Ujio wa CCJ: Yote unayotaka kujua

Ujio wa CCJ: Yote unayotaka kujua

CCJ imeundwa ili kuua nguvu ya CHADEMA. Ila chadema iwe imara sana katika mambo kama haya siamini katika chama kama hiki
 
Jana wakati Mh. Fred Mpendazoe akitangaza kujitoa kwenye chama cha CCM alieleza kwamba, nukuu,

"CCJ siyo Chama cha Upinzani bali ni Chama Mbadala"

Nimejaribu kuitafakari kauli hii kwa makini lakini sijapata mantiki yake vizuri. Maswali ninayojiuliza bilas majibu ni haya:

1: Mpendazoe kusema hivyo anamaanisha kwamba vyama vya upinzani vilivyopo havifai au jina la "Upinzani" halifai?

2: CCJ itafanya mambo yanayolandana na ya CCM?

Wana JF mniweke wazi

Chama cha Upinzani ni chama ambacho kiko kwa ajli ya kupinga na kinyume na chama tawala; chama mbadala ni chama ambacho inaweza kutawala badala ya chama kingine. Yaani, kina uwezo wa kutawala wakati wowote. NI sawasawa na Labour na Conservative kule UK au Republican na Democrat huko US.. vyama hivi vinaweza kubadilishana (mbadala) madaraka bila wananchi kuwa na wasiwasi na wananchi wanaweza kukichagua kimoja badala ya kingine.. n.k

Kwa hivyo CCJ inataka kujiweka kwenye mahali pa kuwa mbadala wa CCM. CCM ni chama cha Kibepari wakati CCJ ni chama cha kijamaa! Vina sera tofauti na mitazamo tofauti kabisa..
 
Chama Pekee makini Tanzani ni CHADEMA lakini hakuna cha CCJ sijui nini ni moto wa kifuu tu
 
Chama cha Upinzani ni chama ambacho kiko kwa ajli ya kupinga na kinyume na chama tawala; chama mbadala ni chama ambacho inaweza kutawala badala ya chama kingine. Yaani, kina uwezo wa kutawala wakati wowote. NI sawasawa na Labour na Conservative kule UK au Republican na Democrat huko US.. vyama hivi vinaweza kubadilishana (mbadala) madaraka bila wananchi kuwa na wasiwasi na wananchi wanaweza kukichagua kimoja badala ya kingine.. n.k

Kwa hivyo CCJ inataka kujiweka kwenye mahali pa kuwa mbadala wa CCM. CCM ni chama cha Kibepari wakati CCJ ni chama cha kijamaa! Vina sera tofauti na mitazamo tofauti kabisa..
Sijaelewa sawa sawa ila kuna ajenda nyingine kabisa na pia naona kuna umuhimu mkubwa sana na kuwa makini na chama hiki. Siamini katika mambo ya haraka haraka sana ndio maana nasema ni chama ambacho wamekiunda CCM ili kuua nguvu ya CHADEMA. Siamini katika chama hiki, Ni kheri DP ya Mtikila kuliko chama hiki
 
I will not give all that credit to THEM excluding all others.



Niliuliza hili swali huko nyuma ni vipi vitendo hivyo?



I don't think so.. Chadema ni chama cha kibepari kama ilivyo CCM.



angalia jibu langu hapo juu;



chadema wamepewa nafasi yao na wameshindwa kuitumia mara nyingi.. wamebakia kutoa hoja za kisomi na kuvutia wasomi kwa hoja za kisomi.. so.. I don't know..
MM leo mbona umewaamkia vibaya Chadema? Chadema wamefanya kazi kubwa mno katika nchi hii. Ndio chama kilichoasisi vita dhidi ya ufisadi. Chadema walipeleka hoja za ufisadi Bungeni. Wabunge wa CCM wakamzomea Dr. Slaa. Akishirikiana na wanachama wenzake, hasa Tindu Lisu, wakawataja timu ya watu 11 watuhumiwa wa ufisadi. Chadema pia wamejitahidi kurekebisha kasoro ya kukaa mjini, wanajitatangaza vijijini kupitia operation Sangara.

