Uhusiano wa Freeman Mbowe na JK Nyerere

Uhusiano wa Freeman Mbowe na JK Nyerere

Status
Not open for further replies.
Polen, Ndugu zangu, naona tunapoteza muda na nguvu kujadili mambo yasio ya msingi. Labda tuongeze mijadala ya tuongezeje uwajibikaji wa watanzania, tuogezeje tija ya kilimo, mbona elimu mbumbumbu inapamba moto!!

mambo ya huyu mtoto wa nani, kwa nini unataka tuandike jina ni maswala lakini hayaongezi tija au ufanisi, hayaongezi mazao wala kujenga barabara
 
Polen, Ndugu zangu, naona tunapoteza muda na nguvu kujadili mambo yasio ya msingi. Labda tuongeze mijadala ya tuongezeje uwajibikaji wa watanzania, tuogezeje tija ya kilimo, mbona elimu mbumbumbu inapamba moto!

mambo ya huyu mtoto wa nani, kwa nini unataka tuandike jina ni maswala lakini hayaongezi tija au ufanisi, hayaongezi mazao wala kujenga barabara

Ohooo TANU yajenga nchi x2
Ohooo TANU yajenga nchi x2
TANU ah!! TANU yajenga nchi x 4
 
Polen, Ndugu zangu, naona tunapoteza muda na nguvu kujadili mambo yasio ya msingi. Labda tuongeze mijadala ya tuongezeje uwajibikaji wa watanzania, tuogezeje tija ya kilimo, mbona elimu mbumbumbu inapamba moto!

mambo ya huyu mtoto wa nani, kwa nini unataka tuandike jina ni maswala lakini hayaongezi tija au ufanisi, hayaongezi mazao wala kujenga barabara


Bravo moderator!

Hata hivo usiwashangae sana hawa ndugu zetu, ndivo walivo...ndivo walivo...ndivo walivooooooooo...! Kumbuka, mfa maji hakosi kutapatapa! Japo mwisho wake ni bayana na anaujuwa, nao ni kifo baada ya kubugia maji mengi tena machafu!

Kwa mtindo huu usishangae ukiwasikia wasukuma nao wanakuja na mada kuwa, 'Kambalage ni msukuma' kwa vile alizaliwa na baba wa kisukuma wakati ule mama yake kambalage(Nyerere) alipoachika kwa mzee Burito(baba wa kufikia wa Nyerere) kwa kipindi cha miaka mitatu na akaenda kuishi kwa ndugu zake waliokuwa usukumani wilayani Magu kijiji cha Shigala katika jimbo la Busega kwa mheshimiwa Chegeni, wakati ule wa enzi za mkoloni! Ila kulingana na mila za wazanaki na wakurya ni kwamba, mwanamke akishaolewa na kutolewa mahali halafu akaachika, basi wale watoto wote atakaowazaa nje ya ndoa katika kile kipindi chote alichoachika, wote huwa ni 'watoto halali' wa yule 'mwanaume wa kwanza' (mzee Burito for this case)aliyetoa mahali.

Lakini yote hayo ni upuuzi tu kama huo wa akina KEVO na JMUSHI! Usikubali na wala usisumbuke hata kidogo kuumiza kichwa chako kufikiria huo upuuzi wao usiokuwa na tija yoyote kwa watanzania!

Hata kama Mbowe ni mtoto wa kambalage(Nyerere), so what?!

Hata kama kambalage(Nyerere) ni msukuma kwa vile baba yake mzazi ni msukuma, so what?!

NOTE: Habari hii ya baba msukuma wa Nyerere nimeipata toka kwa mke wangu ambaye ni msukuma wa Mwanza wilayani Magu.
 
Bravo moderator!

Hata hivo usiwashangae sana hawa ndugu zetu, ndivo walivo...ndivo walivo...ndivo walivooooooooo...! Kumbuka, mfa maji hakosi kutapatapa! Japo mwisho wake ni bayana na anaujuwa, nao ni kifo baada ya kubugia maji mengi tena machafu!

