikiane na Chadema. Taarifa za ufisadi zilizokuwa kwenye mitandao zisingefika kwenye majukwaa ya kisiasa kama isingekuwa ujasiri wa Chadema. Waliuvua ubinafsi wakasema na lolote na liwe. Chadema inamchango mkubwa katika mapambano dhidi ya dhuluma yanayoendelea sasa. Hata mtikisiko katika Bunge baada ya kashfa ya Richmond ni chimbuko la kazi ya Chadema. Leo hii ni hao hao Chadema wanaopambana dhidi ya vipengele vya gharama za uchaguzi vilivyoingizwa mlango wa nyuma baada ya kikao cha Bunge. CUF wako wapi, TLP wako wapi? Je walichofanya si siasa ya uhakika. Haya waliyofanya kwa nini unasema ni hoja za kisomi tu? Kwanza watanzania sasa ni waelewa. Ukiwapelekea hoja nyepesi watakuuliza. Unakumbuka mtoto wa kidato cha pili aliyemuuliza nadhani waziri mkuu- tena kijijini: mnasema tusome tupate ajira, sasa inakuwaje mkuu wa mkoa anarundikiwa vyeo vitatu mtu mmoja, hizo ajira zitapatikana wapi?
Mkuu sasa unakatisha watu tamaa waliofanya kazi inayoonekana kwa watanzania wote. Hatusemi Chadema wamemaliza kazi, la hasha. Kwa raslimali kidogo walizokuwa nazo waendelee kujiimarisha kwenye serikali za mitaa. Nadhani hapa ndiko hoja yako ilikolala. Na ndio maana tunasema CCJ washirikiane na Chadema, waunganisha nguvu ili wawafikie watanzania wengi zaidi hasa wa vijijini.