Chadema pia wamehimili misukosuko ya CCM wakisaidiwa na TLP na hata CUF: rejea wakati wa kifo cha Wangwe. Hata Mpendazoe ambaye amepata nguvu ya kupiga vita ufisadi ni kwa sababu ya kazi iliyoanzishwa na Chadema. Ndio maana ni vema CCJ ishirikiane na Chadema. Taarifa za ufisadi zilizokuwa kwenye mitandao zisingefika kwenye majukwaa ya kisiasa kama isingekuwa ujasiri wa Chadema. Waliuvua ubinafsi wakasema na lolote na liwe. Chadema inamchango mkubwa katika mapambano dhidi ya dhuluma yanayoendelea sasa. Hata mtikisiko katika Bunge baada ya kashfa ya Richmond ni chimbuko la kazi ya Chadema. Leo hii ni hao hao Chadema wanaopambana dhidi ya vipengele vya gharama za uchaguzi vilivyoingizwa mlango wa nyuma baada ya kikao cha Bunge. CUF wako wapi, TLP wako wapi? Je walichofanya si siasa ya uhakika. Haya waliyofanya kwa nini unasema ni hoja za kisomi tu? Kwanza watanzania sasa ni waelewa. Ukiwapelekea hoja nyepesi watakuuliza. Unakumbuka mtoto wa kidato cha pili aliyemuuliza nadhani waziri mkuu- tena kijijini: mnasema tusome tupate ajira, sasa inakuwaje mkuu wa mkoa anarundikiwa vyeo vitatu mtu mmoja, hizo ajira zitapatikana wapi?

Mkuu sasa unakatisha watu tamaa waliofanya kazi inayoonekana kwa watanzania wote. Hatusemi Chadema wamemaliza kazi, la hasha. Kwa raslimali kidogo walizokuwa nazo waendelee kujiimarisha kwenye serikali za mitaa. Nadhani hapa ndiko hoja yako ilikolala. Na ndio maana tunasema CCJ washirikiane na Chadema, waunganisha nguvu ili wawafikie watanzania wengi zaidi hasa wa vijijini.
 
Ingefaa zaidi kama wangetumia upepo uliopo sasa kufanya merger.

Una mawazo mazuri sana. Kweli hili likifanyika basi CCM watapigwa na kiwewe na kuwa na wasiwasi mkubwa katika uchaguzi unaokuja provided hawa jamaa wapya watakuja na sera ambazo zitawafurahisha Watanzania walio wengi kwa kuweka maslahi ya nchi mbele.
 
Nasikia siku hizi kwenye CCM ubunge sio cheo tena, hata Kasheshe hajui Mpendazoea alikuwa na cheo gani!! Nasikia mwingine yupo maelezo anajichomoa, ila yeye hajasema anaenda wapi!!

Kaka samahani nilikuwa najua ana cheo cha wananchi kupitia kwa CCM, ila nilitaka kujua yeye ni mjumbe wa NEC, CC au nini?
 
Alitoka mzee mzima Njelu Kasaka muasisi wa G55, iwe du!!! haya mbunge ambaye hata NEC alikuwa haingii, hapana wakuuu. kwa kweli siione jambo zito la kuongelea hapa.... raha usikie Malecela, Warioba, Sitta, Kinana, Mwakyembe etc... ndio ametoka... hapo .... nitaangalia hiyo thread kila dk. 5.
 
Mimi nafikiri kuwepo na changes za kiungozi katika chama cha CHADEMA ili kiweze kuimarika na kwenda mbele. Nafikiri kungekuwepo na switching ya Katibu na Mwenyekiti, mimi naona Dr. Slaa akiwa mwenyekiti na Mbowe akachukua ukatibu, mambo yatasonga, maana kumeishakuwa na dalili ya matumizi mabaya ya pesa kwa upande wa Mbowe kwa kutumia cheo chake cha Uenyekiti, lakini kwa upeo wa watanzania nafikir wanamuona kama Dr. Slaa ni mtu ambaye anaweza kuongoza nchi kama akipitishwa kugombea uraisi na akashinda, pia upinzani waweza kukubali kushirikiana kumuungania kama mgombea mmoja. Hata Lipumba atampa zote...na CCJ nafikiri nao watakuwa naye pamoja na vya vingine. Lakini Mbowe..kijana safi lakini hizi kasoro ndogo ndogo zinaaacha doa kwenye fikra za wengi.
 