Kwa mtindo huu usishangae ukiwasikia wasukuma nao wanakuja na mada kuwa, 'Kambalage ni msukuma' kwa vile alizaliwa na baba wa kisukuma wakati ule mama yake kambalage(Nyerere) alipoachika kwa mzee Burito(baba wa kufikia wa Nyerere) kwa kipindi cha miaka mitatu na akaenda kuishi kwa ndugu zake waliokuwa usukumani wilayani Magu kijiji cha Shigala katika jimbo la Busega kwa mheshimiwa Chegeni, wakati ule wa enzi za mkoloni! Ila kulingana na mila za wazanaki na wakurya ni kwamba, mwanamke akishaolewa na kutolewa mahali halafu akaachika, basi wale watoto wote atakaowazaa nje ya ndoa katika kile kipindi chote alichoachika, wote huwa ni 'watoto halali' wa yule 'mwanaume wa kwanza' (mzee Burito for this case)aliyetoa mahali.

Lakini yote hayo ni upuuzi tu kama huo wa akina KEVO na JMUSHI! Usikubali na wala usisumbuke hata kidogo kuumiza kichwa chako kufikiria huo upuuzi wao usiokuwa na tija yoyote kwa watanzania!

Hata kama Mbowe ni mtoto wa kambalage(Nyerere), so what?!

Hata kama kambalage(Nyerere) ni msukuma kwa vile baba yake mzazi ni msukuma, so what?!

NOTE: Habari hii ya baba msukuma wa Nyerere nimeipata toka kwa mke wangu ambaye ni msukuma wa Mwanza wilayani Magu.

Naomba uache unafiki.Suala la JK Nyerere kuwa Msukuma umelileta mwenyewe kwa nini sasa walihoji na kuwaona Kevo na JMushi kama wajinga?Usinge hoji inaonyesha hata wewe una jambo Mtanzania kama wewe uliyekosa mwelekeo kwa kuita wenzako wapuuzi!
 
Mnakumbuka jibu ambalo Mwalimu alimpa mwandishi mmoja wa habari pale Nairobi alipomuuliza hivi: Nasikia ulikuwa/una mpango wa kuiangusha serikali ya Mzee Mwinyi?

Mwalimu akamjibu: Mtu akija akakwambia kwamba mimi( Mwalimu) ndiye nimekuzaa utamkubalia? (Hapa sijanukuu neno kwa neno). Thread hii kwa mtazamo wangu inafanana na swali la mwandishi huyo.
 
Maswali
1.Ni kweli ni mtoto wa Baba wa Taifa?
2.Ni kweli mzee wake ni Mwana CCM wa zamani?
3.Ni kweli kuhusu hizi safari za Butiama?

Ama mwenye lolote lenye kushabihiana na hili.

Tobaaa!!!! mi sipo!!!!
 
Mnakumbuka jibu ambalo Mwalimu alimpa mwandishi mmoja wa habari pale Nairobi alipomuuliza hivi: Nasikia ulikuwa/una mpango wa kuiangusha serikali ya Mzee Mwinyi?
Mwalimu akamjibu: Mtu akija akakwambia kwamba mimi( Mwalimu) ndiye nimekuzaa utamkubalia? (Hapa sijanukuu neno kwa neno). Thread hii kwa mtazamo wangu inafanana na swali la mwandishi huyo.
kwi kwi kwi kwi julius alikuwa na majibu......

Mimi nimesikia Mkuu wa kaya ni mtoto wa Chief marealle......mnabisha?
 
Naomba uache unafiki.Suala la JK Nyerere kuwa Msukuma umelileta mwenyewe kwa nini sasa walihoji na kuwaona Kevo na JMushi kama wajinga?Usinge hoji inaonyesha hata wewe una jambo Mtanzania kama wewe uliyekosa mwelekeo kwa kuita wenzako wapuuzi!

Mkuu CC,

Nililiweka hapa makusudi ili nikuoneshe wewe pamoja na hao wenzako kwamba, madai yote hayo ni upuuzi mtupu, tena ni sumu kali kwa ustawi wa watanzania kama taifa moja. Muachane na story za mbowe na chimbuko lake! Tunamengi ya kujadili hapa kama taifa moja kwa ustawi wa watanzania, na si mbowe na habari zake feki za chimbuko lake feki! Nashukuru kwa vile umenifahamu uzuri!
 
Maswali
1.Ni kweli ni mtoto wa Baba wa Taifa?
2.Ni kweli mzee wake ni Mwana CCM wa zamani?
3.Ni kweli kuhusu hizi safari za Butiama?