Una maana gani? sentensi yako haieleweki kabisa.

Katika maelezo yako sikuona msisitizo wa moja kwa moja wa kuitaka CCJ ishirikiane na Chadema umetumia neno wapinzani na wapinzani si Chadema lakini ukona bora habari yako isomeke CCJ Washirikiane na Chadema kwa staili ileile ya magazeti yetu Zitto anasurika Kipigo kumbe ni wasafiri wengi nawe badala ya kuitaka CCJ ishirikiane na wapinzani unasema Chadema nadhani nimeeleweka
 
Katika maelezo yako sikuona msisitizo wa moja kwa moja wa kuitaka CCJ ishirikiane na Chadema umetumia neno wapinzani na wapinzani si Chadema lakini ukona bora habari yako isomeke CCJ Washirikiane na Chadema kwa staili ileile ya magazeti yetu Zitto anasurika Kipigo kumbe ni wasafiri wengi nawe badala ya kuitaka CCJ ishirikiane na wapinzani unasema Chadema nadhani nimeeleweka
Soma posts zangu zote katika threah hii utaona msisitizo nilioweka ni CCJ ishirikiane na Chadema. Sikutaja vyama vingine vya siasa, na sababu nimezieleza nilipoulizwa na MM kwa nini ninaona CCJ ishirikiane na Chadema na siyo vyama vingine vya upinzania. Ujumbe uliopo kwenye kichwa cha habari ndio huohuo niliokusudia kwamba CCJ ishirikiane na Chadema.
 
Chama cha Upinzani ni chama ambacho kiko kwa ajli ya kupinga na kinyume na chama tawala; chama mbadala ni chama ambacho inaweza kutawala badala ya chama kingine. Yaani, kina uwezo wa kutawala wakati wowote. NI sawasawa na Labour na Conservative kule UK au Republican na Democrat huko US.. vyama hivi vinaweza kubadilishana (mbadala) madaraka bila wananchi kuwa na wasiwasi na wananchi wanaweza kukichagua kimoja badala ya kingine.. n.k

Kwa hivyo CCJ inataka kujiweka kwenye mahali pa kuwa mbadala wa CCM. CCM ni chama cha Kibepari wakati CCJ ni chama cha kijamaa! Vina sera tofauti na mitazamo tofauti kabisa..


Mwanakijiji

Kauli ya kusema sio 'chama cha upinzani' ni 'chama mbadala' sio ngeni; nakumbuka mwaka 2006 wakati kukiwa na 'upepo wa Kikwete' kwa kiwango cha CCM kutamka kwamba kwa Kikwete kuwa madarakani vyama vya upinzani vitakufa niliwahi kuandika sababu kumi na tatu kwa nini upinzani hautakufa. Wakati huo ilihitaji kufumba macho kumsema Kikwete na serikali yake maana kulikuwa na kundi kubwa la watu katika medani mbalimbali ikiwemo katika vyombo vya habari waliokuwa wamesombwa na 'upepo wa Kikwete'.

Wakati huo nilizungumzia hii dhana ya chama mbadala, naomba nijinukuu "Nianze kwa kuweka bayana kwamba sipendezwi na jina – ‘vyama vya upinzani’. Sisi wanachadema tunapenda kukiita CHADEMA- ‘chama mbadala’. Vyama hivi vinavyoitwa vya upinzani ni vyama ambavyo kwa malengo ya muda mfupi vinalenga kutoa fikra na sera mbadala. Havijaanzishwa kwa ajili ya kupinga tu!. Hivi ni vyama ambavyo kwa malengo ya muda mrefu vinalenga kuchukua dola na kutekeleza misingi na mipango mbadala. Ni serikali zinazosubiri. Sasa je, vyama mbadala vimekufa au vitakufa? Mimi nasema hapana. Vyama mbadala makini havijafa na haviwezi kufa. Labda “vyama magirini”. Mwisho wa kunukuu. (Maelezo zaidi unaweza kuyasoma hapa: http://www.jambonetwork.com/blog/?p=291

Kwa hiyo, maneno ni suala moja. La muhimu ni kutizama vitendo, naamini Karatu nk CHADEMA imeonyesha kufanya kazi kama chama mbadala. Naomba nisitoe maoni wala msimamo wangu wa sasa kuhusu suala la Mpendazoe kuhamia CCJ, ila niseme tu kwamba watanzania na wachambuzi wa mambo wayaangalie mambo kwa kina sana kabla ya kufanya maamuzi. Jambo kubwa ambalo lipaswa kuepukwa katika maamuzi yoyote yatayochukuliwa ni kukubali kusukumwa na upepo ama kuwa bendera ya kufuata upepo. Tunapaswa kuonyesha njia, na sio kuonyesha tu; kuiendea njia, na sio kuiendea bali kuitengeneza njia tunayotaka kama tunataka kwa hakika kufika tunapotaka.

Kauli ambazo zilitolewa na uongozi wa CCJ wakati wakizindua chama chao wiki chache zilizopita juu ya vyama vingine vya upinzani (mbadala) na kauli zinazoendelea kutolewa siamini kama zinatoa dalili njema kwa maana ya mwelekeo wa kudumisha ushindani wa kweli. Lakini nachelea kusijadili kauli hizo kwa sasa, wala kubashiri kwa utimilifu hali ya mambo kwa sasa; kama mtu ataomba maoni yangu kuhusu CCJ basi nitamshauri asubiri kwanza mpaka kitakapopata usajili wa kudumu na kuwa chama shindani cha kuweza kutolewa maoni.

Kwa sasa kwa maoni yangu tunapaswa kujikita katika malengo ya msingi ya kujenga vyama vyenye nguvu mbadala (unaweza kusoma vyama vya upinzani) hususani huko ngazi ya chini kabisa vijijini na mitaani wakati huo huo kuvunja nguvu ya chama dola na kuuporomosha mfumo wa kifisadi. Suala la watu kuchomoka kutoka katika mfumo huo, iwe ni kwenda popote kule litazamwe tu kuwa ni njia mojawapo(one of the means), lakini lisitazamwe kuwa njia kuu(principal/cardinal means) na hatma ya mapambano tunayoyaendesha(the end of our struggle).

Kama tutajikuta tunaingia mtego wa kujikita katika njia moja na kuacha kueneza sera mbadala, kujenga oganizesheni mbadala na kufanya harakati mbadala watakaonasa watatokea wapi?

Kazi ya miaka mingi ya kusimamia uwajibikaji, kutoa dira mbadala na kupambana na mafisadi iheshimiwe na kuendelezwa!

JJ
 
Mimi nafikiri kuwepo na changes za kiungozi katika chama cha CHADEMA ili kiweze kuimarika na kwenda mbele. Nafikiri kungekuwepo na switching ya Katibu na Mwenyekiti, mimi naona Dr. Slaa akiwa mwenyekiti na Mbowe akachukua ukatibu, mambo yatasonga, maana kumeishakuwa na dalili ya matumizi mabaya ya pesa kwa upande wa Mbowe kwa kutumia cheo chake cha Uenyekiti, lakini kwa upeo wa watanzania nafikir wanamuona kama Dr. Slaa ni mtu ambaye anaweza kuongoza nchi kama akipitishwa kugombea uraisi na akashinda, pia upinzani waweza kukubali kushirikiana kumuungania kama mgombea mmoja. Hata Lipumba atampa zote...na CCJ nafikiri nao watakuwa naye pamoja na vya vingine. Lakini Mbowe..kijana safi lakini hizi kasoro ndogo ndogo zinaaacha doa kwenye fikra za wengi.

Nshomile

Asante kwa maoni yako.

Mosi; Suala la Dr Slaa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA au yoyote yule kushika nafasi hiyo kwa sasa tunapoelekea uchaguzi wa mwaka 2010 si kipaumbele kwa sasa kwa kuwa CHADEMA ilishafanya uchaguzi mwaka 2009 na kwa mujibu wa katiba uongozi huo utakaa kwa miaka mitano. Labda yatokee mambo tofauti kabisa ambayo hatuyaombei.