Ama mwenye lolote lenye kushabihiana na hili.

Majibu yasiyo rasmi.
1.Yawezekana.Niliwahi kuelezwa na babu yangu(marehemu) ambaye alikuwa mwana CCM.In short alinieleza japo kijuujuu baada ya kugundua mimi ni mpinzani.I hope he was around, ningejaribu kujua zaidi
2.Swali hili linafananafana na la kwanza???
3.Nimewahi kusikia.
Usintie lawamani kevo
 
Mkuu CC,

Nililiweka hapa makusudi ili nikuoneshe wewe pamoja na hao wenzako kwamba, madai yote hayo ni upuuzi mtupu, tena ni sumu kali kwa ustawi wa watanzania kama taifa moja. Muachane na story za mbowe na chimbuko lake! Tunamengi ya kujadili hapa kama taifa moja kwa ustawi wa watanzania na si mbowe na habari feki za chimbuko lake feki! Nashukuru kwa vile umenifahamu uzuri!

Kama huu ni upuuzi mbona bado upo humu.Siunajua ya kwamba kuna bomu litalipuka ndio maana bado upo?
 
Ndugu Kevo, asante kwa kuleta hii fununu hapa:

Mie nilishawahi kusikia hili na zaidi nilisikia kuwa Jakaya Kikwete pia naye ni Mtoto wa Mwalimu Nyerere. Udaku huo unasema hivi: -

Mwalimu alipokwenda kutambikiwa Bagamoyo alipewa mwanamke wa kulala naye hivyo ndio akazaliwa Jakaya. Kuhusu Freeman ni kwamba Mzee Ichikaeli Mbowe alikuwa rafiki mkubwa wa Mwalimu Nyerere na mfadhili mkubwa wa TANU.

Hivyo basi katika urafiki wao ndio Mwalimu aliweza kukutana na mamake Freeman naye akazaliwa.
 
Mzee ICHIKAEL MBOWE alikuwa rafiki na mfadhili wa mwalimu kama alivyokuwa mzee Rupia...kuna uhusiano wa kirafiki kati ya familia hizi... MWALIMU NYERERE NI GOD FATHER [BABA WA UBATIZO KIKRISTO] ...kikristo God Father or mother ni nafasi kubwa sana kwenye maisha ...hawa ni next to your biological parents kikristo ...uhusiano wa Ichikael na mwalimu ulipelekea mwalimu kumzawadia lile jengo ambalo leo ni bilicanas ...that's why lile jengo lipo compound moja na zile ofisi za serikali ..but ni lao...

Nyerere hakupata kuwaamini wachagga kwani walimpa upinzani kuingiza TANU kwa kuwa huyo Marealle tayari alikuwa na mipango tofauti ya kuunda nchi inaitwa KILIMANJARO [Tanga, Kilimanjaro, Arusha] ...mwalimu alitumia mbinu ya utengano kuingiza TANU Kilimanjaro akiwatumia MZEE NSILLO SWAI na MZEE ICHIKAELI MBOWE. Alitumia weakness ya kihistoria ya UFALME WA MOSHI kwa kuwa wakati wa kuchagua mangi mpinzani mkuu wakati wa uchaguzi huo alitokea MACHAME ..alimwitwa CHIFU shangali...SO NDIO kusema wachagga wa Machame ndio waliokuwa rahisi ku rebel against CHIEFDOM ya Marealle ..alifanikiwa..na tangu hapo urafiki wa Nyerere na kina Nsillo Swai, Shangalis na Mbowe [ambao pia ni cousins wa Shangalis uliimarika]

Wakati wote wa utawala wa Nyerere ...alikuwa hapendi kulala ikulu ya Moshi ambayo kabla ilikuwa nyumba ya ufalme wa Kilimanjaro kabla hajaitaifisha ...alikuwa anapenda kurudi kulala ikulu ya Arusha au NYUMBANI KWA MZEE ICHIKAEL MACHAME au nyumba za kanisa ....kwa kuangalia ukaribu wa hawa watu haya maneno yanakuzwa zaidi na hisia kutokana na urafiki wa familia hizi....