Pili; tuhuma ulizozitoa kuna dalili za matumizi mabaya ya fedha zinazomhusu Mbowe kwa kutumia nafasi yake ya uenyekiti ni vizuri ukazitolea maelezo ya zaida kwa kuzitaja bayana kwa vielelezo kama ambavyo CHADEMA na washirika wake walifanya tulipotoa orodha ya mafisadi: http://www.chadema.or.tz/tamko/tamko.php?id=16. Lakini zingatia kuwa kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA katibu mkuu ndiye muwajibikaji mkuu (Chief accounting officer) inapokuja suala la matumizi ya chama katika shughuli mbalimbali. Kwa kuzingatia hilo, hoja yako ya kwamba Mbowe awe katibu wakati huo huo unamtuhumu kuwa ameshindwa kusimamia fedha inajikanyaga wakati huo huo ukitaka Dr Slaa ambaye unamuamini kwa kusimamia fedha awe Mwenyekiti inajichanganya yenyewe

Tatu, kuhusu maoni yako ya kutaka Dr Slaa ateuliwe kuwa mgombea urais, nashukuru kwa maoni yako ambayo naomba nisiyatolee maoni. Ila naamini kwamba Dr Slaa akipita hapa atasoma maoni yako.

Kwa ujumla hoja yako kuu ni kutaka mabadiliko katika uongozi wa CHADEMA kama msingi wa CHADEMA kwenda mbele; naamini unaweza kuona kwa mifano kwamba toka uchaguzi wa CHADEMA ufanyike Septemba 2009 ni timu hii ya CHADEMA imeendelea kufanya kazi kwa pamoja na kwenda kwa wananchi vijijini kukijenga chama iwe ni kupitia operesheni Sangara ama njia nyingine mathalani wilaya zote za Tanga, wilaya zote za Dodoma na mikoa mingine na bado operesheni hizi zitaendelea maeneo mengine mpaka kieleweke.

Wakati CHADEMA inafanya hivyo, vitazame vyama vingine pia ndio unaweza kutoa hoja vilivyo kama CHADEMA inasonga mbele, inarudi nyuma au iko pale pale.

Baada ya kusema hayo, nisisitize kwamba sisi katika chama tuko wazi kupokea maoni na hoja zenye kujenga, na sio kupokea hoja tu; tunaomba kila mpenda demokrasia na maendeleo popote pale alipo kuchukua hatua ya kuwa sehemu ya mabadiliko anayotaka kuyaona.

Nawatakia mjadala mwema

JJ
 
Alitoka mzee mzima Njelu Kasaka muasisi wa G55, iwe du!!! haya mbunge ambaye hata NEC alikuwa haingii, hapana wakuuu. kwa kweli siione jambo zito la kuongelea hapa.... raha usikie Malecela, Warioba, Sitta, Kinana, Mwakyembe etc... ndio ametoka... hapo .... nitaangalia hiyo thread kila dk. 5.
Hata hivyo hii thread ni tofauti na hoja zako
 
..........................................Wakati huo nilizungumzia hii dhana ya chama mbadala, naomba nijinukuu "Nianze kwa kuweka bayana kwamba sipendezwi na jina – ‘vyama vya upinzani’. Sisi wanachadema tunapenda kukiita CHADEMA- ‘chama mbadala’. Vyama hivi vinavyoitwa vya upinzani ni vyama ambavyo kwa malengo ya muda mfupi vinalenga kutoa fikra na sera mbadala. Havijaanzishwa kwa ajili ya kupinga tu!. Hivi ni vyama ambavyo kwa malengo ya muda mrefu vinalenga kuchukua dola na kutekeleza misingi na mipango mbadala. Ni serikali zinazosubiri. Sasa je, vyama mbadala vimekufa au vitakufa? Mimi nasema hapana. Vyama mbadala makini havijafa na haviwezi kufa. Labda “vyama magirini”. Mwisho wa kunukuu. (Maelezo zaidi unaweza kuyasoma hapa: http://www.jambonetwork.com/blog/?p=291

................................................

nakubaliana na wewe kiongozi kabisa kuwa neno chama mbadala limeasisiwa na chadema na linatumiwa na chadema toka kitambo sasa............... hawa CCJ na mpendazote waowamelidaka tu na kimsingi wamevamia tu siasa za TZ tena nina wasiwasi kama watafaulu kwani wanatumia mitazamo ya kale ya CCM.......... kulekule CCM ilikotoka.................