Lakini I should say one thing, kwa utamaduni wa watu wa kaskazini ...wachagga, wamasai ets ...mtoto akishazaliwa kwenye boma lako ni kosa la jinai tena lenye faini kubwa sana, mtu yeyote kuthubutu kuinua mdomo na kusema ni wa boma lingine. Mtoto akizaliwa ndani ya boma ni wako ...na hapakuwa na kufananisha mtoto au kupekuwa nasaba... Hayo mambo yamekuja siku hizi ukiotesha mtoto kwa mke wa mtu umesaidia "kanisa" na kamwe hatakuhusu hata kama akija kuwa milionea na watoto wako wa mkeo wakiwa mazezeta.... utaendelea kugugumia rohoni tu na hutakaa uwe na haki naye

Kwa kifupi KIMILA HAKUNA HOJA ZA KIHISIA ZA MTOTO NI WA FLANI, MJI ALIOZALIWA MTOTO NDIO KWAKE.....

Na kunayo siri kubwa kwa kinamama wa zamani wa maeneo haya... walikuwa na tabia ya kufanya mix breed kwenye familia kwa sababu kuu kama:-

Kukinga watoto wake wote wasipate magonjwa ya kurithi ya familia ya mmewe [ie kifafa, kichaa, laana.. etc] kwa hiyo wabibi wa zamani walihakikisha kama akizaa watoto 10 lazima wanne achomeke ...ili hata kama bahati mbaya kama kuna tatizo kwenye ukoo huo haiwapati wote na habari hizi ilikuwa ni haramu kuziongelea, SIRI INABAKI KWA MAMA.....

PIA kulikuwa na SIRI ya wakunga, iwapo bahati mbaya mtoto anazaliwa na mapungufu walimnyonga ili kusaidia wazazi wasije pata taabu wakashindwa kulima au kuchunga ngombe..... hayo ni baadhi tu..

Pia zamani ikiwa bahati mbaya kwenye familia mnaye ndugu asiye rijali lazima aoe ...ukiwa kaka au mdogo wake utamsaidia mbegu na itabaki siri yako kwa maisha yako yote ...hii ilifanyika ili kutunza heshima kwa familia, sidhani kama siku hizi kama bahati mbaya nduguyo ana tatizo atakubali umsaidie...

So kwa kifupi hoja yoyote ya kuanza kusema leo mtoto ni wa nani ni haramu mama zetu wanayo siri kubwa.... naamini hata kina mama wa leo.....
 
kwi kwi kwi kwi julius alikuwa na majibu......

Mimi nimesikia Mkuu wa kaya ni mtoto wa Chief marealle......mnabisha?
Sasa kama hii hisia ya mkuu wa kaya kuwa mtoto wa Marealle ni hisia hizo hizo kwanza wanasema hafanani sana na wandugu zake ambapo as I said kwa wazee wa zamani hiyo ni haramu kuhoji au kupinga uhalali wa mzee Khalfani kuwa baba...

Pili inatokana na utamaduni wa kifalme ulikokuwepo zamani ambapo mfalme alitembelea ufalme mwingine ilikuwa ni lazima kama kuonesha ukarimu ...mfalme amruhusu mfalme mgeni kulala kwenye moja ya matembe [nyumba ya malkia] yanayozunguka boma la ufalme wake. Sasa huyu mfalme wa Kilimanjaro ni kweli alipata kutembela ufalme wa Bagamoyo na kama taratibu za protocol zinavyotakiwa zilifanyika... Lakini kamwe hakuna anayeweza kuthibitisha kama mfalme mgeni aliacha chochote pale ...na wala hakuna ushahidi kuwa aliingia tembe la malkia gani wa Bagamoyo na hata kama ingekuwa kweli, utaratibu ni uleule ......watoto wote ni wa mfalme au mkuu wa boma husika.

Kwa hiyo pia hizo ni hisia za kufikirika!!!
 
Kama huu ni upuuzi mbona bado upo humu.Siunajua ya kwamba kuna bomu litalipuka ndio maana bado upo?

Someone help please; NIKISHAJUA KUWA MBOWE NI MTOTO WA NYERERE SO WHAT?? ukinieleza faida ya kujua hili sambamba na hali yetu ya uchumi , nitashukuru sana.Nikishajua kuwa Jakaya ni mtoto wa sijui nani na si mtoto wa Kikwete then so what? Nikishajua faida za kujua haya nitaiunga mkono kwa nguvu zote hii maada.