nawashauri chadema muwe makini sana na mbinu zenu za mapambano........... inaonekana CCJ watakuwa wapinzani wa chadema zaidi na si wa ccm.............. watakuwa mbadala wa chadema zaidi na si wa ccm........ ninukuu vizuri hapo utakumbuka kauli hii siku zijazo................

lakini mnayo fursa nzuri ya kufanya vyema katka uchaguzi huu........... kushiriki kwa CCJ katika uchaguzi huu kutategemea kama maobi yao ya fast tracking ya kupata usajili wa kudumu yatafanikiwa.......... ofisi ya msajili wa vyama vya siasa tayari imeishaonya kuwa ina shughuli nyingi hasa ukizingatia kwa sasa imeanza kazi ya ueleimishaji umma kuhusu sheria mmpya ya gharaman za uchaguzi, kwa kuazia imeanza na mikoa sita na itamalizia awamu hiyo june............. hili linaashiria mabaya kwa maombi ya fast tracking ya CCJ...............

binafsi sina matumaini ya CCJ kushiriki uchaguzi mwaka huu................. ccm haiwezi kuharakisha kusajili mbaya wake ili awanyang'anye wanachama zaidi............ ukitafakari busara iliyoko kwenye uamuzi wa mpendazote utagundua kuwa hiki ni chama chake na ndiye muasisi wake halisi................. tuendelee kutafakari....................

kila la heri katika harakati mkuu............
 
- Wakuu wote JF wasalaam sana, jana niliahidi kupekua kila mahali hapa nyumbani on exactly nini kinaendelea na kinachofanyika, kuhusu hiki chama kipya CCJ yaani the talk of town, toka jana nimekuwa nikihaha kuatufa the dataz kuhusiana na CCJ na niliahidi kwamba nitasema wazi hapa my findings, ni kwamba:-

1. Nimeweza kuthibitisha na ninasema with my clear conscious kwamba CCJ ni for real na ni a very serious political party, chenye nia njema sana na taifa so far na kwamba kikipata registration kitasimamisha mgombea urais, the dataz ni kwamba patawaka moto na inaeleweka tayari huko Magogoni!

2. Nimegundua kwamba ni kweli nyuma yake kina viongozi wengi sana wenye nguvu sana na siasa za sasa za taifa letu.

3. Nimegundua kwamba Mpendazoe, hakuwa kwenye line ya kufukuzwa isipokuwa uzembe wa viongozi wa juu sana katika taifa letu ndio umesababisha "akawaponyoka" kabla hawajamaliza kufikiria what do do with him kwani walishafahamishwa kwamba alikuwa na "mpango" kwa hiyo kwa habari zote za dataz nilizonazo, ninathibitisha kwamba kuondoka kwake jana lilikuwa pigo kubwa sana huko "ndani" na kumeleta mshituko mkubwa sana kwa Wakulu na sasa wanahaha kufuatilia nani wengine wako njiani!

4. The dataz ni kwamba CCJ is so solid kwamba ofisi yake ya HQ ni full funrnished ikiwa na mtambo mmoja wa ajabu sana na wa kwanza Africa nzima, ambao utaweza kuwasajili wanachama wapya papo kwa papo kupitia njia ya Mtandao.

5. Kwamba kadi mpya za CCJ ambayo nimefanikiwa kuinasa mojawapo ukichungulia kwa mbali zina picha ya Mwalimu Baba Wa Taifa, na kwamba Mpendazoe was not in the picture ya the CCJ's master plan, lakini ameamua kwa hiari yake mwenyewe na ni a big plus!

6. Kwamba kuna "mzito" mmoja ambaye kikatiba hahusiki na usajili wa vyama vya siasa, lakini amelishikila faili la usajili wa CCJ kwa siri sana, badala ya kuwepo ofisini kwa Tendwa! na Yes I said it kuna kigogo mmoja amelishikilia faili la CCJ nyumbani kwake na anatembea nalo! kwa leo ninahifadhi jina lake!

- Well samahani sana wakuu kwa sasa naomba nisimame hapa kwanza, upepo ukikaa sawa nitamwaga a lot more na hasa majina ya who is who behind CCJ, yes ninayo yote sasa subira yavuta heri, maana upepo hauko sawa sasa hivi na this CCJ thing!

Respect.


Field Marshall Es! ni Wazee Wa Sauti Ya Umeme!
 
Back
Top Bottom