BOMU KULIPUKA?? Hivi ikishajulikana kuwa Mbowe ni mtoto Nyerere bomu litalipuka??labda kwa watu 'wale' wangapi wana watoto nje ya ndoa zao? wangapi wanalea watoto sio wao? Nyerere hakuwa mtume wala nabii hakuwa malaika wala shetani.Alikuwa mwanadamu kama wengine.Mwenye hulka, utashi, misukumo na mihemko kama mwingine yeyote! So bomu gani kujua kuwa hawa ni ndugu?Kama ni ishu ya kisiasa kuna formula gani kuwa Mbowe akijulikana kuwa mtoto wa Nyerere atagain popularity? kama sio kumuangamiza?.Maana kwa mtu kama mimi nitaogopa kuwa; nae akishika madaraka atalala na wake za watu!!-like father like son.This is proven facts kuwa tunarithi madhaifu na tunarithisha madhifu yetu.

Someone help

''When speculation has done its worst, two and two still make four"
Samuel Johnson - 1709-1784




Kalenge
 
Jamani msichanganye madesa kuna mdau mwingine kashaliongelea hili, Mbowe na Marealle ni wachaga wa sehemu mbili tofauti kwa msio wachaga mnaweza msilifahamu hili, Mbowe ni mmachame na Marealle ni Mmarangu.

Nina wasiwasi na mtoa mada kama huyu anaitwa Freeman Mbowe, na wewe unasema Nyerere alikuwa na uhusiano wa karibu na Marealle, sasa wapi na wapi? angekua anaitwa Freeman Marealle ndio hoja yako ingekuwa valid, otherwise fikiria kabla ya kusema jambo kama hili, mambo ya kudandia bila kufanya uchunguzi ndio yanatufanya tusitiliwe maanani hata tunapoongelea mambo ya maana.
 
Jamani msichanganye madesa kuna mdau mwingine kashaliongelea hili, Mbowe na Marealle ni wachaga wa sehemu mbili tofauti kwa msio wachaga mnaweza msilifahamu hili, Mbowe ni mmachame na Marealle ni Mmarangu.

Nina wasiwasi na mtoa mada kama huyu anaitwa Freeman Mbowe, na wewe unasema Nyerere alikuwa na uhusiano wa karibu na Marealle, sasa wapi na wapi? angekua anaitwa Freeman Marealle ndio hoja yako ingekuwa valid, otherwise fikiria kabla ya kusema jambo kama hili, mambo ya kudandia bila kufanya uchunguzi ndio yanatufanya tusitiliwe maanani hata tunapoongelea mambo ya maana.

Read between lines ndugu. Mbona uwezo wako wa kufikiri na kuelewa ni finyu kiasi hicho? Nimesema nilipata taarifa hii kutoka kwa ndugu wa Karibu wa Marealle aliyeniambia na siyo Nyerere kuwa na uhusiano na Marealle.

Jamani Watanzania tunasikitisha. Jambo dogo kama hili linakuwa so ambiguous wakati liko so straight forward?
 
Alizidi kutueleza ya kwamba Mzee Mbowe kama member wa CCM alikuwa kikazi mikoa ya Kusini na kipindi hicho Nyerere alikuwa Kilimanjaro kikazi hivyo kama rafiki wa karibu wa familia hii alikaa nyumbani kwa Mzee wa Marealle hivyo uhusiano uliokuwa kati yake na mke wa rafiki yake kupelekea kuzaliwa kwa Freemanna kwamba hata katika mazishi ya Nyerere huyu jamaa alipata nafasi ya pekee kabisa kuweka wreath kwenye kaburi la mzee wake na kwamba ni mara nyingi sana yeye huwa anaenda Butiama.

KEVO??.. don't get it, Nyerere was staying at Marealles house while Mbowe was in kusini ya Tanzania?

Sasa uhusiano kati ya mke wa Mbowe na Nyerere unakuja vipi hapa, from what you wrote Nyerere was staying at Marealle's house, Marealle kama watu wasemavyo alikuwa Marangu, na Mbowe alikuwa anaishi Machame, sasa wapi na wapi, au Nyerere alikuwa akitoka Marangu to Machame then back to Machame during that time.

Kwa kuwa hapa hujasema kama Nyerere alifikia kwa Mbowe bali Marealle, YOU DIG
.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom